Katika Kipindi cha kwanza kwenye Moduli hii, ulijifunza kutambua wakati leba halisi imeanza. Ulijifunza pia kuhusu hatua nne za leba na kuhusu miendo afanyayo mtoto anapoendelea kushuka kupitia njia ya uzazi. Katika Kipindi hiki, utajifunza kumchunguza mwanamke ambaye tayari yuko katika leba. Pia utajifunza kuchunguza fetasi na hali yake katika uterasi. Pia utajifunza kuhusu “huduma inayozingatia maslahi ya mwanamke”, yaani huduma inayoheshimu imani na haki zake.
Unapoitwa nyumbani mwa mwanamke au akifika kwenye Kituo chako cha Afya, kwa kawaida leba tayari imeanza. Unapomhudumia mwanamke aliye katika leba kwa mara ya kwanza, ni lazima umchunguze kwa haraka. Amua kuhusu huduma anayohitaji mama aliye katika leba, iwapo atahitaji huduma ya dharura. Ikiwa hana matatizo, chukua historia zaidi ya mwanamke huyo. Tambua habari yoyote inayotokana na historia yake ambayo inaweza kuathiri utaratibu au Malengo ya leba. Mchunguze ili kujua hatua ya leba ambayo amefikia. Kipindi hiki kitakuongezea maarifa ya kufanya uchunguzi na kuchukua habari ya historia; maarifa uliyopata katika Moduli ya Utunzaji wa Kabla ya Kuzaa.
Baada ya Kipindi hiki utakuwa na uwezo wa:
2.1 Kufasili na kutumia maneno muhimu yaliyochapishwa kwa herufi nzito. (MK 2.5)
2.2 Kueleza jinsi ya kumchunguza kwa haraka mwanamke aliye katika leba. (MK 2.1)
2.3 Kueleza vipengele vya huduma inayozingatia maslahi ya mwanamke wakati wa leba na kuzaa. (MK 2.3)
2.4 Kueleza jinsi ya kuchukua historia ya mwanamke aliye katika awamu ya kwanza ya leba ya kawaida. (MK 2.3)
2.5 Kueleza jinsi ya kupapasa fumbatio la mwanamke aliye katika leba ili kuchunguza ukubwa wa mtoto, hali na kutokezea kwake. (MK 2.2)
2.6 Kueleza jinsi ya kuchunguza uke wa mwanamke aliye katika leba ili kutathmini jinsi leba inavyoendelea. (MK 2.4)
2.7 Kutofautisha kati ya Malengo ya kawaida na yasiyo ya kawaida unapomchunguza mwanamke aliye katika leba. (MK 2.4)
Ukimpokea mwanamke aliye katika leba, chunguza hali yake kwa haraka. Je, anahitaji kufanyiwa rufaa ya dharura ya utunzaji, au leba yake inaendelea kama kawaida?
Usitumie kileo kupanguzia uke!
Mwanamke aliyekuja kwenye Kituo cha Afya anaweza kuwa tayari katika awamu ya pili ya leba. Ikiwa hivyo, mpeleke kochini mara moja kisha umtulize. Ikiwa utamhudumia nyumbani, chagua mahali safi na salama. Tayarisha mapema vifaa unavyohitaji kutumia unapozalisha. Vipange na uviweke tayari.
Vifaa unavyohitaji wakati wa kuzalisha vimeelezwa katika Kipindi cha 3.
Ulijifunza jinsi ya kuanzisha kutoa viowevu vya vena katika Kipindi cha 22 kwenye moduli ya Utunzaji wa Kabla ya Kuzaa na Somo la ujuzi wa kiutendaji.
Iwapo mojawapo ya dalili hizi muhimu au dalili zote hizi zimepita hali ya kawaida, mpatie rufaa kwa dharura hadi kituo cha afya (Mchoro 2.1). Iwapo hali imezidi ile ya kawaida kwa kiwango kikubwa, anza kumwongeza viowevu mwilini. Unafaa kufanya hivi iwapo tu umepewa Somo la kufanya hivyo. Baadaye, mpatie rufaa hadi kwenye kituo cha afya.
