Skip to main content
Printable page generated Tuesday, 23 April 2024, 2:52 PM
Use 'Print preview' to check the number of pages and printer settings.
Print functionality varies between browsers.
Unless otherwise stated, copyright © 2024 The Open University, all rights reserved.
Printable page generated Tuesday, 23 April 2024, 2:52 PM

2. Kumchunguza Mwanamke aliye katika Leba

Kipindi cha 2 cha Somo Kumchunguza Mwanamke aliye katika Leba

Utangulizi

Katika Kipindi cha kwanza kwenye Moduli hii, ulijifunza kutambua wakati leba halisi imeanza. Ulijifunza pia kuhusu hatua nne za leba na kuhusu miendo afanyayo mtoto anapoendelea kushuka kupitia njia ya uzazi. Katika Kipindi hiki, utajifunza kumchunguza mwanamke ambaye tayari yuko katika leba. Pia utajifunza kuchunguza fetasi na hali yake katika uterasi. Pia utajifunza kuhusu “huduma inayozingatia maslahi ya mwanamke”, yaani huduma inayoheshimu imani na haki zake.

Unapoitwa nyumbani mwa mwanamke au akifika kwenye Kituo chako cha Afya, kwa kawaida leba tayari imeanza. Unapomhudumia mwanamke aliye katika leba kwa mara ya kwanza, ni lazima umchunguze kwa haraka. Amua kuhusu huduma anayohitaji mama aliye katika leba, iwapo atahitaji huduma ya dharura. Ikiwa hana matatizo, chukua historia zaidi ya mwanamke huyo. Tambua habari yoyote inayotokana na historia yake ambayo inaweza kuathiri utaratibu au Malengo ya leba. Mchunguze ili kujua hatua ya leba ambayo amefikia. Kipindi hiki kitakuongezea maarifa ya kufanya uchunguzi na kuchukua habari ya historia; maarifa uliyopata katika Moduli ya Utunzaji wa Kabla ya Kuzaa.

Malengo ya Somo la Kipindi cha 2

Baada ya Kipindi hiki utakuwa na uwezo wa:

2.1 Kufasili na kutumia maneno muhimu yaliyochapishwa kwa herufi nzito. (MK 2.5)

2.2 Kueleza jinsi ya kumchunguza kwa haraka mwanamke aliye katika leba. (MK 2.1)

2.3 Kueleza vipengele vya huduma inayozingatia maslahi ya mwanamke wakati wa leba na kuzaa. (MK 2.3)

2.4 Kueleza jinsi ya kuchukua historia ya mwanamke aliye katika awamu ya kwanza ya leba ya kawaida. (MK 2.3)

2.5 Kueleza jinsi ya kupapasa fumbatio la mwanamke aliye katika leba ili kuchunguza ukubwa wa mtoto, hali na kutokezea kwake. (MK 2.2)

2.6 Kueleza jinsi ya kuchunguza uke wa mwanamke aliye katika leba ili kutathmini jinsi leba inavyoendelea. (MK 2.4)

2.7 Kutofautisha kati ya Malengo ya kawaida na yasiyo ya kawaida unapomchunguza mwanamke aliye katika leba. (MK 2.4)

2.1 Mchunguze kwa haraka mwanamke aliye katika leba

Ukimpokea mwanamke aliye katika leba, chunguza hali yake kwa haraka. Je, anahitaji kufanyiwa rufaa ya dharura ya utunzaji, au leba yake inaendelea kama kawaida?

2.1.1 Hatua za uchunguzi wa haraka

Unahitaji kukusanya:
  • Kadi yake ya huduma ya kabla ya kuzaa, ikiwa ulimhudumia hapo awali. Ikiwa ni mgeni kwako na tayari yuko katika leba, mwanzishie rekodi mpya ya afya.
  • Patografu ili kurekodi jinsi leba inavyoendelea. (Utajifunza jinsi ya kutumia patografu katika Kipindi cha 4.)
  • Glavu zilizotiwa dawa ya kuua vimelea.
  • Fetoskopu ya kusikiza jinsi moyo wa mtoto unavyodunda.
  • Themometa ya kupima kiwango cha joto la mama.
  • Saa au kipima muda kingine ili kisaidie kupima mdundo wa moyo wa fetasi na kiwango cha mpwito wa ateri za mama.
  • Sijafu ya kupimia shinikizo la damu kwa stethoskopu.
  • Swabu ya kusafisha msamba wa mwanamke kabla ya kumchunguza. [Tumia mipira 3-4 ya shashi iliyotiwa kwenye mchanganyiko wa antiseptiki kama vile savlon (chlorhexidene 2 -4%.] Ikiwa hauna kiowevu cha antiseptiki, tayarisha maji vuguvugu na sabuni.

Usitumie kileo kupanguzia uke!

Mwanamke aliyekuja kwenye Kituo cha Afya anaweza kuwa tayari katika awamu ya pili ya leba. Ikiwa hivyo, mpeleke kochini mara moja kisha umtulize. Ikiwa utamhudumia nyumbani, chagua mahali safi na salama. Tayarisha mapema vifaa unavyohitaji kutumia unapozalisha. Vipange na uviweke tayari.

Vifaa unavyohitaji wakati wa kuzalisha vimeelezwa katika Kipindi cha 3.

Chunguza dalili kuu
  • Shinikizo la damu: vipimo vya kawaida ni kati ya vipimo 90/60 hadi chini ya 140/90.
  • Kiwango cha mpwito wa ateri za mama: kiwango cha kawaida ni midundo 80-100 kwa dakika kwa mwanamke aliye katika leba. Kiwango kilicho juu ni midundo 110 kwa dakika.
  • Kiwangojoto cha mwili: wastani wa nyusi 37. Ikiwa kipo kati ya nyusi 37.5 - 38.4, mwanamke huyo ana homa ndogo. Ikiwa ni nyusi 38.5 au zaidi, ana homa kuu.

Ulijifunza jinsi ya kuanzisha kutoa viowevu vya vena katika Kipindi cha 22 kwenye moduli ya Utunzaji wa Kabla ya Kuzaa na Somo la ujuzi wa kiutendaji.

