2. Kumchunguza Mwanamke aliye katika Leba

Kipindi cha 2 cha Somo Kumchunguza Mwanamke aliye katika Leba

Utangulizi

Katika Kipindi cha kwanza kwenye Moduli hii, ulijifunza kutambua wakati leba halisi imeanza. Ulijifunza pia kuhusu hatua nne za leba na kuhusu miendo afanyayo mtoto anapoendelea kushuka kupitia njia ya uzazi. Katika Kipindi hiki, utajifunza kumchunguza mwanamke ambaye tayari yuko katika leba. Pia utajifunza kuchunguza fetasi na hali yake katika uterasi. Pia utajifunza kuhusu “huduma inayozingatia maslahi ya mwanamke”, yaani huduma inayoheshimu imani na haki zake.

Unapoitwa nyumbani mwa mwanamke au akifika kwenye Kituo chako cha Afya, kwa kawaida leba tayari imeanza. Unapomhudumia mwanamke aliye katika leba kwa mara ya kwanza, ni lazima umchunguze kwa haraka. Amua kuhusu huduma anayohitaji mama aliye katika leba, iwapo atahitaji huduma ya dharura. Ikiwa hana matatizo, chukua historia zaidi ya mwanamke huyo. Tambua habari yoyote inayotokana na historia yake ambayo inaweza kuathiri utaratibu au Malengo ya leba. Mchunguze ili kujua hatua ya leba ambayo amefikia. Kipindi hiki kitakuongezea maarifa ya kufanya uchunguzi na kuchukua habari ya historia; maarifa uliyopata katika Moduli ya Utunzaji wa Kabla ya Kuzaa.

Malengo ya Somo la Kipindi cha 2