Muulize yeye, au mtu aliye naye, kama amewahi kupata dalili zifuatazo, au kama anazo kwa sasa:
Ikiwa kwa sasa mwanamke ana mojawapo ya dalili hizi, chukua hatua zifuatazo mara moja:
Utajifunza jinsi ya kushughulikia leba tata katika vikao vya 8-11 kwenye moduli hii. Utajifunza utaratibu wa kutoa rufaa na unachofaa kufanya ukiwa njiani kuelekea kituo cha afya.
Ulijifunza kuchukua historia ya mwanamke katika Kipindi cha 8 katika moduli ya Utunzaji wa Kabla ya Kuzaa.
Njia mwafaka ya kujua historia ya mwanamke huyu ni kumuuliza. Hata hivyo, unafaa kuwa mwangalifu. Anaweza kuona vigumu kuzungumza nawe kwa mara ya kwanza. Inaweza kuwa vigumu kwake kukweleza kuhusu afya yake ikiwa anaona aibu kuhusu mwili wake au ngono. Ili kumsaidia asiogope, sikiliza kwa makini, mjibu maswali yake, yaweke siri anayokwambia na umhudumie kwa heshima.
Kanuni zinazozingatia maslahi ya mwanamke zimeonyeshwa katika Jedwali 2.1
Ikiwa umemtunza mama huyu wakati wa uchunguzi wa ujauzito, tayari unafahamu habari hii. Ikiwa ni mgeni kwako, nakili jina na umri wake. Umri wake ni muhimu iwapo yeye ni mama mchanga ambaye amepata mimba kwa mara ya kwanza, na aliye chini ya umri wa miaka 18, kama ilivyo mara nyingi katika Afrika.
Ikiwezekana, pia nakili kimo chake, au ukikadiri. Kama yeye ni “mdogo” akilinganishwa na mtoto, anaweza kupata matatizo wakati wa kuzaa. Wakati mwingine kichwa cha mtoto hakiwezi kutoshea kwenye seviksi ndogo.
Utajifunza mengi zaidi kuhusu hali ya “kichwa kutowiana na pelvisi” katika Kipindi cha 9 cha Somo la moduli hii.
Kisha muulize anwani yake, dini na kazi yake na unakili data hii kwenye chati. Mwanamke anaweza kuchagua habari anazotaka kujadili.
Andika dalili kuu anazoonyesha (malalamishi). Ikiwa yuko tayari katika kipindi cha pili cha leba, malalamishi ya kawaida huwa uchungu wa leba (mikazo) na hisia za kusukuma.
Uliza kuhusu idadi ya mimba za awali na watoto (ikiwa wapo) ambao mwanamke huyu amewahi kupata. Pia muulize kuhusu mimba iliyoko sasa. Jedwali 2.2 inakuonyesha jinsi ya kunakili idadi ya mimba na watoto waliozaliwa. Istilahi ya kidesturi ndio iliyotumika hapa. Kipindi cha mimba ni idadi ya wiki ambayo fetusi imeishi kwenye uterasi. Wastani wa idadi za wiki ambayo fetusi huwa imepevuka ni 40. Wiki hizi huhesabiwa kutoka tarehe ya mwisho ya kawaida ya hedhi.
Ugravida ni idadi ya mimba zote za awali, bila kuzingatia Malengo ya mimba hizo. Mimba zilizotoka kwa ghafla au uavyaji kabla ya wiki 28 ya ujauzito pia huhesabiwa.
Usawa ni idadi ya watoto waliozaliwa baada ya wiki 28 za mimba, wakiwemo waliozaliwa hai au wafu.
Baadhi ya wanawake hawajui idadi kamili ya wiki za ujauzito. Ikiwa wanakadiria kuwa walizaa baada ya miezi 7 hivi (wiki 30), ijumuishe katika usawa.
Mwanamke amekuja Kituoni mwako akiwa na leba katika kipindi cha upevu wa mimba. Anakuarifu kwamba amezaa watoto wawili walio hai hapo awali (watoto wote wawili wakiwa katika kipindi cha wiki 40). Pia alizaa mtoto mmoja mfu katika wiki ya 32. Mwanamke huyu pia alikuwa na mimba iliyotoka ghafla katika wiki ya 26. Nakili hesabu ya ugravida na usawa wa mwanamke huyu.
