14. Masuala ya Uendelezaji wa Afya Katika Ujauzito

Kipindi cha 14 Masuala ya Uendelezaji wa Afya Katika Ujauzito

Utangulizi

Uendelezaji wa afya ni shughuli yoyote inayolenga kutimiza afya bora katika jamii au nchi. Huhusisha elimu ya kiafya kwa watu binafsi ili kuwawezesha kudhibiti na kubadilisha mitindo yao ya kimaisha ili kuboresha afya yao. Hili ndilo lengo kuu la Kipindi hiki katika muktadha wa jukumu lako kama mwalimu wa afya wa wanawake wajawazito katika safari za utunzaji katika ujauzito. Lakini jinsi unavyojua kutoka katika Kipindi cha 2 cha Moduli hii, shughuli za uendelezaji wa afya huenda zaidi ya kulenga mienendo ya mtu binafsi na huhusisha tatuzi anuwai za kijamii na kimazingira zinazoboresha afya na hali njema kwa jamii na vile vile watu binafsi. Uendelezaji wa afya pia huhusisha uzuiaji wa magonjwa - Vitendo vinavyotekelezwa ili kuzuia magonjwa kuendelea, na uchunguzi wa kiafya - utaratibu wa kupima watu binafsi ili kujua ikiwa wamo katika hatari ya kukumbwa na tatizo la kiafya. Uhusiano kati ya uendelezaji afya, elimu ya kiafya, uzuiaji wa magonjwa na uchunguzi wa kiafya umeelezwa katika Picha 2.1 katika Kipindi cha 2.

Utunzaji katika ujauzito (Utunzaji kamili katika ujauzito, Kipindi cha 13) unatoa kiingilio kikuu kwa huduma anuwai za uendelezaji wa afya na uzuiaji wa magonjwa. Ni muhimu kwa wanaotoa utunzaji wa kiafya na wanawake kuongea kuhusu masuala muhimu yanayoathiri afya ya mwanamke na ujauzito wake.

Katika kipindi cha ujauzito, unaweza kuendeleza afya ya wanawake walio chini ya utunzaji wako na afya ya watoto wao kabla na baada ya kuzaliwa kwa kuwaelimisha kina mama kuhusu manufaa ya lishe bora, kupumzika vya kutosha, usafi, upangaji uzazi na unyonyeshaji wa mtoto pasipo kumpa chakula kingine chochote, chanjo na juhudi zingine za uzuiaji wa magonjwa. Lengo lako ni kukuza ufahamu za wanawake kwa masuala haya ili waweze kufanya uamuzi bora unaoathiri matokeo ya ujauzito wao - lakini kamwe usisahau wala kupuuza ugumu utakaowakabili wanawake wengine katika harakati za kuboresha mitindo yao ya kimaisha.

Malengo ya Somo la Kipindi cha 14