Iwapo mojawapo ya dalili hizi muhimu au dalili zote hizi zimepita hali ya kawaida, mpatie rufaa kwa dharura hadi kituo cha afya (Mchoro 2.1). Iwapo hali imezidi ile ya kawaida kwa kiwango kikubwa, anza kumwongeza viowevu mwilini. Unafaa kufanya hivi iwapo tu umepewa Somo la kufanya hivyo. Baadaye, mpatie rufaa hadi kwenye kituo cha afya.

Mchoro 2.1 Mpe rufaa kwa haraka mwanamke mwenye ishara muhimu zisizo za kawaida.
Mtazame na umsikize mwanamke huyu
  • Je, alibebwa alipokuwa akiletwa katika kituo cha afya?
  • Kuna damu kwenye nguo yake au sakafuni chini yake?
  • Je, anakoroma, kupiga kite ama kuinamisha kichwa?
Mchoro 2.2 Ikiwa mama anavuja damu kwa wingi, anahitaji usaidizi wa dharura.

Muulize yeye, au mtu aliye naye, kama amewahi kupata dalili zifuatazo, au kama anazo kwa sasa:

  • Kuvuja damu kutoka ukeni
  • Maumivu makali ya kichwa au kuona uluwiluwi
  • Mitukutiko ya mwili au kukosa fahamu
  • Matatizo ya kupumua
  • Homa
  • Maumivu makali ya fumbatio
  • Kuvuja kwa kiowevu cha amnioni kabla ya wakati (maji kuvunjika kabla ya wakati).

Ikiwa kwa sasa mwanamke ana mojawapo ya dalili hizi, chukua hatua zifuatazo mara moja:

  • Paza sauti kuomba usaidizi.
  • Tulia na uweke makini yako kwa mwanamke huyo.
  • Kaa naye wala usimwache pekee.
  • Mpe kwa haraka huduma zinazohitajika kabla ya rufaa kisha umfanyie rufaa hadi kwenye kituo cha afya kilicho karibu.

Utajifunza jinsi ya kushughulikia leba tata katika vikao vya 8-11 kwenye moduli hii. Utajifunza utaratibu wa kutoa rufaa na unachofaa kufanya ukiwa njiani kuelekea kituo cha afya.

2.2 Chukua historia ya mwanamke aliye katika leba

Ulijifunza kuchukua historia ya mwanamke katika Kipindi cha 8 katika moduli ya Utunzaji wa Kabla ya Kuzaa.

Njia mwafaka ya kujua historia ya mwanamke huyu ni kumuuliza. Hata hivyo, unafaa kuwa mwangalifu. Anaweza kuona vigumu kuzungumza nawe kwa mara ya kwanza. Inaweza kuwa vigumu kwake kukweleza kuhusu afya yake ikiwa anaona aibu kuhusu mwili wake au ngono. Ili kumsaidia asiogope, sikiliza kwa makini, mjibu maswali yake, yaweke siri anayokwambia na umhudumie kwa heshima.

2.2.1 Umuhimu wa huduma inayozingatia maslahi ya mwanamke

Kanuni zinazozingatia maslahi ya mwanamke zimeonyeshwa katika Jedwali 2.1

Kisanduku 2.1 Huduma inayozingatia maslahi ya mwanamke aliye katika leba na kuzaa
  1. Kuwezesha kutolea huduma iliyo bora kwa mwanamke na ina viashirio vifuatavyo:
    • Huzingatia imani, tamaduni na desturi zake
    • Hutilia maanani hali ya mwanamke huyu ya kihisia, kisaikolojia na kijamii.
    • Huwezesha ushauri mwafaka.
  2. Kumhimiza mwanamke, na yeyote ambaye angependa kuwa naye wakati wa leba. Wote huhusika katika utunzaji wake. Jukumu lako ni kuwafunza jinsi ya kumtunza na kuwaelimisha wote kuhusu yale yote yanayoendelea.
  3. Kutilia maanani na kuheshimu haki za mwanamke:
    • Haki yake ya kuarifiwa kuhusu afya yake na ya mtoto.
    • Haki yake ya kuarifiwa kuhusu utaratibu wa leba na kuzaa na anachotarajia leba inapoendelea.
    • Haki yake ya kukubali au kukataa kufanyiwa uchunguzi na huduma zingine.
  4. Kuwahimiza wahudumu wote wa afya kutumia ustadi wa uhusiano mwema na kuwasiliana kikamilifu kwa lugha ambayo mwanamke anaweza kuelewa.

2.2.2 Nakili data kuhusu demografia ya jamii.

Ikiwa umemtunza mama huyu wakati wa uchunguzi wa ujauzito, tayari unafahamu habari hii. Ikiwa ni mgeni kwako, nakili jina na umri wake. Umri wake ni muhimu iwapo yeye ni mama mchanga ambaye amepata mimba kwa mara ya kwanza, na aliye chini ya umri wa miaka 18, kama ilivyo mara nyingi katika Afrika.

Ikiwezekana, pia nakili kimo chake, au ukikadiri. Kama yeye ni “mdogo” akilinganishwa na mtoto, anaweza kupata matatizo wakati wa kuzaa. Wakati mwingine kichwa cha mtoto hakiwezi kutoshea kwenye seviksi ndogo.

Utajifunza mengi zaidi kuhusu hali ya “kichwa kutowiana na pelvisi” katika Kipindi cha 9 cha Somo la moduli hii.

Kisha muulize anwani yake, dini na kazi yake na unakili data hii kwenye chati. Mwanamke anaweza kuchagua habari anazotaka kujadili.

Andika dalili kuu anazoonyesha (malalamishi). Ikiwa yuko tayari katika kipindi cha pili cha leba, malalamishi ya kawaida huwa uchungu wa leba (mikazo) na hisia za kusukuma.

