Huduma baada ya kuzaa kwa mama inapaswa kukabiliana na mahitaji yake maalum, kuanzia saa moja baada ya kutoka kwa kondo na kuendelea kuwepo kwa wiki sita zinazofuata. Huduma hii ni pamoja na uzuiaji, kugundua mapema na kutibu matatizo, na utoaji wa ushauri kuhusu unyonyeshaji, upangaji uzazi, chanjo, na lishe bora wakati wa ujauzito. Ili kufanya huduma baada ya kuzaa kwa mama iwe ya kawaida, unashauriwa kutumia uchunguzi, ushauri na kadi za kurekodi huduma baada ya kuzaa. Hizi kadi huhakikisha kwamba umepitia hatua zote muhimu katika kila ziara ya nyumbani.
Katika Kipindi hiki cha somo, tutaangazia hasa kwa kimsingi utaratibu wa uchunguzi unayohitaji kufanya ili kuhakikisha kwamba mama anapata nafuu baada ya kuzaa, kimwili na kihisia. Tutakushauri pia jinsi unapaswa kumpa mawaidha juu ya kutunza afya yake na kupata nafuu, kudumisha usafi wa mwili wake ili kupunguza hatari ya maambukizi, na kile anachopaswa kula - hasa anaponyonyesha.
Baada ya Kipindi hiki, unafaa kuwa na uwezo wa:
5.1 Kufafanua na kutumia kwa ufasaha maneno yote muhimu yaliyochapishwa kwa herufi nzito.(Maswali ya Kujitathmini 5.1 na 5.2)
5.2 Kuelezea vipimo vya mwili unavyopaswa kufanya kwa mama aliyezaa baada ya kuzalisha, na katika ziara inayofuatia baadaye, ili kuhakikisha kwamba anapata nafuu vizuri. (Swali la Kujitathmini 5.2)
5.3 Kueleza jinsi utamshauri mama kuhusu lishe bora katika kipindi baada ya kuzaa na ni virutubishi vidogo gani za nyongeza ungempa. (Swali la Kujitathmini 5.2)
5.4 Kuelezea aina za usaidizi utakazompa mama baada ya kuzaa ambayo ungemshawishi mpenzi wake na familia yake kumpa, ikiwa ni pamoja na kutafuta huduma ya mara moja iwapo watagundua kuwepo kwa dalili za hatari. (Swali la Kujitathmini 5.2)
Huduma zinazotolewa mara kwa mara kwa mama wakati wa kipindi baada ya kuzaa hasa zinajumuisha hatua za kuzuia zinazolenga kutambua mapema visababishi vya kawaida vya maradhi kwa kina mama na vifo katika jamii vijijini. Wakati wa kila ziara, baada ya kuzaa, hakikisha kuwa unafanya shughuli zifuatazo za kawaida, hata wakati mama halalamiki kuhusu chochote.
Ulijifunza jinsi ya kuchunguza ishara muhimu katika Kipindi cha 9 cha Moduli ya Utunzaji katika Ujauzito.
Chunguza ishara muhimu kwa mama, yaani, joto lake, kiwango cha mpigo kwa mshipa, na shinikizo la damu, na kuhakikisha kwamba ziko katika kiwango cha kawaida. Mara tu baada ya kuzaliwa, chunguza mipigo yake kwa mshipa na shinikizo la damu angalau mara moja kila saa, na joto lake angalau mara moja katika saa sita za kwanza.
Je, ishara muhimu za kawaida zinapaswa kuwa aje ikiwa mama anaendelea kupata nafuu vizuri tangu wakati wa kuzalisha?
Joto lake linapaswa kuwa karibu na Sentigredi 37; kiwango chake cha mpigo wa mshipa inapaswa kuwa kati ya midundo 60 - 80 kwa dakika moja wakati ametulia; systoli yake ya shinikizo la damu (nambari ya juu, ambayo hupima shinikizo wakati moyo wake unakazika) inapaswa kuwa mmHg 90 - 135, wakati diastoli ya shinikizo la damu yake (nambari ya chini, ambayo hupima shinikizo wakati moyo wake imetulia) inapaswa kuwa 60-85 mmHg.