Yeye ni Gravida 5: amewahi kupata watoto 2 + mtoto mmoja mfu katika wiki ya 32 + mimba 1 iliyotoka katika wiki ya 26 + na mimba 1 iliyopo kwa sasa. Yeye ni Para 3: amezaa watoto 2 walio hai + mtoto 1 mfu kama baada ya wiki 28.
Mwisho wa jibu
Muulize tarehe ya kwanza ya kipindi kilichotangulia cha hedhi ya kawaida (TKHK).Ukishapata habari hii, unaweza kukokotoa tarehe ya kuzaa inayotarajiwa na umri wa fetasi. Ukishajua tarehe ya kuzaa inayotarajiwa, unaweza kutambua kama leba imekuja kabla ya wakati, kwa wakati ufaao au imepitisha wakati wa kawaida. Mara nyingi wanawake hawakumbuki TKHK yao. Muulize ni lini alipohisi mtoto akicheza dani yake kwa mara ya kwanza. Mwendo huu huanza takriban wiki 18-20 kwa wanawake primigravida na wiki 16-18 kwa maltipara.
Muulize mteja iwapo kuna dalili zozote hatari alizogundua. (Dalili ni hisia ambazo mtu hupata na anaweza kuzieleza. Ishara ni kitu ambacho mhudumu aliyehitimu pekee hutambua baada ya kufanya uchunguzi.)
Je, unaweza kukumbuka dalili hatari za ujauzito ulizojifunza katika Kipindi cha 17 cha moduli ya Utunzaji katika Ujauzito?
Dalili hatari ni pamoja na kuvuja damu ukeni, (nzito kuzidi damu tetelezi), maumivu ya kichwa mfululizo, kupoteza fahamu, maumivu makali katika epijastriamu na fumbatio. Dalili zingine hatari ni pamoja na kuvuja kwa kiowevu cha amnioni kabla ya leba na utetelezi usio wa kawaida kutoka kwenye uke. Ikiwa mwanamke atalalamika kuwa na mojawapo ya dalili hizi, mpatie rufaa kwa dharura hadi kituoni cha afya kilicho karibu.
Mwisho wa jibu
Ukichunguza mwili wa mwanamke aliye katika leba, zingatia zaidi fumbatio, uke na seviksi. Kumbuka kufanya yafuatayo:
Ukichunguza fumbatio la mwanamke, tathmini ukubwa na umbo lake na kovu.
Kupapasa inamaanisha kuchunguza fumbatio kwa kugusagusa sehemu mahususi kwa mikono yako au kuisongesha kwa njia fulani ukitumia kiwango fulani cha nguvu. Mwambie mwanamke alale chali, akunje miguu yake magotini kisha akanyage kitanda kwa nyayo. Anafaa awe katika hali ya kuweza kuzungushwa. Wakati mwingine inakupasa usimame mbele ya miguu yake kisha upapase fumbatio lake ukielekea kichwani mwake. Wakati mwingine inakupasa usimame nyuma yake ukielekea upande wa miguu yake.Wakati mwingine inakupasa usimame nyuma yake.
Je unaweza kukumbuka umuhimu wa kupapasa mwanamke aliye katika leba? (Umuhimu huu ni sawa na ule wa wakati wa ujauzito. Rejelea moduli ya Utunzaji katika Ujauzito, Kipindi cha 11).
Kupapasa husaidia kutambua ukubwa wa fetasi, jambo ambalo husaidia kuchunguza kutanguliza kwa fetasi, yaani sehemu ya mtoto inayo “tangulia”kwenye seviksi wakati wa kuzaa. Kupapasa pia husaidia kutambua hali ya fetasi katika mwili wa mwanamke. (Kwa mfano, fetasi imeelekea mbele au nyuma?)
Mwisho wa jibu
Aina nne za kupapasa zinajulikana kama manevazaLeopold. Ni sharti uzifanye kwa utaratibu unaofaa.