2.2.3 Historia ya ujauzito uliopo na uliopita

Uliza kuhusu idadi ya mimba za awali na watoto (ikiwa wapo) ambao mwanamke huyu amewahi kupata. Pia muulize kuhusu mimba iliyoko sasa. Jedwali 2.2 inakuonyesha jinsi ya kunakili idadi ya mimba na watoto waliozaliwa. Istilahi ya kidesturi ndio iliyotumika hapa. Kipindi cha mimba ni idadi ya wiki ambayo fetusi imeishi kwenye uterasi. Wastani wa idadi za wiki ambayo fetusi huwa imepevuka ni 40. Wiki hizi huhesabiwa kutoka tarehe ya mwisho ya kawaida ya hedhi.

Kisanduku 2.2 Hali ya ugravida na usawa

Ugravida ni idadi ya mimba zote za awali, bila kuzingatia Malengo ya mimba hizo. Mimba zilizotoka kwa ghafla au uavyaji kabla ya wiki 28 ya ujauzito pia huhesabiwa.

  • Gravida 1 ama primigravida: mimba ya kwanza
  • Gravida 2: mimba ya pili, na kadhalika
  • Maltigravida: kuwa mjamzito mara 2 au zaidi (idadi kamili haionyeshwi)

Usawa ni idadi ya watoto waliozaliwa baada ya wiki 28 za mimba, wakiwemo waliozaliwa hai au wafu.

Baadhi ya wanawake hawajui idadi kamili ya wiki za ujauzito. Ikiwa wanakadiria kuwa walizaa baada ya miezi 7 hivi (wiki 30), ijumuishe katika usawa.

  • Nulipara ama Para 0: hakuna mimba yoyote iliyofikia wiki 28.
  • Primipara ama Para 1: mtoto mmoja baada ya wiki 28
  • Para 2: Watoto wawili baada ya wiki 28
  • Maltipara: watoto wawili au saidi baada ya wiki 28.
  • Maltipara kuu: watoto watano au zaidi baada ya wiki 28.
  • Mwanamke amekuja Kituoni mwako akiwa na leba katika kipindi cha upevu wa mimba. Anakuarifu kwamba amezaa watoto wawili walio hai hapo awali (watoto wote wawili wakiwa katika kipindi cha wiki 40). Pia alizaa mtoto mmoja mfu katika wiki ya 32. Mwanamke huyu pia alikuwa na mimba iliyotoka ghafla katika wiki ya 26. Nakili hesabu ya ugravida na usawa wa mwanamke huyu.

  • Yeye ni Gravida 5: amewahi kupata watoto 2 + mtoto mmoja mfu katika wiki ya 32 + mimba 1 iliyotoka katika wiki ya 26 + na mimba 1 iliyopo kwa sasa. Yeye ni Para 3: amezaa watoto 2 walio hai + mtoto 1 mfu kama baada ya wiki 28.

    Mwisho wa jibu

Kukadiria tarehe ya kuzaa inayotarajiwa

Muulize tarehe ya kwanza ya kipindi kilichotangulia cha hedhi ya kawaida (TKHK).Ukishapata habari hii, unaweza kukokotoa tarehe ya kuzaa inayotarajiwa na umri wa fetasi. Ukishajua tarehe ya kuzaa inayotarajiwa, unaweza kutambua kama leba imekuja kabla ya wakati, kwa wakati ufaao au imepitisha wakati wa kawaida. Mara nyingi wanawake hawakumbuki TKHK yao. Muulize ni lini alipohisi mtoto akicheza dani yake kwa mara ya kwanza. Mwendo huu huanza takriban wiki 18-20 kwa wanawake primigravida na wiki 16-18 kwa maltipara.

2.2.4 Dalili na ishara hatari

Muulize mteja iwapo kuna dalili zozote hatari alizogundua. (Dalili ni hisia ambazo mtu hupata na anaweza kuzieleza. Ishara ni kitu ambacho mhudumu aliyehitimu pekee hutambua baada ya kufanya uchunguzi.)

  • Je, unaweza kukumbuka dalili hatari za ujauzito ulizojifunza katika Kipindi cha 17 cha moduli ya Utunzaji katika Ujauzito?

  • Dalili hatari ni pamoja na kuvuja damu ukeni, (nzito kuzidi damu tetelezi), maumivu ya kichwa mfululizo, kupoteza fahamu, maumivu makali katika epijastriamu na fumbatio. Dalili zingine hatari ni pamoja na kuvuja kwa kiowevu cha amnioni kabla ya leba na utetelezi usio wa kawaida kutoka kwenye uke. Ikiwa mwanamke atalalamika kuwa na mojawapo ya dalili hizi, mpatie rufaa kwa dharura hadi kituoni cha afya kilicho karibu.

    Mwisho wa jibu

2.3 Uchunguzi wa mwili wakati wa leba

Ukichunguza mwili wa mwanamke aliye katika leba, zingatia zaidi fumbatio, uke na seviksi. Kumbuka kufanya yafuatayo:

  • Dumisha siri
  • Zingatia kanuni za huduma inayozingatia maslahi ya mwanamke (Kisanduku 2.1)
  • Mchunguze kutoka kichwa hadi miguuni
  • Tambua iwapo ana dalili za anemia (kuparara dani ya vikawa vya macho, kucha za vidole na ufizi.
  • Tambua iwapo ana rangi ya manjano machoni (umanjano). Rangi hii huashiria ugonjwa wa ini.

2.3.1 Kuchunguza fumbatio

Ukichunguza fumbatio la mwanamke, tathmini ukubwa na umbo lake na kovu.

  • Ukubwa: Je, fumbatio lake ni kubwa sana au dogo sana ukilinganisha na umri wa fetasi? Ikiwa fumbatio lake ni dogo sana, inawezekana kuwa mtoto hajakua ipasavyo. Ikiwa ni kubwa sana, mwanamke anaweza kuwa na mapacha au hali inayoitwa polihidramniosi (uwepo wa kiowevu kingi cha amnioni). Ikiwa fumbatio ni kubwa au dogo sana, mpatie rufaa mwanamke hadi kwenye kituo cha afya.
  • Umbo: Je fumbatio lake lina umbo la yai, yaani pana kidogo katika sehemu ya juu ya uterasi na lembamba kwenye sehemu ya chini? Kuelekea kileleni mwa ujauzito, umbo hili huonyesha kwamba mtoto anatanguliza kichwa. Ikiwa fumbatio lina umbo la duara kama mpira, inaweza kuwa ishara kuwa mtoto yuko katika hali mbaya ndani ya uterasi. (Utajifunza kuhusu haya hapa na katika Kipindi cha 8)
  • Kovu: Je, mwanamke yuko na kovu katika sehemu ya chini ya uterasi kutokana na upasuaji wa awali (Mchoro 2.3)? Kwa kawaida, kovu hili huwa juu ya mfupa wa kinena. Uterasi inaweza kupasuka wakati wa kuzaa ikiwa ina kovu. (Utajifunza haya katika Kipindi cha 10).
Mchoro 2.3 Upasuaji wa awali unaongeza hatari katika leba ijayo.