Mwisho wa jibu
Mpatie mama rufaa ya haraka ambaye anaonyesha dalili ya mshtuko na/au kutokwa na damu baada ya mtoto kuzaliwa.
Ikiwa shinikizo la damu yake iko chini mno na inashuka, na mipigo ya mshipa yake inaenda haraka na inaongezeka, anaelekea kuwa na mshtuko. Huenda kinasababishwa na utokaji wa damu wa kuhatarisha maisha. Kama hakuna dalili ya kutokwa na damu kutoka ukeni, anaweza kuwa anapoteza damu ndani ya mwili.
Gusa (hisi) fumbatio lake kupima mikazo ya uterasi ili kuhakikisha kwamba iko imara. Mara tu baada ya kuzaa, unapaswa kuwa na uwezo wa kuhisi mikazo karibu na kitovu cha mama, na kuteremka chini katika pelvisi yake kwa mwendo wa kasi zaidi kwa wiki mbili zijazo. Chunguza uterasi yake kila baada ya dakika 15 kwa ya masaa mawili ya kwanza baada ya kuzaa na kila dakika 30 kwa saa ya tatu. Ikiwezekana, chunguza kila saa kwa saa tatu zifuatazo. Iwapo uterasi iko ngumu, iwache wakati wa vipimo. Ikiwa utahisi ikiwa laini, sugua fumbatio juu ya uterasi ili uisaidie iwe na mikazo. Mfunze mama kujifanyia hivi (Mchoro 5.1).
Dawa ulizompa mama (kwa mfano, misoprostol au oxytocin) kusaidia kutoa plasenta na kuzuia kuvuja damu pia itasaidia uterasi kupata mikazo. Kwa hivyo hunyonyesha mtoto wake. Mama pia anaweza kuwa na haja ya kukojoa ikiwa kibofu chake cha mkojo kimejaa, kinachosaidia uterasi kujikaza vizuri. Chunguza mikazo ya uterasi katika ziara zote baada ya kipindi cha kuzalisha.

Msaidie mama kujisafisha baada ya kuzaa. Badilisha matandiko yoyote yale chafu na usafishe damu iliyo mwilini mwake. Nawa mikono kwanza na uvae glavu kila mara kabla ya kugusa viungo vya uzazi vya mama, kama ulivyofanya kabla kuzalisha. Hii itamlinda kutokana na bakteria yoyote ambayo inaweza kuwa kwa mikono yako. Safisha viungo vya uzazi vyake kwa utaratibu, kwa kutumia sabuni na maji safi sana na kitambaa safi (Mchoro 5.2). Usitumie kemikali ya kuua viini vya maradhi yoyote ambayo inaweza kuwasha tishu zake zilizonyororo. Osha kuelekea chini, mbali na uke. Kuwa mwangalifu ili usipeleke chochote kutoka mkundu kuelekea ukeni. Hata kipande kidogo cha kinyesi kisichoonekana kinaweza kusababisha maambukizi.
Baada ya kuzalisha, ni kawaida kwa mwanamke kutokwa na damu kiasi sawa na ya hedhi. Damu lazima pia ionekane kama ile ya hedhi - utusitusi, au waridi. Mara ya kwanza, damu hutoka katika mbubujiko mdogo au kumwagika wakati uterasi inakazika, au wakati mama atakapokohoa, kusonga, au kusimama. Baada ya siku mbili hadi tatu, mtiririko unapaswa kupungua na kuwa mchozo mwekundu ulio majimaji zaidi inayojulikana kama lokia (Kipindi cha 2).
Kutokwa na damu nyingi sana ni hatari. Ili kuchunguza utokaji wa damu nyingi katika saa sita za kwanza baada ya kuzalisha, chunguza pedii ya mama mara kwa mara – milimita 500 (karibu vikombe viwili) ya kupoteza damu ni nyingi mno. Ikiwa atalowesha pedii moja kwa saa, inachukuliwa kama kutokwa na damu nyingi. Ikiwa mama anatokwa na damu nyingi, na hauwezi kuizuia, mpeleke hospitalini. Chunguza kwa ishara za mshtuko. Kumbuka kwamba kutokwa na damu baada ya kuzaa ni kisababishi kikubwa cha vifo vya wajawazito na kinaweza kutokea wakati wowote katika kipindi cha huduma baada ya kuzaa - ingawa ni ya kawaida katika siku saba za kwanza.

