Vipindi vya masomo vya hapo awali vilitanguliza ufafanuzi, ishara, dalili na awamu za leba ya kawaida. Pia ulijifunza kuhusu fetasi kutanguliza veteksi kikawaida katika kuzaa. Katika Kipindi hiki cha somo utajifunza kuhusu milalo isiyo ya kawaida inayotokea sana (ya kutanguliza matako, bega, uso, au paji la uso). Pia utajifunza mbinu za kuitambua na hatua zinazohitajika kwa kuzuia matatizo yanayotokea katika leba. Wakati mwingine uzazi huzuilika kwa sababu mtoto yuko katika mlalo usio wa kawaida. Hatua ya dharura inaweza kuokoa maisha ya mama na mtoto wake. Pia utajifunza kuhusu uzazi wa pacha. Watoto hawa wawili hufungamana pamoja na hii humzuia yeyote kuzaliwa. Iwapo watoto watafungamana, matatizo yanaweza kutokea.
Baada ya Kipindi hiki cha somo utaweza:
8.1 Kufafanua na kutumia kwa usahihi maneno yote muhimu yaliyoandika kwa herufi nzito. (Maswali ya kujitathmini 8.1 na 8.2)
8.2 Kueleza jinsi ya kutambua fetasi iliyotanguliza veteksi. Tambua veteksi kwenye fetasi iliyo katika mlalo mbaya na isiyokuwa katika nafasi ya kawaida. (Maswali ya kujitathmini 8.1 na 8.2)
8.3 Kueleza visababishi na matatizo ya fetasi na mama kutokana na mlalo mbaya wa fetasi katika leba ya mimba iliyokomaa. (Swali la kujitathmini 8.3)
8.4 Kuelezea jinsi ya kutambua mimba ya zaidi ya mtoto mmoja na matatizo yanayoweza kutokea. (Swali la kujitathmini 8.4)
8.5 Kueleza lini na jinsi ya kumpa rufaa mwanamke mwenye leba kutokana na mlalo usio wa kawaida wa fetasi au mimba ya zaidi ya mtoto mmoja. (Swali la kujitathmini 8.4)
Katika takriban asilimia 95 ya uzazi, sehemu ya fetasi inayotangulia ukingoni mwa pelvisi ni sehemu iliyo juu zaidi ya kichwa cha fetasi. Sehemu hii ya kichwa huitwa veteksi (Picha 8.1). Hali hii huitwa mlalo wa kutanguliza veteksi. Tambua kuwa kidevu cha mtoto kimepindwa kuelekea kwenye kifua chake. Veteksi ndiyo sehemu inayotangulia kuingia kwenye pelvisi ya mama. Katika nafasi na hali hii, kichwa cha mtoto husemekana kuwa “kimejikunja vizuri”.
Mwanzoni mwa ujauzito, mtoto hugeuzwa upande mwingine. Upande wa chini wa mtoto huelekezwa chini kuelekea seviksi ya mama. Mlalo huu huitwa wa kutanguliza matako. Mwanzoni mwa kukua, kichwa cha fetasi huwa kikubwa kuliko matako yake. Mara nyingi kichwa huchukua kaviti pana zaidi, yaani fandasi ya uterasi. Fetasi inapoendelea kuwa kubwa, matako huwa makubwa kuliko kichwa. Mtoto hugeuza mlalo wake mwenyewe ambapo matako yake sasa huchukua fandasi. Kwa ufupi, mwanzoni mwa ujauzito fetasi nyingi huwa katika mlalo wa kutanguliza matako. Baadaye katika ujauzito, fetasi nyingi hujipindua na kutanguliza veteksi.
Utajifunza kuhusu leba iliyozuiliwa katika Kipindi cha 9 cha Somo.
Mtoto anaweza kujitokeza kwenye pelvisi ya mama katika hali nyingine mbali na kutanguliza veteksi. Aina hii ya mlalo huitwa mlalo usio wa kawaida au mlalo mbaya. Milalo hii ina hatari zaidi ya kuzuiliwa na matatizo mengine ya uzazi kuliko mlalo wa kutanguliza veteksi. Aina za mlalo mbaya zinazotokea maranyingi ni kutanguliza matako, bega, uso au paji la uso. Tutajadili kila moja katika Kipindi hiki. Kumbuka kuwa mtoto anaweza kuwa “kichwa kikiwa chini” lakini katika mlalo usio wa kawaida. Mifano ni kutanguliza uso au paji la uso katika hali ambapo uso au paji la uso wa mtoto ndiyo kitangulizi.
