10. Kukadiria Umri wa Ujauzito kutoka kwa Kipimo cha Urefu wa Fandasi

Kipindi cha 10 Kukadiria Umri wa Ujauzito kutoka kwa Kipimo cha Urefu wa Fandasi

Utangulizi

Katika kipindi hiki, utajifunza jinsi ya kuchukua kipimo muhimu ambacho kinapaswa kufanywa katika kila safari ya utunzaji katika ujauzito - kupima urefu wa sehemu ya juu ya uterasi ya mama kama njia ya kukadiria ikiwa mtoto wake anakua kikawaida. Tutakufundisha njia mbili za kufanya hivi - kutumia vidole na kutumia chenezo laini. Hii hukuwezesha kukadiria kipindi cha ujauzito wake, na kuchunguza usahihi wa tarehe anapotarajiwa kuzaa ikikokotolewa tangu kipindi cha mwisho cha kawaida cha hedhi cha mama. Kisha tutajadili sababu zinazoweza kuifanya uterasi kukua haraka sana au polepole sana na hatua unazopaswa kuchukua ukishuku kuwa huenda kuna tatizo.

Malengo ya Somo la Kipindi cha 10