2.3.2 Kuchunguza kwa kupapasa fumbatio

Kupapasa inamaanisha kuchunguza fumbatio kwa kugusagusa sehemu mahususi kwa mikono yako au kuisongesha kwa njia fulani ukitumia kiwango fulani cha nguvu. Mwambie mwanamke alale chali, akunje miguu yake magotini kisha akanyage kitanda kwa nyayo. Anafaa awe katika hali ya kuweza kuzungushwa. Wakati mwingine inakupasa usimame mbele ya miguu yake kisha upapase fumbatio lake ukielekea kichwani mwake. Wakati mwingine inakupasa usimame nyuma yake ukielekea upande wa miguu yake.Wakati mwingine inakupasa usimame nyuma yake.

  • Je unaweza kukumbuka umuhimu wa kupapasa mwanamke aliye katika leba? (Umuhimu huu ni sawa na ule wa wakati wa ujauzito. Rejelea moduli ya Utunzaji katika Ujauzito, Kipindi cha 11).

  • Kupapasa husaidia kutambua ukubwa wa fetasi, jambo ambalo husaidia kuchunguza kutanguliza kwa fetasi, yaani sehemu ya mtoto inayo “tangulia”kwenye seviksi wakati wa kuzaa. Kupapasa pia husaidia kutambua hali ya fetasi katika mwili wa mwanamke. (Kwa mfano, fetasi imeelekea mbele au nyuma?)

    Mwisho wa jibu

Aina nne za kupapasa zinajulikana kama manevazaLeopold. Ni sharti uzifanye kwa utaratibu unaofaa.

Maneva ya kwanza yaLeopold - Kupapasa fandasi

Kupapasa fandasi ni kugusagusa sehemu ya juu ya uterasi yenye umbo kubwa. (Sehemu hii ya fumbatio huitwa fandasi). Wakati wa utunzaji katika ujauzito, unafaa kupima urefu wa uterasi kutoka kwenye mfupa wa kinena wa mama hadi kwenye fandasi. Linganisha kipimo hiki na umri wa fetasi ili kutambua kama mtoto anakua vyema. Papasa fandasi ya mwanamke aliye katika leba ili kubaini jinsi mtoto anavyolala uterasini. Papasa pande zote za uterasi ukitumia viganja vya mikono yote miwili. Weka vidole vyako pamoja (Mchoro 2.4) Ipapase uterasi ili kutambua kama sehemu ya juu ya uterasi ni gumu na ya duara ama ni nyororo na isiyo na umbo maalum. Ikiwa uterasi ni nyororo na isiyo na umbo maalum na haisukumiki baada ya kuifinya kidogo, basi matako ya mtoto yako kwenye fandasi (Mchoro 2.4) na kichwa “kinaelekea chini.” Hali hii huitwa kutanguliza kichwa. Aina mbali mbali za kutanguliza kichwa zimeelezwa kwenye Kipindi cha 8. Aina inayotokea mara nyingi huitwa kutanguliza veteksi. Mtoto huzaliwa kwa urahisi zaidi ikiwa ametanguliza veteksi.

Mchoro 2.4 Kupapasa fandasi – maneva ya kwanza. Mtoto ametanguliza kichwa (Rejeleo: Shirika la Afya Duniani, 2008, Managing Prolonged and Obstructed Labour, Figure 7.4, page 115)

Ukigusa uterasi na kuhisi umbo gumu la duara kwenye fandasi, basi hicho ni kichwa cha mtoto. Ikiwa leba imeshaanza, mtoto yuko katika hali ya kutanguliza matako. (Katika hali hii, matako ndiyo sehemu inayotangulia.) Inashauriwa kumpa rufaa mwanamke aliye na mtoto ambaye ametanguliza matako, kwa sababu utaratibu wa kuzaa unaweza kuwa mgumu na kuwa katika hatari kubwa ya kuwa na matatizo. Ikiwa utahisi kama fandasi ni “tupu”, mtoto anaweza kuwa amelala kihanamu au kukingama uterasini.

Maneva ya pili ya Leopold: kupapasa pembeni

Maneva ya pili husadia kugundua hali ya fetasi: je, mtoto yuko katika hali ya longitudo (sambamba), mshazari (kukingama), au kihanamu (mlalo) uterasini? Hali ya longitudo ni ya kawaida (Michoro 2.4 na 2.5). Pendekeza rufaa ya dharura kwa mwanamke aliye na hali ya kihanam. Haiwezekani mtoto kuzaliwa kupitia ukeni akiwa katika hali hii. Daktari atafanya upasuaji wa kuzaa ili kuzalisha mtoto.

Mchoro 2.5 Kupapasa pembeni – maneva ya pili.(a) Sehemu ya nyuma ya fetasi imeelekea upande wa mbele wa mama. (b) Sehemu ya nyuma ya fetasi imeelekea upande wa nyuma wa mama. (Rejeleo: Shirika la Afya Duniani, 2008, Managing Prolonged and Obstructed Labour, Figures 7.4 and 7.5, pages 115 and 116)

Weka mikono yako kwenye sehemu za kando za katikati ya fumbatio. Sukuma polepole kwa mkono wako mmoja huku ukiimarisha mkono mwingine kushikilia uterasi. Kisha sukuma taratibu kwa mkono mwingine huku ukiimarisha ule wa kwanza. Ukihisi umbo gumu la duara, yaani kichwa cha mtoto katika upande mmoja, na fandasi ni tupu, basi mtoto yuko katika hali ya kihanamu. Mhamishe kwa dharura mama yeyote aliye katika leba na ambaye mtoto yuko katika hali ya kihanamu.

