7. Unyonyeshaji, kanuni ya mfululizo joto na kuwapa ushauri kina Mama walio na virusi vya ukimwi (VVU)

Kipindi cha 7 Unyonyeshaji, kanuni ya mfululizo joto na kuwapa ushauri kina Mama walio na virusi vya ukimwi (VVU)

Utangulizi

Katika kipindi, baada ya kuzaa ushauri kwa mama aliye na mtoto mchanga huangazia mambo mengi, pamoja na yale ambayo yamejadiliwa katika vikao vya somo vya awali. Mambo hayo ni pamoja na uzuiaji wa maambukizi, lishe kwa mama na upangaji uzazi. Katika Kipindi hiki cha somo, tunarejelea kwa undani mada mbili ambazo zimeguziwa hapo mbeleni: jinsi ya kuanza na kudumisha unyonyeshaji bora na jinsi ya kumpatia mtoto joto kwa kutumia kanuni ya mfululizo joto. Sehemu ya kwanza ya Kipindi hiki cha somo kinahusu ulishaji wa mtoto mwenye uzito wa kawaida, afya nzuri na mzima. Halafu tunaangalia ushauri maalum ambayo kina mama walio na VVU wanahitaji kuhusu ulishaji wa watoto walio wazima na wenye uzito wa kawaida. Kipindi cha 8 cha somo kinajadili huduma wa kijumla unaohitajika ili kulisha na kudumisha halijoto wa muda mwilini au uzito wa chini kwa watoto wachanga.

Malengo ya Somo la Kipindi cha 7