Mtoto anaweza pia kuwa katika nafasi isiyo ya kawaida hata akiwa ametanguliza veteksi. Inaweza kuwa vigumu kugundua inapotendeka. Katika uzazi wa kawaida, wakati kichwa cha mtoto kimekabiliwa kwenye pelvisi, upande wa nyuma wa fuvu la kichwa cha mtoto huelekezwa upande wa mbele wa pelvisi ya mama. Upande wa nyuma wa fuvu la kichwa cha mtoto huitwa kisogo. Upande wa mbele ya pelvisi ya mama huitwa simfisisi ya kinena.Simfisisi ya kinena ni mahali ambapo mifupa miwili ya kinena inaungana pamoja. Hali hii ya fuvu la kichwa cha fetasi huitwa hali ya kisogo kuwa upande wa mbele (Picha 8.2a). Ikiwa kisogo cha fuvu la kichwa cha mtoto kinaelekea upande wa nyuma wa mama, hali hii ya kisogo kuwa upande wa nyuma (Picha 8.2b) ni veteksi kutokuwa katika nafasi ya kawaida. Ni vigumu zaidi kwa mtoto kuzaliwa akiwa katika hali hii. Uzuri ni kwamba zaidi ya takriban asilimia 90 ya watoto ambao veteksi haiko katika nafasi yake huzunguka na kuwa katika hali ya kisogo kuwa upande wa mbele na kuzaliwa kikawaida.
Ulijifunza nafasi za mwelekeo: mbele na nyuma katika Moduli ya Utunzaji katika Ujauzito, sehemu ya 1, Kipindi cha 3.
Tambua kwamba fuvu la kichwa cha mtoto pia linaweza kulazwa upande wa kushoto au wa kulia katika hali ya kisogo kuwa upande wa mbele au upande wa nyuma.
Unaweza kukosa kutambua ni kwa nini mtoto yuko katika mlalo usio wa kawaida au katika nafasi isiyo ya kawaida wakati wa kuzaa. Hata hivyo, hali hizihuongeza hatari ya mlalo mbaya na kutokuwa katika nafasi ya kawaida:
Mimba ya zaidi ya mtoto mmoja ndio mahusiko ya sehemu ya 8.7 ya Kipindi hiki. Ulijifunza kuhusu plasenta privia katika Moduli ya Utunzaji katika Ujauzito, Kipindi cha 21.
Iwapo mtoto anajitokeza katika mlalo au nafasi isiyo ya kawaida, inaweza kuwa vigumu kukamilisha miendo saba mikuu. Ulijifunza kuhusu miendo hii katika Vipindi vya 3 na 5. Hatimaye, uzazi huwa mgumu zaidi na hatari ya matatizo haya huongezeka.
Ulijifunza kuhusu kupasuka kwa membrani kabla ya muda wake katika Kipindi cha 17 cha Moduli ya Utunzaji katika Ujauzito, sehemu ya 2.
Kumbuka matatizo haya unapojifunza kuhusu aina zinazotokea mara nyingi za mlalo mbaya na jinsi ya kuzitambua.
Katika mlalo wa kutanguliza matako, fetasi hujilaza matako yake yakiwa nyuma. Matako na/au miguu ndizo sehemu zinazotangulia wakati wa kuzaliwa. Mlalo wa kutanguliza matako hutokea katika takriban asilimia 3-4 za uzazi unaotendeka baada ya wiki 34 ya ujauzito.
Je, ni lini ambapo mlalo wa kutanguliza matako huwa nafasi ya kawaida kwa fetasi?
Mwanzoni mwa ujauzito, matako ya mtoto huelekezwa chini kuelekea kwenye seviksi ya mama. Kichwa ndicho sehemu kubwa zaida katika awamu hii ya ukuaji. Kichwa chake huwa kwenye fandasi ya uterasi, ambayo ndiyo sehemu pana zaidi ya kaviti ya uterasi.