Tumia mkono ulio na glavu kwa utaratibu kuchunguza viungo vya uzazi vya mama (Mchoro 5.3) kwa miraruko, vibonge vya damu, au hematoma (kutokwa na damu ndani ya ngozi). Ikiwa mwanamke ana mraruko unaohitaji kushonwa, weka shinikizo juu yake kwa dakika 10 kwa kutumia kitambaa safi au pedi na kumrufaa kwa kituo cha afya. Ikiwa mraruko ni mdogo, pengine unaweza kupona bila kushonwa, bora tu iwe imetunzwa kwa safi ili kuzuia maambukizi katika jeraha.
Mweleze apumzike iwezekanavyo na umwambie kuwa hapaswi kupanda juu au kushuka milima yaliyowima. Mtu mwingine anapaswa kufanya kazi za kifamilia za kupika na kusafisha kwa siku chache. Ili apate nafuu haraka, anapaswa pia kula vyakula vingi vyenyewe afya, kuweka sehemu ya viungo vya uzazi viwe safi (kuosha na maji baada ya kutumia choo) na kufunika kwa kitambaa au pedi safi.
Wakati mwingine uterasi hukazika na kuwa ngumu na utokaji wa damu huwa ni kiasi, Ilhali mama bado anahisi kizunguzungu na mdhaifu. Iwapo hii itatokea, anaweza kuwa anatokwa na damu chini ya ngozi ukeni mwake ambapo huitwa hematoma (Kielelezo 5.4). Ngozi katika eneo hili mara nyingi huvimba, huwa na rangi ya utusitusi, nyepesi kwa kudhurika, na nyororo.


Chunguza kama seviksi imechomoza (imeshuka chini kwa ufunguzi wa uke; Mchoro 5.5). Tatizo hili si hatari, na seviksi kwa kawaida hurudi ndani baada ya siku chache. Msaidie mama kuinua nyonga ili iwe juu kuliko kichwa chake. Mwambie afanye mazoezi ya kukaza misuli ya uke na kuta za pelvisi angalau mara nne kwa siku.
Ikiwa seviksi itabaki katika ufunguzi wa uke zaidi ya wiki mbili, anapaswa kupewa rufaa. Seviksi ambayo itakaa ikiwa imechomoza inaweza kutatiza iwapo mama atapata mtoto mwingine

Kibofu cha mkojo kiliojaa kinaweza kusababisha uvujaji wa damu na matatizo mengine. Kibofu cha mkojo kinaweza kuwa kimejaa baada ya kuzaa, lakini anaweza kuwa hana hamu ya kukojoa. Mwambie akojoe katika saa mbili au tatu za kwanza. Ikiwa amechoka sana kwa kuamka na kutembea, anaweza kuchuchumaa kwa bakuli kitandani au sakafuni (Mchoro 5.6). Anaweza pia kukojoa kwa taulo au kitambaa nene wakati amelala chini. Ikiwa hawezi kukojoa, unaweza kumsaidia kwa kumwagia maji safi, iliyo na joto kwa viungo vya uzazi wakati anapojaribu kukojoa.
Ikiwa mama hawezi kukojoa baada ya saa nne, na kibofu chake cha mkojo hakijajaa, anaweza kuwa na upungufu wa maji mwilini. Msaidie anywe viowevu. Ikiwa kibofu chake kimejaa na bado hawezi kukojoa, lazima aingizwe katheta ili kutoa mkojo ulio kwa kibofu cha mkojo wake. Ikiwa umepata mafunzo ya kufanya hivi, tumia katheta kama ilivyoonyeshwa katika Kipindi cha 22 cha Moduli ya Utunzaji katika Ujauzito na masomo yako ya ujuzi tendaji. Kisha mpatie rufaa kwa kituo cha afya au hospitali kilicho karibu.
