19. Magonjwa ya Kihipatensheni ya Ujauzito

Kipindi cha 19 Magonjwa ya Kihipatensheni ya Ujauzito

Utangulizi

Magonjwa ya kihipatensheni ya ujauzito ni mojawapo ya visababishi vitatu vikuu vya maradhi na vifo (pamoja na kutokwa na damu, na maambukizi) kwa kina mama. Mchango wa hipatensheni (shinikizo la juu la damu) kwa vifo na maradhi ya fetasi na watoto wachanga pia ni mkubwa. Magonjwa ya kihipatensheni yanaweza kutatiza hadi asilimia 10 ya ujauzito wote, huku kiwango kikubwa zaidi cha asilimia hiyo kikitokea katika wanawake walio na ujauzito wa kwanza (primigravida). Hipatensheni hufafanuliwa kama shinikizo la damu zaidi ya 140/90mmHg, ambapo nambari ya juu ndiyo shinikizo la sistoli na nambari ya chini ndiyo shinikizo la diastoli.

Shinikizo la damu hupimwa kwa milimita za zebaki (mmHg)kwa sababu vifaa vya kwanza vilikuwa na zebaki.

  • Je, unakumbuka kinachomaanishwa na shinikizo la sistoli na la diastoli?

  • Shinikizo la sistoli ni shinikizo la damu katika mishipa ya damu moyo unaponywea. Shinikizo la diastoli hupimwa moyo unapolegea katikati ya mipigo.

    Mwisho wa jibu

Jukumu kuu la huduma yako ya utunzaji katika ujauzito ni kuwafahamisha wanawake wajawazito kuhusu dalili za hatari za magonjwa ya kihipatensheni, kuchunguza shinikizo lao la damu katika kila safari (ulijifunza jinsi ya kufanya hivi katika Kipindi cha 9), na kufanya utambuzi wa hipatensheni kwa wakati unaofaa na kuwapa rufaa wanawake walioathiriwa mapema iwezekanavyo.

Katika kipindi hiki, utajifunza kuhusu mabadiliko katika mwili wa mwanamke kutokana na hipatensheni na jinsi yanavyoathiri mama na fetasi, uainishaji wa hipatensheni, visababishi vikuu, jinsi ya kutambua aina tofauti, na hatua utakazochukua ili kuzuia matatizo yanayokithiri na hata kifo.

Malengo ya Somo la Kipindi cha 19