Mwisho wa jibu
Unaweza kuona kulala kingamo katika Picha 8.7 baadaye katika Kipindi hiki.
Katika hali nyingi, huoni sababu dhahiri inayoweza kuifanya fetasi kutanguliza matako baada ya muda kamili wa ujauzito. Mara nyingi mlalo wa kutanguliza matako wakati wa kuzaa huhusishwa na fetasi kulala kingamo mwanzoni mwa ujauzito. Kulala kingamo humaanisha kuwa fetasi imelala kwa upande kutoka upande mmoja hadi mwingine wa fumbatio ya mama, na imeangalia plasenta iliyojipandikiza kwa upande. Plasenta ikiwa mbele ya uso wa mtoto, inaweza kuzuia mchakato wa kawaida wa kupinduka. Wakati wa kupinduka mtoto hugeuza kichwa chini anapoendelea kuwa mkubwa katika ujauzito. Kutokana na haya, mtoto hugeuka kwa upande huo mwingine na kuishia katika mlalo wa kutanguliza matako. Mlalo wa kutanguliza matako katika leba unaweza pia kusababishwa na mambo haya:
Kutambua mlalo wa kutanguliza matako, tomasa fumbatio. Hisi kichwa cha fetasi juu ya kitovu cha mama. Kichwa huhisika kama bonge gumu, laini na lenye umbo la mviringo utakalohisi likisonga kwa upole katikati ya mikono yako.
Je, kwa nini unafikiri kuwa bonge linalosonga hapo juu kwenye fumbatio ni dalili ya mlalo wa kutanguliza matako? (Ulijifunza haya katika Kipindi cha 11 cha Somo cha Moduli ya Utunzaji katika ujauzito.)
Kichwa cha mtoto kinaweza kutingika kidogo kwa sababu ya ulegevu wa shingo la mtoto. Kwa hivyo ukihisi bonge la mviringo linalosongakwenye upande wajuu wa kitovu cha mama, kuna uwezekano mkubwa kuwa ni kichwa cha mtoto. Ikiwa mtoto yuko “chini juu” katika mlalo wa kutanguliza veteksi, mgongo wake wote husonga ukijaribu kutikisa sehemu za fetasi zilizo kwenye fandasi (Picha 8.3).
Mwisho wa jibu
Baada ya fetasi kukabiliwa na leba kuanza, unaweza kuhisi matako ya mtoto yakiwa laini na yenye umbo lisilotabirika wakati wa uchunguzi wa ukeni. Huhisi tofauti na lile bonge la mviringo la fuvu la kichwa cha fetasi katika mlalo wa kutanguliza veteksi. Membreni za fetasi zinapopasuka, unaweza kuhisi matako na /au miguu dhahiri zaidi. Unaweza kuhisi mkundu wa mtoto. Unaweza kuona mekoniamu mbichi, nzito nyeusi kwenye kidole chako unachochunguzia. Ikiwa miguu ya mtoto imenyooka, unaweza kuhisi sehemu ya siri. Huenda ukaweza kujua jinsia ya mtoto huyo kabla ajazaliwa.
Aina tatu za mlalo wa kutanguliza matako zimeelezewa katika Picha 8.4:
Wape rufaa wote walio na hali ambazo mtoto ametanguliza matako waende katika kituo cha afya cha ngazi ya juu kilicho karibu.
Aina zote za mlalo wa kutanguliza matako husababisha hatari kuu kwa mtoto:
Uzazi wa mlalo wa kutanguliza matako unaweza kusababisha kujeruhiwa kwa njia ya uzazi ya mama au jenitalia za nje zinaweza kutanuliwa kupita kiasi kwa sababu sehemu za fetasi haziwezi kupita.
Prolapsi ya kiungamwana katika mlalo wa kawaida wa kutanguliza veteksi ilielezewa katika Kipindi cha 17 cha Somo cha Moduli ya Utunzaji katika Ujauzito. Kuchubuka kwa Plasenta kulielezewa katika Kipindi cha 21 cha Somo.
Je, kuna athari gani kwa mtoto akikwama, leba imezuiliwa, kiungamwana kimechomoza au kukitokea kuchubuka kwa plasenta?
Matokeo ni haipoksia. Mtoto huyo hukoseshwa oksijeni na anaweza kukumbwa na kuharibika kwa ubongo kwa kudumu au afariki.