Kupapasa fandasi ni kugusagusa sehemu ya juu ya uterasi yenye umbo kubwa. (Sehemu hii ya fumbatio huitwa fandasi). Wakati wa utunzaji katika ujauzito, unafaa kupima urefu wa uterasi kutoka kwenye mfupa wa kinena wa mama hadi kwenye fandasi. Linganisha kipimo hiki na umri wa fetasi ili kutambua kama mtoto anakua vyema. Papasa fandasi ya mwanamke aliye katika leba ili kubaini jinsi mtoto anavyolala uterasini. Papasa pande zote za uterasi ukitumia viganja vya mikono yote miwili. Weka vidole vyako pamoja (Mchoro 2.4) Ipapase uterasi ili kutambua kama sehemu ya juu ya uterasi ni gumu na ya duara ama ni nyororo na isiyo na umbo maalum. Ikiwa uterasi ni nyororo na isiyo na umbo maalum na haisukumiki baada ya kuifinya kidogo, basi matako ya mtoto yako kwenye fandasi (Mchoro 2.4) na kichwa “kinaelekea chini.” Hali hii huitwa kutanguliza kichwa. Aina mbali mbali za kutanguliza kichwa zimeelezwa kwenye Kipindi cha 8. Aina inayotokea mara nyingi huitwa kutanguliza veteksi. Mtoto huzaliwa kwa urahisi zaidi ikiwa ametanguliza veteksi.
Ukigusa uterasi na kuhisi umbo gumu la duara kwenye fandasi, basi hicho ni kichwa cha mtoto. Ikiwa leba imeshaanza, mtoto yuko katika hali ya kutanguliza matako. (Katika hali hii, matako ndiyo sehemu inayotangulia.) Inashauriwa kumpa rufaa mwanamke aliye na mtoto ambaye ametanguliza matako, kwa sababu utaratibu wa kuzaa unaweza kuwa mgumu na kuwa katika hatari kubwa ya kuwa na matatizo. Ikiwa utahisi kama fandasi ni “tupu”, mtoto anaweza kuwa amelala kihanamu au kukingama uterasini.
Maneva ya pili husadia kugundua hali ya fetasi: je, mtoto yuko katika hali ya longitudo (sambamba), mshazari (kukingama), au kihanamu (mlalo) uterasini? Hali ya longitudo ni ya kawaida (Michoro 2.4 na 2.5). Pendekeza rufaa ya dharura kwa mwanamke aliye na hali ya kihanam. Haiwezekani mtoto kuzaliwa kupitia ukeni akiwa katika hali hii. Daktari atafanya upasuaji wa kuzaa ili kuzalisha mtoto.
Weka mikono yako kwenye sehemu za kando za katikati ya fumbatio. Sukuma polepole kwa mkono wako mmoja huku ukiimarisha mkono mwingine kushikilia uterasi. Kisha sukuma taratibu kwa mkono mwingine huku ukiimarisha ule wa kwanza. Ukihisi umbo gumu la duara, yaani kichwa cha mtoto katika upande mmoja, na fandasi ni tupu, basi mtoto yuko katika hali ya kihanamu. Mhamishe kwa dharura mama yeyote aliye katika leba na ambaye mtoto yuko katika hali ya kihanamu.
Maneva ya pili pia husaidia kubani kama mtoto ameelekea ndani au nje. Baini kwa kugusa kama umbo ni la kawaida. Ukihisi umbo kubwa nyoofu chini ya mkono mmoja, inawezekana kuwa ni mgongo wa mtoto. Mtoto huyu ameelekea upande wa ndani (Mchoro 2.5a). Ikiwa mtoto ataanza katika hali hii, itakuwa rahisi kwake kufanya miendo sabakuu akizaliwa. Ulijifunza kuhusu miendo hii katika Kipindi cha 1 (Mchoro 1.3). Ukihisi “vibonge” visivyo na umbo maalum, pengine vibonge hivyo ni miguu, magoti, na viwiko vya mtoto. Mtoto huyu ameelekea upande wa nje (Mchoro 2.5b). Ni vigumu zaidi kwa mtoto aliyeanza katika hali kuzunguka anaposhukia ukeni.
Maneva ya tatu husaidia kuthibitisha ulichohisi hapo awali kuhusu hali ya fetasi. Je, mtoto ametanguliza kichwa au matako?
Hali ya kutanguliza kichwa nini?