Maneva ya pili pia husaidia kubani kama mtoto ameelekea ndani au nje. Baini kwa kugusa kama umbo ni la kawaida. Ukihisi umbo kubwa nyoofu chini ya mkono mmoja, inawezekana kuwa ni mgongo wa mtoto. Mtoto huyu ameelekea upande wa ndani (Mchoro 2.5a). Ikiwa mtoto ataanza katika hali hii, itakuwa rahisi kwake kufanya miendo sabakuu akizaliwa. Ulijifunza kuhusu miendo hii katika Kipindi cha 1 (Mchoro 1.3). Ukihisi “vibonge” visivyo na umbo maalum, pengine vibonge hivyo ni miguu, magoti, na viwiko vya mtoto. Mtoto huyu ameelekea upande wa nje (Mchoro 2.5b). Ni vigumu zaidi kwa mtoto aliyeanza katika hali kuzunguka anaposhukia ukeni.

Maneva ya Leopold ya tatu: kupapasa nyonga kwa ndani

Maneva ya tatu husaidia kuthibitisha ulichohisi hapo awali kuhusu hali ya fetasi. Je, mtoto ametanguliza kichwa au matako?

  • Hali ya kutanguliza kichwa nini?

  • Katika hali ya kutanguliza kichwa, kichwa cha fetasi huelekea chini huku matako yakiwa kwenye fandasi (upande wa juu wa uterasi)

    Mwisho wa jibu

Tazama upande wa miguu ya mwanamke kisha uweke mikono yako katika sehemu ya chini ya fumbatio lake. Tumia vidole kufinya kwa utaratibu ukielekea ndani, juu ya mfupa wa kinena (Mchoro 2.6). Hisi kwa kupapasa sehemu inayaotangulia ikifungamana na seviksi. Ikiwa utahisi umbo gumu na la duara, basi sehemu inayotanguliza ni kichwa. Ikiwa ni laini na isiyo na umbo maalum, mtoto anaweza kuwa ametanguliza matako.

Mchoro 2.6 Kupapasa pelvisi kiundani. Maneva ya tatu husaidia kubaini sehemu inayotanguliza. Watoto hawa wote wametanguliza kichwa, lakini (a) yuko na kisogo kinachoelekea juu, na (b) yuko na kisogo kilichoelekea chini. (Rejeleo: Shirika la Afya Duniani, 2008, kama kwenye Mchoro wa 2.5)

Ulijifunza kuhusu majina ya mielekeo, kama vile juu na chini, katika Kipindi cha 3 cha moduli ya Utunzaji wa Wajawazito kabla ya Kuzaa, Sehemu ya 1.

Tumia maneva hii kuthibithisha ulichohisi katika maneva ya pili. Ikiwa mgongo wa mtoto umeelekea upande wako, basi kisogo chake kinaelekea juu. Kisogo ni sehemu ya nyuma ya fuvu la fetasi, kwa mtoto aliye katika hali ya juu (Mchoro 2.6a). Hali ya juu imeelekea upande wa mbele wa mama. Mtoto anayezaliwa akiwa katika hali ya kisogo kuelekea chini (Mchoro 2.6) anaweza kuwa na ugumu katika wakati wa kuzaliwa.

Maneva ya nne ya Leopold: Mshikamano wa Pawlick

Maneva ya nne pia huitwa aina ya kushika ya Pawlick. Tumia maneva hii kubaini ikiwa kichwa cha fetasi (katika hali ya kutanguliza kichwa) kimeteremka hadi pelvisi ya mama na kufungamana kwenye seviksi. (Ulijifunza kuhusu kufungamana katika Kipindi cha 1). Ili kukadiria kiwango cha kufungamana kwa kichwa seviksini, shika kichwa cha fetasi kwa vidole vyako (Mchoro 2.7). Ikiwa vidole vyote vitano vinaweza kushika kichwa kikiwa juu kiasi kwenye mfupa wa kinena wa mama, inaashiria kuwa kichwa kingali hakijafungamana seviksini. Ikiwa unaweza kushika kichwa kwa upana wa vidole viwili tu, basi kimefungamana.

Mchoro 2.7 Aina ya kushika ya Pawlick– maneva ya nne husaidia kubaini kama sehemu inayotanguliza imefungamana. (Rejeleo: Shirika la Afya Duniani, 2008 kama katika Mchoro 2.4)

2.3.3 Kupima kima cha mdundo moyo

Tumia fetoscopu au stethoskopu kusikiliza kima cha mdundo wa moyo punde tubaada ya mkazo. Kusikiliza sauti ndani ya fumbatio huitwa oskatesheni. Katika hatua wazi ya awamu ya kwanza ya leba, hesabu idadi ya midundo ya moyo wa fetasi kwa dakika moja angalau mara moja baada ya kila dakika 30. Katika awamu ya pili ya leba hesabu idadi ya midundo katika kila dakika 5. Ikiwa mdundo wa moyo si wa kawaida, fetasi inaweza kuwa katika matatizo. Hivyo basi, mwagizie mama rufaa hadi katika kituo cha afya kwa dharura, isipokuwa mtoto akiwa karibu kuzaliwa. Kima kisicho cha kawaida cha mdundo wa moyo ni kile kilicho chini ya 120 au zaidi ya 160 kwa dakika kwa muda wa dakika 10 mfululizo. (Utajifunza kuhusu matatizo ya fetasi katika Kipindi cha 4.)

2.3.4 Kukadiria mikazo

Ili kukadiri marudio na muda wa mikazo, weka mkono wako juu ya fumbatio la mama, ukiuzungusha juu ya fandasi. Utahisi fumbatio likikazana na kuwa gumu. Mama anaweza kupiga kite wakati wa mkazo. Hesabu idadi ya marudio (idadi ya mikazo katika kila dakika 10) na muda (wakati baina ya mikazo ikihesabiwa kwa sekunde). Andika vipimo hivi katika chati inayoitwa patografu. Pia utanakili dalili muhimu za mama na vipimo vya kima mdundo wa moyo wa fetasi. (Ulijifunza kuhusu patografu katika Kipindi cha 4.)