Ulijifunza kuhusu visababishi na matokeo ya haipoksia katika Moduli ya utunzaji katika ujauzito.
Mwisho wa jibu
Mlalo wa kutanguliza uso hutokea wakati shingo la mtoto limerefushwa (limekunjwa kuelekea nyuma) kiasi kwamba kisogo kinagusa uti wa mgongo wa mtoto huyo (Picha 8.5). Katika hali hii, uso wa mtoto ndio unaotangulia.
Mpe mama rufaa iwapo mtoto aliye katika mlalo wa kutanguliza uso huku kidevu chake kikiwa kimeangalia upande wa uti wa mgongo wa mama hatazunguka na hivyo basi leba kuendelea kwa muda mrefu.
Takribani mimba ya 1 kwa kila 500 inayotimiza muda kamili huwa katika mlalo wa kutanguliza uso. Picha 8.5 yaonyesha jinsi kichwa kilivyojikunja shingoni. Watoto wanaojitokeza katika hali ambapo kidevu kimeangalia upande wa uti wa mgongo wa mama (Picha 8.5b) kwa kawaida huzunguka wenyewe katika leba. Wanajiweka katika hali ya “kidevu mbele”, ambayo hurahisisha kuzaliwa kwao. Hata hivyo wasipozunguka na kujiweka katika hali ya kidevu upande wa mbele wa pelvisi, huenda wasizaliwe kupitia ukeni. Kidevu cha mtoto hukwama kwenye sakramu ya mama. (Sakramu ni mfupa uliobinuka nyuma ya pelvisi.) Mtoto aliye katika hali hii lazima azaliwe kupitia upasuaji.
Visababishi vya mlalo wa kutanguliza uso ni sawa na vile vya mlalo wa kutanguliza matako:
Huenda usigundue mlalo wa kutanguliza uso unapotomasa fumbatio la mama. Ikiwa kidevu kimeangalia upande wa nyuma, ugunduzi ni mgumu. Unapochunguza fumbatio, unaweza kuhisi umbo lisilo la kawaida. Uti wa fetasi huwa umejipinda katika umbo la S. Unapofanya uchunguzi ukeni, unaweza kugundua mlalo wa kutanguliza uso kwa msingi wa sababu hizi:
Hata hivyo, leba inapoendelea, uso wa mtoto hupata edema (kufura kutokana na kujaa kwa viowevu). Hali hii hufanya iwe vigumu kuutofautisha na umbo laini unalogusa katika mlalo wa kutanguliza matako.
Matatizo kwa fetasi ni haya:
Katika mlalo wa kutanguliza paji la uso, kichwa cha mtoto huwa kimerefuka kidogo shingoni (ikilinganishwa na kilivyo katika mlalo wa kutanguliza uso). Kwa hivyo, paji lake la uso ndiyo sehemu inayotangulia (Picha 8.6). Mlalo huu hautokei sana. Ni 1 tu kwa uzazi 1000 uliokomaa ambao huwa katika mlalo wa kutanguliza paji la uso.
Umeona mambo haya yote kama visababishi vya milalo mingine mibaya:
Mlalo wa kutanguliza paji la uso kwa kawaida haugunduliwi kabla ya mwanzo wa leba. Hata hivyo, wahudumu wa uzazi wenye uzoefu mwingi wanaweza kugundua mlalo wa kutanguliza paji la uso. Wakati wa uchunguzi wa fumbatio, kichwa huwa juu katika fumbatio la mama. Kichwa huonekana kikubwa mno na hakiteremki kuingia kwenye pelvisi, hata kukiwa na mikazo bora ya uterasi. Wakati wa kufanya uchunguzi ukeni, sehemu inayotangulia huwa juu na inaweza kuwa vigumu kuifikia. Unaweza kugusa mwanzo wa pua na macho. Lakini hauwezi kugusa kinywa, mwisho wa pua au kidevu. Pia unaweza kugusa fontaneli (utosi) ya mbele. Hata hivyo, baada ya saa fulani za kuwepo kwa leba, uvimbe mkubwa upande wa mbele ya fuvu la kichwa cha fetasi unaweza kuifunika alama hii.
