22. Kuanzisha matibatu ya udungaji wa viowevu mishipani na kuweka katheta ndani ya mwanamke mjamzito

Kipindi cha 22 Kuanzisha Matibabu ya Kudungia Viowevu Mishipani na Kumwingiza Katheta Mwanamke Mjamzito

Utangulizi

Katika kipindi hiki, utajifunza kuhusu mbinu mbili muhimu za utunzaji wa dharura kwa mwanamke mjamzito:

  • Anayevuja damu (kupoteza damu haraka sana kutoka kwa uterasi) kwa sababu zilizoelezwa katika kipindi cha 20 na 21 au
  • Asiyeweza kukojoa (kupitisha mkojo) kwa sababu ya kizuizi kinachomzuia kukojoa. Kwa kawaida, hii ni kwa sababu shinikizo la mtoto huzuia urethra- neli inayotoa mkojo kutoka kwa kibofu cha mama.

Kipindi hiki ni maandalizi ya mafunzo ya ujuzi wa kiutendaji kuhusu mbinu hizi zote utakazozipata katika kituo cha afya au hospitalini.

Hapa tutakutangulizia vifaa utakavyohitaji, na kukueleza jinsi ya kuanzisha na kudumisha matibabu ya kudungia viowevu mishipani na pia jinsi ya kutia katheta kwenye kibofu cha mama mjamzito. Pia utajifunza jinsi ya kuzingatia utaratibu wa kudhibiti maambukizi unapotumia mbinu hizi.

Kabla ya kutekeleza mbinu yoyote kati ya hizi, hakikisha umemweleza mwanamke kwa lugha anayoelewa yale mtakayofanya na sababu za kuhitaji mbinu zenyewe.

Mfahamishe kuwa, punde tu utakapokamilisha utaratibu huu ni lazima aende katika kituo cha afya cha kiwango cha juu ili apate matibabu zaidi.

Hakikisha kuwa usafiri unatayarishwa unapoandaa matibabu ya kudungia viowevu mishipani wake au kutia katheta kwenye kibofu.

Malengo ya Somo la Kipindi cha 22