Katika hali ya kutanguliza kichwa, kichwa cha fetasi huelekea chini huku matako yakiwa kwenye fandasi (upande wa juu wa uterasi)
Mwisho wa jibu
Tazama upande wa miguu ya mwanamke kisha uweke mikono yako katika sehemu ya chini ya fumbatio lake. Tumia vidole kufinya kwa utaratibu ukielekea ndani, juu ya mfupa wa kinena (Mchoro 2.6). Hisi kwa kupapasa sehemu inayaotangulia ikifungamana na seviksi. Ikiwa utahisi umbo gumu na la duara, basi sehemu inayotanguliza ni kichwa. Ikiwa ni laini na isiyo na umbo maalum, mtoto anaweza kuwa ametanguliza matako.
Ulijifunza kuhusu majina ya mielekeo, kama vile juu na chini, katika Kipindi cha 3 cha moduli ya Utunzaji wa Wajawazito kabla ya Kuzaa, Sehemu ya 1.
Tumia maneva hii kuthibithisha ulichohisi katika maneva ya pili. Ikiwa mgongo wa mtoto umeelekea upande wako, basi kisogo chake kinaelekea juu. Kisogo ni sehemu ya nyuma ya fuvu la fetasi, kwa mtoto aliye katika hali ya juu (Mchoro 2.6a). Hali ya juu imeelekea upande wa mbele wa mama. Mtoto anayezaliwa akiwa katika hali ya kisogo kuelekea chini (Mchoro 2.6) anaweza kuwa na ugumu katika wakati wa kuzaliwa.
Maneva ya nne pia huitwa aina ya kushika ya Pawlick. Tumia maneva hii kubaini ikiwa kichwa cha fetasi (katika hali ya kutanguliza kichwa) kimeteremka hadi pelvisi ya mama na kufungamana kwenye seviksi. (Ulijifunza kuhusu kufungamana katika Kipindi cha 1). Ili kukadiria kiwango cha kufungamana kwa kichwa seviksini, shika kichwa cha fetasi kwa vidole vyako (Mchoro 2.7). Ikiwa vidole vyote vitano vinaweza kushika kichwa kikiwa juu kiasi kwenye mfupa wa kinena wa mama, inaashiria kuwa kichwa kingali hakijafungamana seviksini. Ikiwa unaweza kushika kichwa kwa upana wa vidole viwili tu, basi kimefungamana.
Tumia fetoscopu au stethoskopu kusikiliza kima cha mdundo wa moyo punde tubaada ya mkazo. Kusikiliza sauti ndani ya fumbatio huitwa oskatesheni. Katika hatua wazi ya awamu ya kwanza ya leba, hesabu idadi ya midundo ya moyo wa fetasi kwa dakika moja angalau mara moja baada ya kila dakika 30. Katika awamu ya pili ya leba hesabu idadi ya midundo katika kila dakika 5. Ikiwa mdundo wa moyo si wa kawaida, fetasi inaweza kuwa katika matatizo. Hivyo basi, mwagizie mama rufaa hadi katika kituo cha afya kwa dharura, isipokuwa mtoto akiwa karibu kuzaliwa. Kima kisicho cha kawaida cha mdundo wa moyo ni kile kilicho chini ya 120 au zaidi ya 160 kwa dakika kwa muda wa dakika 10 mfululizo. (Utajifunza kuhusu matatizo ya fetasi katika Kipindi cha 4.)
Ili kukadiri marudio na muda wa mikazo, weka mkono wako juu ya fumbatio la mama, ukiuzungusha juu ya fandasi. Utahisi fumbatio likikazana na kuwa gumu. Mama anaweza kupiga kite wakati wa mkazo. Hesabu idadi ya marudio (idadi ya mikazo katika kila dakika 10) na muda (wakati baina ya mikazo ikihesabiwa kwa sekunde). Andika vipimo hivi katika chati inayoitwa patografu. Pia utanakili dalili muhimu za mama na vipimo vya kima mdundo wa moyo wa fetasi. (Ulijifunza kuhusu patografu katika Kipindi cha 4.)
Utachunguza uke kwa sababu zifuatazo:
Kipindi hiki hulenga sababu ya kwanza tu. Sababu hizo zingine za kuchunguza uke zimeelezwa katika vikao vinavyokuja.