Kumbuka wajihi wa uvimbe wa kawaida na fontaneli ya nyuma iliyoonyeshwa katika Picha 4.4.
Matatizo ya mlalo wa kutanguliza paji la uso ni sawa na yale ya milalo mingine mibaya:
Je, ni upi unoweza kukumbana nao: mlalo wa kutanguliza uso au paji la uso?
Mlalo wa kutanguliza uso hutokea sana. Huu hutokea katika mimba ya 1 kwa kila leba 500 zilizokomaa. Mlalo wa kutanguliza paji la uso hautokei sana, kwani hutokea katika ujauzito 1 kwa kila leba 1000 zilizokomaa.
Mwisho wa jibu
Mlalo wa kutanguliza bega hautokei sana katika mimba iliyokomaa. Hata hivyo, mlalo wa kutanguliza bega hutokea iwapo fetasi imelala kingamano kwenye uterasi (Picha 8.7). Pengine haikukamilisha mvunguko ilipokuwa ikipinduka kutoka katika hali ya kutanguliza matako hadi kutanguliza veteksi. Labda imelala kingamano tangu mwanzoni mwa mimba. Mtoto akilala chali, huenda mgongo wake ndio kitangulizi. Iwapo mtoto amelala kifudifudi (ameangalia chini), mkono wake unaweza kujitokeza kupitia kwenye seviksi. Mtoto aliye katika hali ya kingamano hawezi kuzaliwa kupitia ukeni na leba hiyo huzuiliwa. Wape rufaa kwa haraka wenye watoto walio katika mlalo wa kutanguliza bega.
Usijaribu kumgeuza mtoto aliyeulalia upande wake.Isipokuwa mhudumu wa afya mwenye ujuzi amgeuze, mtoto huyo anafaa kuzaliwa kwa njia ya upasuaji.
Mlalo wa kutanguliza bega unaweza kusababishwa na vipengele vinavyohusu mama au fetasi.
Vipengele vinavyomhusu mama ni:
Vipengele vinavyoihusu fetasi ni:
Je, “plasenta privia” na “polihadromino” huashiria nini?
Plasenta privia ni hali ya plasenta imeufunika mwanya wa seviksi kikamilifu au kwa kiasi. Polihadromino ni kiasi kingi cha kiowevu cha amnioni. Matatizo haya yote mawili yanaweza kusababisha milalo mibaya.
Mwisho wa jibu
Unapotomasa fumbatio uterasi huonekana kuwa pana na urefu wa fandasi ni mdogo kuliko inavyotarajiwa kwa kipindi hiki cha ujauzito. Urefu ni mdogo kwa sababu kichwa wala matako ya mtoto hayako kwenye fandasi. Kwa kawaida unaweza kuhisi kichwa kwenye upande mmoja wa fumbatio la mama. Wakati wa uchunguzi wa ukeni, huenda usihisi kitangulizi mwanzoni mwa leba. Lakini leba ikiendelea vizuri, unaweza kuhisi mbavu za mtoto. Bega linapoingia ukingoni mwa pelvisi, mkono wa mtoto unaweza kuchomoza na kuonekana nje ya uke.
Matatizo ni haya:
Kumbuka kuwa mlalo wa kutanguliza bega una maana kuwa mtoto hawezi kuzaliwa kupitia ukeni. Ukigundua mlalo wa kutanguliza bega kwa mwanamke aliye tayari katika leba, mpe rufaa mara moja aende katika kituo cha afya cha kiwango cha juu.
Katika visa vyote vya mlalo mbaya au kutokuwa katika nafasi ya kawaida, usijaribu kumgeuza mtoto kwa kutumia mikono yako! Ni daktari au mkunga maalum aliyehitimu tu anayepaswa kujaribu kumgeuza mtoto. Mpe mama rufaa ili yeye pamoja na mtoto wake waweze kupata huduma ya dharura ya uzazi.