Je, ni jambo gani muhimu unapaswa kufanya kabla ya kumpima mama ambaye amezaa wakati huo?
Nawa mikono yako vizuri kila wakati ili kupunguza uwezekano wa kupitisha bakteria zinazoweza kuwa kwa mikono. Ikiwa unapima sehemu yake ya viungo vya uzazi, kisha baada ya kunawa mikono, vaa glavu.
Mwisho wa jibu

Kina mama wengi huwa tayari kula mara baada ya kuzaliwa, na ni vizuri kwao kula aina yoyote ya lishe bora wanataka. Ikiwa mama ambaye anazaa mara ya kwanza hahisi njaa, angalau anapaswa kuwa na kitu cha kula. Maji ya matunda au chai atmit ni nzuri kwa sababu itawapa nguvu (Mchoro 5.7). Wanawake wengi hutaka kunywa kitu kilicho na joto, kama chai. Baadhi ya maji ya matunda, kama maji ya machungwa, pia huwa na vitamini C, ambayo inaweza kumsaidia kupata nafuu. (Lakini anapaswa kujiepusha na soda kama Coke, ambayo ina sukari nyingi na kemikali lakini haina lishe.)
Iwapo mama hawezi (au hataweza) kula au kunywa ndani ya saa tatu baada ya kuzaa:
Baada ya kuzaa, ulaji wa mara kwa mara inapaswa kuongezwa ili kurudisha nguvu ya kunyonyesha pamoja na nguvu na afya yake. Anapaswa kula takriban 10% zaidi kuliko kabla awe mjamzito ikiwa hana shughuli nyingi au anafanya kazi yake ya kawaida na takriban 20% zaidi kama yuko na uwezo. Katika hali halisi, anashauriwa kuchukua angalau mlo mmoja au miwili zaidi kila siku. Ushauri wa lishe bora ni pamoja na:
Familia nyingi vijijini hawana uwezo wa kununua chakula cha ziada kwa kina mama ambao wamezaa kwa mara ya kwanza. Kipindi cha 14 katika Moduli ya Utunzaji katika ujauzito kinatoa ushauri kuhusu kula vizuri kwa kutumia pesa kidogo
Mshauri mama kuchukua virutubishi vidogo kuongeza lishe mara kwa mara ili kuzuia matatizo ya upungufu na anemia, kama tutakavyoeleza.

Kuongeza madini ya iodini kwa chumvi huitwa iodination na inapendekezwa utumie chumvi iliyo na iodini kwa upishi katika kipindi baada ya kuzaa, hasa katika maeneo ya nchi ambazo tezi ni ya kawaida kama matokeo ya madini ya iodini kidogo sana katika mlo (Mchoro 5.8). Uongezaji wa madini ya iodini kwa chumvi imeonekana kuwa njia yenye ufanisi mno ya kuzuia upungufu wa iodini. Kutumia mafuta yenye iodini kwa njia ya kunywa au kudungwa sindano inaweza kutumika kama hatua ya muda mfupi katika maeneo endemiki ambapo ni vigumu kupatikana kwa chumvi iliyo na iodini. Mshawishi mama atumie chumvi iliyo na iodini kila siku wakati wa kipindi baada ya kuzaa, kama inapatikana. Hata hivyo, kama tezi inapatikana hapo, mama anaweza kupewa dosi ya mafuta iliyo na iodini baada tu ya kuzaa.
Mshauri mama jinsi ya kuzuia upungufu wa vitamini A, ambayo si tishio tu kwa kuona kwake, lakini pia ni kisababishi kikubwa cha upofu utotoni mwa watoto walionyonyeswa na mama aliye na upungufu wa vitamini A. Vitamini A katika mlo huongezea kinga dhidi ya maambukizi na ni muhimu hasa kwa utengenezaji wa maziwa ya mama yaliyo na virutubishi.
