2. Puperiamu ya Kawaida

Kipindi cha 2 Puperiamu ya Kawaida

Utangulizi

Katika Kipindi hiki cha somo, utajifunza kuhusu mabadiliko ya kawaida yanayotokea kwa wanawake katika majuma sita ya kwanza baada ya kuzaa. Kipindi hiki cha baada ya kuzaa pia kinajulikana kama puperiamu hasa kwa madaktari, wauguzi na wakunga. Mabadiliko haya huhusisha mchakato wa kawaida wa marekebisho ya kisaikolojia katika kipindi hiki. Je, unakumbuka mabadiliko ya kifiziolojia katika ujauzito uliyojifunza kwenye Kipindi cha 3 cha somo moduli ya Utunzaji katika Ujauzito? Hapa tunalenga urekebishi wa kawaida puperiamu, hasa mabadiliko yanayotokea katika mfumo wa uzazi na mifumo mingine ya mwili.

Wanawake wengine unaowahudumia baada ya kuzaa huenda wasielewe mabadiliko yote wanayoyapitia baada ya kuzaa. Wanaweza kushtuliwa na mabadiliko ambayo ni ya kawaida kabisa au wapuuze dalili ambazo kwa hakika ni za hatari. Wanawake wengine huona kulea mtoto mchanga kuwa jambo la kawaida na rahisi ilhali kwa wengine, jukumu hili ni gumu. Kama mhudumu wa afya anayeihudumia jamii nje ya hospitali, una fursa ya kipekee ya kuwasaidia kina mama na familia zao kustahimili marekebisho hayo katika kipindi cha baada ya kuzaa.

Malengo ya mafunzo ya Kipindi cha 2