Nawa mikono yako vizuri kwa kutumia sabuni na maji safi kwa muda wa dakika mbili. Kisha vaa glavu safi. Mwelezee mama yale unayodhamiria kufanya. Uke huchunguzwa kwa kutumia vidole viwili vilivyovalishwa glavu. Fanya uchunguzi wote unaohitaji kabla haujaondoa vidole ukeni. Baada ya kuviondoa, usivirudishe ukeni tena.
Eleza kwa nini havirudishwi ukeni?
Ukirudisha vidole vyako ukeni unaweza, kusababisha maambukizi.
Mwisho wa jibu.
Usichunguze uke kwa zaidi ya kila saa 4, isipokuwa kuwepo sababu mwafaka kufanya hivyo. (Mfano wa sababu mwafaka ni kuthibitisha ikiwa awamu ya pili ya leba imeanza.)
Mwagize mama alale chali, akunje miguu yake kwenye magoti, aweke nyayo zake bapa na apanue magoti. Safisha pembeni mwa uke kwa utaratibu ukutumia shashi safi iliyotumbukizwa kwenye kiowevu cha antiseptiki. Tenganisha midomo ya uke kwa kutumia vidole viwili vya mkono usio tumika (mkono unaotumika ni ule unaotumia kuandikia). Tumbukiza vidole vyako viwili (kidole cha shahada na cha kati) katika malai ya antiseptiki kisha uviingize ukeni taratibu. Fuata mkondo wa uke, upande wa juu na nyuma. Mwagize mama avute hewa kwa nguvu na ajaribu kutulia. Mwanamke aliyetulia hatatiziki sana na utaratibu huu.
Kupanuka kwa seviksi ni ongezeko la kipenyo cha uwazi wa seviksi, linalokadiriwa kwa sentimita. Kupanuka hufanyika baada ya seviksi kufitika (seviksi inapojitandazia kwenye uterasi, inajulikana kama iliyofitika. Mchoro 1.1) Unapaswa kufanya mazoezi ya kukadiria kwa usahihi kipenyo cha uwazi wa seviksi. Zoezi 2.1 litakusaidia.
Chukua takriban dakika 20 kufanya zoezi hili. Unahitaji kipande cha karatasi gumu au kadi nyembamba, rula, bikari (ya kuchorea duara), penseli na makasi.
Ukirejelea Kipindi cha 1 cha somo, seviksi ina kipenyo kiasi gani wakati leba inapoendelea kutoka (a) hatua fiche hadi hatua wazi katika awamu ya kwanza? (b) hatua wazi katika awamu ya kwanza hadi awamu ya pili?
(a) sentimita 4; (b) sentimita 10 (imepanuka kabisa)
Mwisho wa jibu
Ukadiriaji wa mwisho katika Kipindi hiki ni kuchunguza sehemu ya nje ya uzazi wa mama na pembeni mwa sehemu ya ndani ya uke ili kutambua dalili za hatari.
Katika moduli ya Huduma za baada ya Kuzaa, unajifunza jinsi ya kuweka dawa ya (tetracycline) macho ya mtoto mchanga ili kumkinga kutokana na uwezekano wa maambukizi na viini kutoka kwenye njia ya uzazi.
Ukiona mojawapo ya hizi dalili hatari, mpe mwanamke huyo rufaa hadi kwenye kituo cha afya, isipokuwa wakati mtoto yuko karibu kuzaliwa. Kipindi cha somo kifuatacho kinaelezea jinsi ya kutunza mwanamke aliye katika leba.
Katika Kipindi hiki, umejifunza:
Kwa vile umekamilisha Kipindi hiki, jibu maswali yafuatayo ili kuthibitisha jinsi ulivyotimiza Malengo ya Somo la Kipindi hiki. Andika majibu yako katika shajara yako ya somo kisha uyajadili na mkufunzi wako katika mkutano wa Kipindi kifuatacho. Linganisha majibu yako na Maandishi ya Maswali ya Kujitathmini yaliyo mwishoni mwa moduli hii.
Chukulia kwamba umeitwa nyumbani mwa mwanamke wa umri wa chini aliye katika leba. Ni nini unachofaa kufanya kwa dharura?