Mshauri mama jinsi ya kuzuia upungufu wa vitamini A, ambayo si tishio tu kwa kuona kwake, lakini pia ni kisababishi kikubwa cha upofu utotoni mwa watoto walionyonyeswa na mama aliye na upungufu wa vitamini A. Vitamini A katika mlo huongezea kinga dhidi ya maambukizi na ni muhimu hasa kwa utengenezaji wa maziwa ya mama yaliyo na virutubishi.
Mboga zilizo na rangi ya manjano kama karoti, matunda ya njano kama maembe, na mboga yenye rangi ya kijani kibichi kama vile mchicha na kabichi huwa na vitamini A nyingi. Vile vile ini, mafuta ya samaki, maziwa, mayai, na siagi.

Mwisho wa jibu
Kumbuka kwamba kipimo cha upeo wa vitamini A kwa wajawazito ni IU 500,000; zaidi ya hapo ni sumu
Mojawapo ya huduma ya kawaida baada ya kuzaa ni kuchunguza kama mama amepata kapsuli ya vitamini A. Kipimo kilichopendekezwa kwa kina mama wanaonyonyesha ni kapsuli moja ya vitamini A, IU 200,000 mara moja baada ya kuzaa au ndani ya wiki sita baada ya kuzaa. Mweleze kwamba vitamini A humsaidia kupata nafuu vizuri na mtoto anapata kupitia maziwa yake. Mweleze iwapo anahisi kichefuchefu au ana maumivu ya kichwa baada ya kutumia kapsuli hii, itaacha baada ya siku kadhaa.
Upungufu wa damu kutoka mwanzo inaweza kuchochewa na madhara ya kuvuja damu kwa mama na ni moja ya kisababishi kikubwa cha vifo vya wajawazito katika kipindi baada ya kuzaa. Shawishi kina mama kula vyakula vilivyo na madini ya ioni (kwa mfano, mboga zilizo na rangi ya kijani kibichi, maharagwe, mbaazi na dengu, kuku na nyama nyekundu, nyama ya ogani kama vile ini na figo, na bidhaa za nafaka nzima), na vyakula ambavyo huongeza ufyonzaji wa ioni (matunda na mboga zilizo na vitamini C). Mshauri kukunywa tembe moja iliyo na miligramu 60 ya ioni na mikrogramu 400 cha folate (folic acid) kila siku kwa muda wa miezi mitatu baada ya kuzaa, na umpatie kiasi kinachotosha kwa miezi mitatu. (Baadhi ya maeneo yanaweza kuwa na tembe zilizo na ioni na folate zikiwa mbalimbali, lakini kipimo ni sawa.) Mshauri kuhifadhi tembe salama pahali ambapo watoto hawawezi kupata kwa urahisi.
Huduma bora ya kawaida baada ya kuzaa kwa mama ni pamoja na kumshauri kuhusu mahitaji yake ya lishe. Je, utamshauri kuhusu nini?
Kwamba lazima aanze kunywa na kula katika masaa machache ya kwanza baada ya kuzaa; kunyonyesha inamaanisha anahitaji kula zaidi (hasa vyakula vyenye protini nyingi); kama yuko katika eneo ambapo tezi yanapatikana, mshawishi yeye kutumia chumvi iliyo na iodini; ukimwelezea umuhimu wa mboga na vyakula vingine ambavyo viko na vitamini A, ioni, au folate.
Mwisho wa jibu
Baada ya kuwasili katika nyumba, jambo la kwanza unahitaji kuhakikisha ni kwamba mama na mtoto hawajatengwa na wanafamilia wengine kwa sababu za kitamaduni. Unaweza kuwa ulitatua tatizo hili wakati wa mazungumzo ya awali na wanafamilia, lakini kila unapomtembelea hakikisha kwamba mama ana usaidizi anayohitaji kutoka kwa jamii na kuwa wanafamilia wanamtembelea mara kwa mara. Ukiwa pamoja na viongozi wa jamii, unapaswa kujaribu kukomesha mazoea ya kutenganisha, kwa kumweka mama aliyezaa na mtoto wake kado na jamii, ikiwa bado hili linatekelezwa katika jamii yako. Badala yake, mshauri mama kuwa kila siku awe karibu na mtu kwa masaa 24 ya kwanza. Washauri wanafamilia kuwasiliana mara kwa mara kila siku wakati wa wiki ya kwanza ili kuchukua hatua haraka iwapo ishara zozote hatari zitatokea katika hali yake.