2.3.5 Kuchunguza uke

Utachunguza uke kwa sababu zifuatazo:

  • Kubaini ikiwa leba halisi imeanza na awamu iliyofikia. Seviksi imepanuka kiasi gani?
  • Kukadiria jinsi leba inavyoendelea. Je, upesi wa kupanuka kwa seviksi ni gani na fetasi imeshuka umbali upi katika uzazi?
  • Kutambua sehemu ya fetasi inayotangulia na hali ya fetasi.
  • Kutambua kufinyangika kwa mifupa ya fuvu. Je, mifupa ya fuvu imepishana kufuatia shinikizo toka misuli ya uzazi?
  • Kadiria ukubwa wa pelvisi ya mama na iwapo ni kubwa kiasi cha kupitisha fetasi.
  • Chunguza rangi ya kiowevu cha amnioni.

Kipindi hiki hulenga sababu ya kwanza tu. Sababu hizo zingine za kuchunguza uke zimeelezwa katika vikao vinavyokuja.

Kukadiria kiwango cha kupanuka kwa seviksi

Nawa mikono yako vizuri kwa kutumia sabuni na maji safi kwa muda wa dakika mbili. Kisha vaa glavu safi. Mwelezee mama yale unayodhamiria kufanya. Uke huchunguzwa kwa kutumia vidole viwili vilivyovalishwa glavu. Fanya uchunguzi wote unaohitaji kabla haujaondoa vidole ukeni. Baada ya kuviondoa, usivirudishe ukeni tena.

  • Eleza kwa nini havirudishwi ukeni?

  • Ukirudisha vidole vyako ukeni unaweza, kusababisha maambukizi.

    Mwisho wa jibu.

Usichunguze uke kwa zaidi ya kila saa 4, isipokuwa kuwepo sababu mwafaka kufanya hivyo. (Mfano wa sababu mwafaka ni kuthibitisha ikiwa awamu ya pili ya leba imeanza.)

Mwagize mama alale chali, akunje miguu yake kwenye magoti, aweke nyayo zake bapa na apanue magoti. Safisha pembeni mwa uke kwa utaratibu ukutumia shashi safi iliyotumbukizwa kwenye kiowevu cha antiseptiki. Tenganisha midomo ya uke kwa kutumia vidole viwili vya mkono usio tumika (mkono unaotumika ni ule unaotumia kuandikia). Tumbukiza vidole vyako viwili (kidole cha shahada na cha kati) katika malai ya antiseptiki kisha uviingize ukeni taratibu. Fuata mkondo wa uke, upande wa juu na nyuma. Mwagize mama avute hewa kwa nguvu na ajaribu kutulia. Mwanamke aliyetulia hatatiziki sana na utaratibu huu.

Kupanuka kwa seviksi ni ongezeko la kipenyo cha uwazi wa seviksi, linalokadiriwa kwa sentimita. Kupanuka hufanyika baada ya seviksi kufitika (seviksi inapojitandazia kwenye uterasi, inajulikana kama iliyofitika. Mchoro 1.1) Unapaswa kufanya mazoezi ya kukadiria kwa usahihi kipenyo cha uwazi wa seviksi. Zoezi 2.1 litakusaidia.

Zoezi 2.1 Jifunze kupima utanuzi wa seviksi

Chukua takriban dakika 20 kufanya zoezi hili. Unahitaji kipande cha karatasi gumu au kadi nyembamba, rula, bikari (ya kuchorea duara), penseli na makasi.

  1. Chora duara 10 katika karatasi gumu. Duara ya kwanza iwe na kipenyo cha sentimita 1. Ongeza kipenyo cha kila duara kwa ukubwa wa sentimita 1: sentimita 1, sentimita 2, hivyo hivyo, hadi sentimita 10.
  2. Wacha mpaka mpana kati ya kila duara kisha ukate kadi iwe miraba 10 yenye ukubwa sawa.
  3. Toa undani wa kila duara ukitumia makasi.
  4. Andika kiasi cha kipenyo cha kila duara kwenye kadi.
  5. Chagua duara moja kisha uingize kwenye shimo hili kidole kimoja au viwili (vinavyotumika kuchunguza uke). Je, vidole vyote viwili vinatoshea? Kisha, funga macho yako na ujaribu kukadiria kiasi cha kipenyo cha duara kwa kipimo cha sentimita.
  6. Jaribu kukadiria kipenyo cha kila duara ukiwa umefunga macho yako. Kisha, thibitisha kama uko sahihi. Rudia zoezi hili mara kadhaa.
  • Ukirejelea Kipindi cha 1 cha somo, seviksi ina kipenyo kiasi gani wakati leba inapoendelea kutoka (a) hatua fiche hadi hatua wazi katika awamu ya kwanza? (b) hatua wazi katika awamu ya kwanza hadi awamu ya pili?

  • (a) sentimita 4; (b) sentimita 10 (imepanuka kabisa)

    Mwisho wa jibu

2.3.6 Kuchunguza sehemu ya nje ya uzazi na uke

Ukadiriaji wa mwisho katika Kipindi hiki ni kuchunguza sehemu ya nje ya uzazi wa mama na pembeni mwa sehemu ya ndani ya uke ili kutambua dalili za hatari.

Katika moduli ya Huduma za baada ya Kuzaa, unajifunza jinsi ya kuweka dawa ya (tetracycline) macho ya mtoto mchanga ili kumkinga kutokana na uwezekano wa maambukizi na viini kutoka kwenye njia ya uzazi.