Mtathmini mwanamke huyo upesi ili kuamua kama ni lazima kumpa rufaa ya huduma kwa dharura.
Ukiona dalili za dhikisho la fetasi, ikiwa moja wapo ya ishara muhimu zipo katika hali isiyo ya kawaida, au kukiwepo na mojawapo ya dalili hatari, mpe rufaa kwa hapo. (Dalili ya matatizo ya fetasi ni mdundo wa moyo ulio katika hali isiyo ya kawaida.)
Mwisho wa jibu
Umepapasa fumbatio la mwanamke aliye katika leba. Jaza mapengo yaliyo katika Kisanduku 2.1.
Jina la papaso | Sehemu ya fumbatio inayopapaswa | Unachofaa kuchunguza |
---|---|---|
Papaso la fandasi | ||
Mikono ikiwa imewekwa kwenye pande zote za sehemu ya kati ya fumbatio, mkono mmoja ukifuatwa na mwingine ikisumia ndani Ukitazama upande wa miguu, mikono ikiwa upande wa chini ya fumbatio, sukuma juu tu ya mfupa wa kinena, ukielekeza ndani kwa vidole vyako | ||
Iwapo kichwa cha fetasi kimefungamana kwenye seviksi. Ukiweza kushika kichwa kutumia upana wa vidole viwili juu ya mfupa wa kinena cha mama, kichwa kimefungamana. |
Jina la papaso | Sehemu ya fumbatio itakayo papaswa | Cha kuangalia |
---|---|---|
Papaso la fandasi | Mikono ikiwa karibu na sehemu ya juu ya fumbatio ya mama, sukuma vidole vyako ukizungushia fandasi ya uterasi | Hali ya fetasi – Ikiwa iko katika hali ya longitudo (kawaida), mshazari au kukingama |
Papaso la pembeni | Mikono ikiwekwa bapa kwenye sehemu zote mbili za katikati ya fumbatio; mkono wa kwanza ukifuatwa na wa pili kusukuma ndani. | Uaguaji kamili wa mtoto alivyo lala na kama ni ‘kichwa chini’ au kutanguliza tako |
Papaso la ndani zaidi la pelvisi | Tazama kuelekea miguu ya mama, mikono ikiwa upande wa chini ya fumbatio lake, sukuma ndani kwa vidole juu ya mfupa wa kinena kidogo. | Ili kuhakikisha hali ya kichwa (kichwa chini) kutanguliza kichwa au (chini kabisa) kitangulizi |
Mshiko wa Pawlick | Vidole vinashikilia kichwa cha fetasi juu ya mfupa wa kinena kidogo. | Kama kichwa cha fetasi kimefungamana na seviksi. Ikiwa Unaweza kushika kichwa kwa upana wa vidole juu ya mfupa wa kinena wa mama, kichwa kimefungamana. |
Mwisho wa jibu
Makeda ametembelea Kituo chako cha Afya. Umemchunguza upesi kisha ukabaini kuwa hatahitaji rufaa ya dharura. Sasa unachukua historia yake. Utachukua vipi historia yake na ni habari gani unayofaa kupata kutoka kwake?
(a) Ili kuchukua historia ya Makeda, mhimize kuwa na uwazi wa kuzungumza nawe. Fuata kanuni za utunzaji mwafaka kwa mwanamke unapomuuliza maswali. Sikiza kwa makini, jibu maswali yake na uweke siri anayokufichulia. (Tazama Ksanduku 2.1 ili kupata maelezo kuhusu huduma mwafaka kwa mwanamke.)
(b) Ujumbe unaohitaji kutoka kwa Makeda:
Mwisho wa jibu
Sasa umepata historia ya Makeda na unataka kumchunguza. Je, utafanya nini kwanza na ni nini unachochunguza?
Kabla ya kumchunguza ukeni, fuata kanuni za utunzaji mwafaka wa mwanamke na umwakikishie Makeda kuhusu siri zake. Kisha nawa mikono kabisa na uvae glavu mpya. Chunguza yafuatayo wakati unapochunguza:
Mwisho wa jibu
Ni maelezo gani yasiyo ya kweli? Katika kila kauli, eleza lisilo la kweli.
Mwisho wa jibu