15. Kuwashauri Wanawake Wajawazito kuhusu Dalili za Hatari

Kipindi cha 15 Kuwashauri Wanawake Wajawazito kuhusu Dalili za Hatari

Utangulizi

Kipindi hiki kitakupa maarifa ya jinsi ya kuwashauri wanawake wajawazito kuhusu dalili za hatari zinazotokea sana zinazoweza kuwakumba baadhi yao katika ujauzito. Ushauri bora katika lugha wanayoweza kuelewa utawawezesha kujua wanapohitaji kupata usaidizi wa dharura kutoka kwako au katika kituo cha afya ikiwa mojawapo ya dalili hizi itatokea.

Tayari umeelewa tofauti kati ya dalili na ishara katika Kipindi cha 8, na katika Kipindi cha 9 ulijifunza kuhusu ishara na dalili za hatari zinazotokea sana katika ujauzito. Kipindi hiki kitaanza kwa kukueleza kwa kifupi kanuni za kijumla na sehemu maalumu za kuwashauri wanawake wajawazito. Kisha tutatoa muhtasari wa dalili zinazohusiana au zisizohusiana na ujauzito ambazo wanawake wajawazito wanaweza kuhisi au kutambua kulingana na umri wa ujauzito. Baadaye katika kipindi hiki, tutakuelekeza jinsi na unapofaa kuwashauri wanawake wajawazito kwa mujibu wa dalili hizi za hatari, na kusisitiza umuhimu wa kuwahusisha waume/ wenzi wao katika ushauri huu.

Malengo ya Somo la Kipindi 15