1. Utunzaji Baada ya Kuzaa katika Kituo cha Afya na katika Jamii

Kipindi cha 1 Utunzaji baada ya kuzaa katika kituo cha afya na katika Jamii

Utangulizi

Utunzaji wa baada ya kuzaa ni utunzaji anaopewa mama na mtoto wake mchanga mara tu baada ya kuzaa na kwa wiki sita ya kwanza ya maisha (Picha 1.1). Kipindi hiki hudhihirisha kuanzishwa kwa awamu mpya ya maisha ya kifamilia kwa wanawake na wenzi wao na mwanzo wa rekodi ya kiafya maishani mwa watoto wachanga (au watoto waliozaliwa - jina linalotumiwa mara nyingi na madaktari, wauguzi na wakunga).

Ingawa kipindi cha baada ya kuzaa hakina utata kwa wanawake na watoto wengi, utunzaji bora wa baada ya kuzaa pia inahusu kutambua mchepuko wowote dhidi ya upataji nafuu unaotarajiwa baada ya kuzaa, na kutathmini na kutatua ipasavyo kwa wakati ufaao. Ni jambo la kusikitisha kuwa katika nchi nyingi za Sahara ya Afrika chini ya asilimia 37 ya wanawake ndio huzalia kwenye vituo vya afya na chini ya asilimia 10 hupokea utunzaji wowote baada ya kuzaa katika muda wa siku mbili baada ya kuzaa. Kwa hivyo, jukumu lako kama mhudumu wa afya nje ya hospitali ni muhimu katika kuboresha hali hii, kutambua dalili za hatari na kupunguza athari mbaya kwa kina mama na watoto wachanga.

Katika kila nchi barani Afrika, kipindi cha baada ya kuzaa mara nyingi hutambulika kwa vitendo maalumu vya kitamaduni. Kuelewa imani na asasi za kijamii katika jamii yako ni jambo la kimsingi katika kuhakikisha utunzaji bora wa baada ya kuzaa. Katika Kipindi hiki cha kwanza cha somo, utajifunza kuhusu ni kwa nini huduma katika kipindi cha baada ya kuzaa ni muhimu sana na kuhusu umuhimu wa kushiriki na kujihusisha kwa jamii katika kutimiza utunzaji bora wa baada ya kuzaa. Tunatoa muhtasari wa baadhi ya mbinu za uhamasishaji wa jamii kwa kifupi na kujadili jinsi ya kujenga ubia na watu mashuhuri wanaoweza kukusaidia kuwatunza kina mama na watoto wao.

Malengo ya Somo la Kipindi cha 1