  • Kuna mchozo wowote usio wa kawaida (mzito, wenye rangi ya manjano au nyeupe, na wenye uvundo) kutoka ukeni. Kuna vidonda vilivyovimba kwenye sehemu ya nje ya uzazi? Dalili hizi zinaweza kusababishwa na maambukizi ya njia ya mkojo au ya zinaa.
  • Kuna kovu ukeni zinazotokana na majeraha aliyopata alipokuwa akizaa mara ya kwanza au kutokana na ukeketaji (tohara)? Kovu hizi huchangia kuongeza kwa hatari ya kupata fistula. (Fistula ni uwazi ulioraruka baina ya uke na viungo vingine)
  • Je, uke umevimba? Uke unaweza kufunga njia anayopitia mtoto?

Ukiona mojawapo ya hizi dalili hatari, mpe mwanamke huyo rufaa hadi kwenye kituo cha afya, isipokuwa wakati mtoto yuko karibu kuzaliwa. Kipindi cha somo kifuatacho kinaelezea jinsi ya kutunza mwanamke aliye katika leba.

Muhtasari wa Kipindi cha 2 cha Somo

Katika Kipindi hiki, umejifunza:

  1. Kutayarisha vifaa vyako mapema kushughulikia leba na kuzaa, ili uwe tayari kuondoka punde tu unapoitwa.
  2. Kuchunguza upesi ishara muhimu (shinikizo la damu, kiwango cha mpito wa ateri na kiwangojoto cha mwili) za mwanamke katika leba.
  3. Kufuata kanuni za utunzaji usimwathiri mwanamke. Heshimu imani, matakwa na haki zake. Mhimize yeye na wanaomtunza nyumbani wamhudumie wakati wa leba na kuzaa.
  4. Kuuliza habari kuhusu mwanamke huyo na kuinakili: jina, umri, anwani, ugravida na usawa, siku ya mwisho kuona hedhi, mara ya kwanza kuhisi fetasi ikisonga, na muda uliopita baada tangu mkazo wa kwanza.
  5. Kuuliza kuhusu dalili za hatari: kuvuja damu ukeni, maumivu ya kichwa, mtukutiko wa maungo, matatizo ya kupumua, homa, maumivu makali ya fumbatio, kuvuja kwa kioevu cha amnioni kabla ya wakati wake (kupasuka kwa maji).
  6. Kutumia zile maneva nne za Leopold katika kupapasa fumbatio. Kutambua kutanguliza na hali fetasi, na jinsi ambavyo sehemu inayotanguliza ilivyofungamana.
  7. Kuchunguza uke wa mwanamke aliye katika leba. Kadiria kiwango cha kupanuka kwa seviksi, jinsi fetasi ilivyotanguliza, na kiwango ambacho fetasi imeshuka. Kadiria fuvu la fetasi, na utafute dalili za maambukizi ya uke, kovu au uvimbe.

Maswali ya Kujitathmini ya Kipindi cha 2 cha Somo

Kwa vile umekamilisha Kipindi hiki, jibu maswali yafuatayo ili kuthibitisha jinsi ulivyotimiza Malengo ya Somo la Kipindi hiki. Andika majibu yako katika shajara yako ya somo kisha uyajadili na mkufunzi wako katika mkutano wa Kipindi kifuatacho. Linganisha majibu yako na Maandishi ya Maswali ya Kujitathmini yaliyo mwishoni mwa moduli hii.

MK 2.1 (linatathmini Malengo ya Mafundisho)

Chukulia kwamba umeitwa nyumbani mwa mwanamke wa umri wa chini aliye katika leba. Ni nini unachofaa kufanya kwa dharura?

Answer

Mtathmini mwanamke huyo upesi ili kuamua kama ni lazima kumpa rufaa ya huduma kwa dharura.

  • Chunguza mdundo wa moyo wa fetasi. (Je, vipo katika hali ya kawaida ya midundo 120-160 /dakika?)
  • Chunguza dalili muhimu (shinikizo la damu, kiwango cha mpwito wa ateri na kiwango joto) ili kuona kama zipo katika hali ya kawaida. (Kifungu cha 2.1.1).
  • Tafuta dalili za kuvuja damu au kioevu cha amnioni.
  • Muulize (au aliye naye) ana maumivu ya kichwa au kuona uluwiluwi, matatizo ya kupumua, mtukutiko wa maungo, au maumivu makali ya fumbatio.

Ukiona dalili za dhikisho la fetasi, ikiwa moja wapo ya ishara muhimu zipo katika hali isiyo ya kawaida, au kukiwepo na mojawapo ya dalili hatari, mpe rufaa kwa hapo. (Dalili ya matatizo ya fetasi ni mdundo wa moyo ulio katika hali isiyo ya kawaida.)

Mwisho wa jibu

MK 2.2 (linatathmini Malengo ya Somo)

Umepapasa fumbatio la mwanamke aliye katika leba. Jaza mapengo yaliyo katika Kisanduku 2.1.

Kisanduku 2.1 Maneva za Leopold
Jina la papasoSehemu ya fumbatio inayopapaswaUnachofaa kuchunguza
Papaso la fandasi

Mikono ikiwa imewekwa kwenye pande zote za sehemu ya kati ya fumbatio, mkono mmoja ukifuatwa na mwingine ikisumia ndani

Ukitazama upande wa miguu, mikono ikiwa upande wa chini ya fumbatio, sukuma juu tu ya mfupa wa kinena, ukielekeza ndani kwa vidole vyako

Iwapo kichwa cha fetasi kimefungamana kwenye seviksi. Ukiweza kushika kichwa kutumia upana wa vidole viwili juu ya mfupa wa kinena cha mama, kichwa kimefungamana.
Answer
Kisanduku 2.1 maneva ya Leopold Imekamilika
Jina la papasoSehemu ya fumbatio itakayo papaswaCha kuangalia
Papaso la fandasiMikono ikiwa karibu na sehemu ya juu ya fumbatio ya mama, sukuma vidole vyako ukizungushia fandasi ya uterasiHali ya fetasi – Ikiwa iko katika hali ya longitudo (kawaida), mshazari au kukingama
Papaso la pembeniMikono ikiwekwa bapa kwenye sehemu zote mbili za katikati ya fumbatio; mkono wa kwanza ukifuatwa na wa pili kusukuma ndani.Uaguaji kamili wa mtoto alivyo lala na kama ni ‘kichwa chini’ au kutanguliza tako
Papaso la ndani zaidi la pelvisiTazama kuelekea miguu ya mama, mikono ikiwa upande wa chini ya fumbatio lake, sukuma ndani kwa vidole juu ya mfupa wa kinena kidogo. Ili kuhakikisha hali ya kichwa (kichwa chini) kutanguliza kichwa au (chini kabisa) kitangulizi
Mshiko wa PawlickVidole vinashikilia kichwa cha fetasi juu ya mfupa wa kinena kidogo.Kama kichwa cha fetasi kimefungamana na seviksi. Ikiwa Unaweza kushika kichwa kwa upana wa vidole juu ya mfupa wa kinena wa mama, kichwa kimefungamana.

