3. Puperiamu isiyo ya Kawaida

Kipindi cha 3 Puperiamu isiyo ya Kawaida

Utangulizi

Kama ulivyojifunza katika Kipindi cha 2, puperiamu huendelea vizuri kwa wanawake wengi. Puperiamu ni muda wa angalau wiki 6 baada ya kuzaa, ambapo mawazo hurejea kwa hali ya isiyo ya ujauzito. Hata hivyo, wakati mwingine wanawake hupata matatizo ya kiafya ambazo unapaswa kuyatilia maanani. Unaweza kushughulikia baadhi ya matatizo haya mwenyewe, lakini unaweza kurufaa mengine hospitalini au kwa kituo cha afya kwa utathmini zaidi na matibabu. Maambukizi ni miongoni mwa matatizo maarufu ya puperiamu na kisababishi kikuu cha vifo vya wajawazito Kusini mwa Jangwa la Afrika. Joto jingi mwilini ni dalili kuu na antibiotiki ni tiba kuu. Hatua bora zaidi ya kuzuia maambukizi ni kudumisha usafi na elimusiha wakati wa kuzaa.

Neno ‘postpartum’ linamaanisha ‘baada ya kuzaa na mahusiko yake’.

Matatizo mengine ya kawaida ni kuchelewa kuvuja damu baada ya kuzaa, maambukizi kwa mfumo wa mkojo, shinikizo la juu la damu, na matatizo ya akilini. Katika kipindi hiki, utajifunza kuhusu matatizo yasiyo ya kawaida ambayo yanaweza kutokea wakati wa puperiamu, na mojawapo ya tatizo lisilo la kawaida linalotisha maisha – mvilio ndani ya mshipa wa damu (damu kuganda ndani ya mishipa ambayo huzuia mtiririko wa damu).

Malengo ya Somo la Kipindi cha 3