Mshawishi mwenzake kuwa karibu na mama angalau kwa wiki ya kwanza katika kipindi baada ya kuzaa ili ampatie usaidizi wa kihisia na kumtunza yeye na mtoto (Mchoro 5.9). Katika mazingira ya Afrika, utunzaji wa mama kawaida ni wajibu wa nyanya na/au mama mkwe. Kwa vile tayari wamepitia haya, wako katika hali bora wa kumpatia usaidizi wa kimwili na kihisia kwa mama na mtoto wake. Wanaweza kumwondoa kutoka shughuli za nyumbani za kawaida, ambayo inahitaji kuhamashishwa.
Baadhi ya kina mama hawahisi vizuri kuhusu watoto wachanga (Mchoro 5.10). Kunaweza kuwa na sababu nyingi kwa hii. Mama anaweza kuwa amechoka sana, au ni mgonjwa au anatokwa na damu. Anaweza kuwa hakutaka mtoto, au kuwa na wasiwasi kwamba hawezi kumtunza. Kama ulivyojifunza katika Kipindi cha 3 cha Somo, anaweza kuwa anafadhaika sana: ishara kama hizi ni kama mama anaonekana kuwa na huzuni, utulivu, na hana hamu ya kitu chochote. Pia chunguza ishara zingine za tabia isiyo kuwa ya kawaida ambayo ni tofauti na ile yake ya kawaida.

La kufanya iwapo unajishughulisha na mama kukosa haja na mtoto wake:
Kichaa baada ya kuzaa kinaweza kutisha maisha, hivyo ichukue kama hali ya dharura. Utajifunza zaidi kuhusu kichaa katika Moduli juu ya Magonjwa yasiyo kuwa ya Kuambukiza, Huduma za Dharura, na Afya ya Akili.
Hali hii ni nadra (inayoathiri takribani mmoja kati ya wanawake 1,000), lakini ni kali sana na mama lazima apewe rufaa kwa haraka kwa matibabu maalamu kama anaonyesha dalili yoyote kati ya zifuatazo:
Mhimize mama, mwenzake, na wanafamilia wengine kupata huduma mara moja wakiona dalili yoyote hatari, ikiwa ni kwa hali yake ya kimwili au hisia. Ucheleweshaji ndio sababu kuu ya vifo vya kina mama na wachanga muda tu baada ya kuzaa na ni pamoja na:
Kuwapa motisha mama na familia juu ya kutafuta huduma mapema ndio msingi katika utoaji wa huduma mwafaka baada ya kuzaa. Unapaswa kujaribu kuweka uwezo kwa jamii wa kukabiliana na hali yoyote ya dharura ambayo inaweza kutokea wakati wa kipindi baada ya kuzaa. Hasa, lazima tahadhari itolewe katika kila kijiji kwa kubuni mfumo wa rufaa wa dharura kwa kina mama na wachanga walio kwa hali inayohatarisha maisha.
Katika Kipindi cha 5, umejifunza kwamba:
Sasa kwa kuwa umekamilisha Kipindi hiki cha somo, unaweza kutathmini mafanikio ya matokeo ya kujifunza kwa kujibu maswali yafuatayo. Andika majibu yako katika Shajara yako ya somo na uyajadili na na mkufunzi wako katika mkutano ujao wa Usaidizi kwa Somo. Unaweza kulinganisha majibu yako na Maelezo juu ya Maswali ya Kujitathmini yaliyo mwishoni wa Moduli hii.
Uliwasili kama umechelewa kuzalisha mtoto ambaye alizaliwa masaa mawili kabla ya wewe kufika huko. Utafanya nini?