Mwisho wa jibu

MK 2.3 (linatathmini Malengo ya Somo)

Makeda ametembelea Kituo chako cha Afya. Umemchunguza upesi kisha ukabaini kuwa hatahitaji rufaa ya dharura. Sasa unachukua historia yake. Utachukua vipi historia yake na ni habari gani unayofaa kupata kutoka kwake?

Answer

(a) Ili kuchukua historia ya Makeda, mhimize kuwa na uwazi wa kuzungumza nawe. Fuata kanuni za utunzaji mwafaka kwa mwanamke unapomuuliza maswali. Sikiza kwa makini, jibu maswali yake na uweke siri anayokufichulia. (Tazama Ksanduku 2.1 ili kupata maelezo kuhusu huduma mwafaka kwa mwanamke.)

(b) Ujumbe unaohitaji kutoka kwa Makeda:

  • Jina lake, umri, kimo, anwani, dini (iwapo anataka kukwambia) na kazi (iwapo ameajiriwa).
  • ‘Dalili yake tangulizi’ ni nini (kwa mfano leba, kuhisi uchovu)?
  • Je, ameshawahi kupata mimba au kuzaa tena? (Alikuwa na matatizo yoyote? Ni matatizo mangapi iwapo alikumbana nayo?)
  • Siku ya kwanza ya kipindi kilichopita cha hedhi ya kawaida ilikuwa gani?
  • Je, ametambua dalili zozote hatari (kwa mfano kuvuja damu kutoka ukeni, maumivu ya kichwa, mchozo usio wa kawaida kutoka ukeni)?

Mwisho wa jibu

MK 2.4 (linatathmini Malengo ya Somo 2.6 na 2.7)

Sasa umepata historia ya Makeda na unataka kumchunguza. Je, utafanya nini kwanza na ni nini unachochunguza?

Answer

Kabla ya kumchunguza ukeni, fuata kanuni za utunzaji mwafaka wa mwanamke na umwakikishie Makeda kuhusu siri zake. Kisha nawa mikono kabisa na uvae glavu mpya. Chunguza yafuatayo wakati unapochunguza:

  • Kiasi ambacho seviksi imepanuka.
  • Kiasi cha pelvisi ya Makeda na iwapo fetasi itaweza kupita
  • Kiwango cha kufinyangika (kupishana) kwa mifupa ya fuvu la fetasi kufuatia shinikizo kwenye njia ya uzazi.
  • Mchozo wowote unaonuka na usio wa kawaida; kovu yoyote au kufura. (Dalili hizi ni hatari. Ukizitambua dalili hizi, mhamishe Makeda hadi kwenye kituo cha afya.)

Mwisho wa jibu

MK 2.5 (linatathmini Malengo ya Somo la 2.1)

Ni maelezo gani yasiyo ya kweli? Katika kila kauli, eleza lisilo la kweli.

  1. Kiwangojoto cha mwili cha nyusi 39 ni dalili ya homa ya kiwango cha juu.
  2. Umri wa ujauzito ni miaka aliyo nayo mama wakati anapokuwa mjamzito.
  3. Usawa ni idadi ya watoto waliozaliwa hai baada ya wiki 28 za ujauzito.
  4. Ugravida ni idadi ya mimba amewahi kupata bila kuzingatia Malengo ya mimba hiyo.
  5. Unapochunguza fumbatio la mwanamke aliye katika leba, angalia ukubwa, umbo na kovu.
  6. Kuchunguza kwa kupapasa fandasi mlio kama wa ngoma unaosikia unaposikiza moyo wa mtoto ukitumia fetoskopu.
  7. Kutanguliza matako ni ishara kuwa utaratibu wa kuzaa utakuwa na matatizo.
  8. Oskulesheni ni milio ambayo mama aliye katika leba kwa wakati mwingine hutoa.
Answer
  1. A ni kweli. Homa ya kiwango cha juu ni kiwangojoto kilichozidi nyusi 38.5 (homa ya kiwango cha chini ni kati ya nyusi 37.5 - 38.4.)
  2. B si kweli. Umri wa ujauzito ni idadi ya wiki ambazo fetasi imekuwa ndani ya uterasi. Muda huu huhesabiwa kutoka siku ambayo kipindi cha mwisho cha hedhi ya kawaida kilianza.
  3. C si kweli. Usawa ni idadi ya watoto waliozaliwa baada ya wiki 28 za ujauzito.
  4. D si kweli. Ugravida ni idadi ya mimba amewahi kupata bila kuzingatia Malengo ya mimba hiyo.
  5. E ni kweli. Kovu isiyo ya kawaida ni ishara kuwa uterasi inaweza kuwa na kovu, jambo linaloongeza hatari ya kupasuka kwa uterasi.
  6. F si kweli. Kuchunguza kwa kupapasa fandasi ni jina lililopewa utaratibu wa kupapasa sehemu ya chini ya uterasi yenye umbo la kuba (inayojulikana kama fandasi) ili kutambua hali ya kichwa cha mtoto.
  7. G si kweli. Kutanguliza matako ni wakati matako ya mtoto ndiyo sehemu iliyotangulia. Kutanguliza matako ni ishara kuwa utaratibu wa kuzaa unaweza kuwa na matatizo. Unafaa kumhamisha mwanamke huyu hadi kwenye kituo cha afya.
  8. H si kweli. Oskulesheni ni kusikiza sauti zilizo ndani ya fumbatio.

Mwisho wa jibu