Mwisho wa jibu
Lishe bora na usaidizi kwa mama baada ya kuzaa ni masuala muhimu ya huduma bora baada ya kuzaa. Kamilisha Jedwali 5.1 ilikuonyesha, kila tatizo katika safu ya kwanza:
| Tatizo au uwezekano walo iwapo halitashugulikiwa | Hatua mama au familia yake inaweza kuchukua ili kumsaidia | Matibabu au hatua zingine unaweza kuchukua |
|---|---|---|
| Tezi (inayosababishwa na upungufu wa madini ya iodini) | ||
| Kutokula au kunywa katika masaa machache ya kwanza | ||
| Ukosefu wa nguvu(kudumisha nguvu wakati wa kunyonyesha) | ||
| Upungufu wa vitamini A | ||
| Anaemia | ||
| Utengwaji wa mama na mtoto | ||
| Kutokuwa na hamu na mtoto | ||
| Usaidizi kwa mama |
| Tatizo au uwezekano wa tatizo | Hatua mama au familia yake wanaweza kuchukua ili kumsaidia | Matibabu au hatua zingine unazoweza kuchukua |
|---|---|---|
| Tezi (inayosababishwa na upungufu wa madini ya iodini) | Matumizi ya chumvi iliyowekwa iodini kwa kupikia | Dozi ya mafuta iliyo wekwa iodini baada ya kuzaa, kama tezi inapatikana kwa urahisi. |
| Kutokula au kunywa katika masaa machache ya kwanza | Mama anapaswa kujaribu na kukumbuka kwamba ni lazima anywe na ale kwa ajili ya afya yake na ya mtoto. | Chunguza kama kuan utokaji wa damu, homa, au ishara zingine za ugonjwa ambazo zinaweza kuwa ndio kiini cha tatizo; mshawishi mama kuzungumza kuhusu vile anajihisi. |
| Ukosefu wa nguvu(kudumisha nguvu wakati wa kunyonyesha) | Kula mara moja au mbili zaidi kwa siku vyakula vyenye protini vingi (nyama, maziwa, mafuta, karanga, na kadhalika) kama inawezekana. | Chunguza kama kuna miiko kuhusu vyakula, zungumza na familia juu ya kuhakikisha mama anakula chakula cha kutosha na kuepukana na kazi ngumu. |
| Upungufu wa vitamini A | Ongezea ulaji wa vitamini A nyingi, mboga na matunda, kwa mfano, karoti, maembe, kabichi, mchicha; pia ule ini, mafuta ya ini ya samaki, maziwa, mayai, na siagi. | Mpatie kapsuli moja ya vitamini A iliyo na IU 200,000 baada ya kuzaa au ndani ya wiki sita za kuzaa; elezea umuhimu wa vyakula vyenye vitamini A. |
| Anaemia | Ongezea ulaji wa mboga na matunda yenye ioni na folate. | Mpatie tembe za kutosha (miligramu 60 ioni na mikrogramu 400 folate) ameze moja kila siku kwa miezi mitatu |
| Utengwaji wa mama na mtoto. | Wanafamilia kukaa na mama na mchanga kutoa ili kuwapa usaidizi, licha ya kanuni za kiutamaduni. | Eleza ni kwa nini mama anahitaji mtu kukaa karibu naye, hasa katika siku saba ya kwanza, wakati kuna hatari kubwa; huduma ya haraka inahitajika iwapo chochote kibaya kitatokezea. |
| Kutokuwa na hamu na mtoto | Familia imtunze na imsaidie zaidi na kuwe na mtu wa kuhudumia mchanga kama kuna haja. | Chunguza kuwepo kwa ugonjwa, kuvuja damu au maambukizi. Zungumza naye. Chunguza kama anasikia sauti, au ‘kuona vitu’. Kama ni hivyo mwelekeze kwa daktari wa akili kwa usaidizi. |
| Usaidizi kwa mama | Mwenzake, nyanya na/au mama mkwe wachukue baadhi ya kazi za nyumbani za kawaida. | Hakikisha kwamba mwenzake na familia wanajua dalili hatari na umuhimu wa kutochelewa kumpeleka mama kwenye kituo cha afya. |
Mwisho wa jibu