Sehemu hii inaeleza kuhusu mimba ya zaidi ya mtoto mmoja, ambayo ni zaidi ya fetasi moja kwenye uterasi. Zaidi ya asilimia 95 ya mimba ya zaidi ya mtoto mmoja ni pacha (fetasi mbili). Lakini unaweza pia kupata watatu (fetasi tatu), wanne (fetasi nne), watano (fetasi tano) na idadi zingine za juu. Uwezekano wa kupata zaidi ya fetasi moja hupunguka kulingana na ongezeko katika idadi ya fetasi. Visa vya kupata mapacha ni tofauti kwa kila nchi. Nchi zilizo Mashariki mwa Asia kama vile Japan na Uchina zina uwezekano mdogo wa visa vya upataji wa mapacha. Mashariki mwa Asia, 1 kati ya mimba 1000 ni pacha wa kidugu au pacha wasiofanana. Wafrika weusi wana uwezekano mkubwa wa kupata mapacha. Nchini Nigeria, 1 kati ya mimba 20 ni pacha wa kidugu. Mimba ya zaidi ya mtoto mmoja huhusishwa sana na upotezaji wa mimba katika awamu ya kwanza na watoto kufariki wakati wa kuzaliwa, hasa kutokana na kuzaliwa kabla ya muda kamili wa mimba kumalizika.
Mapacha wanaweza kufanana (wa monozaigoti) au wasifanane na wa kidugu (wa daizigoti). Mapacha wa monozaigoti hutokea kwenye yai moja lililotungishwa (zaigoti). Kwa hivyo wao huwa wa jinsia moja na hutumia plasenta moja. Kwa upande mwingine, mapacha wa daizigoti hutokana na zaigoti mbili tofauti. Kwa hivyo, wanaweza kuwa wa jinsia moja au la na pia wana plasenta tofauti. Picha 8.8 inaonyesha aina za mimba ya mapacha na mchakato wa kukua kwake.
Wakati wa uchunguzi wa fumbatio, unaweza kutambua vitu hivi:
Wanawake walio na mimba ya pacha hutatizika sana na matatizo madogo madogo ya ujauzito kama vile kichefuchefu cha mjamzito asubuhi, kichefuchefu, na kiungulio. mimba ya pacha ni kisababishi kimoja cha hiparemisisi gravidaramu (kichefuchefu kingi na kutapika kupindukia katika ujauzito). Kina mama wa mapacha pia wamo katika hatari zaidi ya kupata anemia itokanayo na ukosefu wa ayoni na folati katika ujauzito.
Je, unaweza kupendekeza ni kwa nini anemia ni hatari kubwa katika mimba ya zaidi ya mtoto mmoja?
Lazima mama apate virutubishi vya kuwalisha watoto wawili (au zaidi). Ikiwa hapati ayoni na folati ya kutosha katika lishe yake au kupitia katika vyakula vya ziada, atapata anemia.
Mwisho wa jibu
Matatizo mengine ni kama haya:
Watoto pacha wanaweza kuwa wadogo ikilinganishwa na umri wa ujauzito huo. Watoto pacha wana uwezekano mkubwa wa kupata matatizo yanayohusiana na uzani wa chini wa kuzaliwa. (Matatizo haya ni kama kuwa wenye kuathiriwa na maambukizi kwa urahisi, kupoteza joto na ugumu katika kunyonya).
Utajifunza kwa kina kuhusu watoto waliozaliwa wakiwa na uzani wa chini katika moduli ya Utunzaji baada ya kuzaa.
Jinsi ulivyoona katika Kipindi hiki, mlalo wowote isipokuwa ule wa kutanguliza veteksi unazo hatari zake kwa mama na mtoto. Kwa sababu hii, wanawake wote wanaokumbwa na milalo isiyo ya kawaida au mimba ya zaidi ya mtoto mmoja wanafaa kupata huduma bora kutoka kwa wataalam wakuu wa afya. Wanawake hawa wanapaswa kuhudumiwa katika kituo cha afya kilicho na uwezo wa kutoa huduma bora ya dharura ya uzazi. Utambuzi wa mapema na rufaa kwa mwanamke aliye na mojawapo ya hali hizi inaweza kuokoa maisha yake pamoja na ya mtoto wake.
Je, ni nini unachoweza kufanya ili kupunguza hatari zinazotokana na mlalo mbaya wa fetasi au mimba ya zaidi ya mtoto mmoja kwa wanawake unaowatunza?
Katika utunzaji maalum wa manawake katika ujauzito, chunguza mlalo usio wa kawaida wa fetasi kila wanapokutembelea baada ya majuma 36 ya ujauzito. Ukigundua mlalo usio wa kawaida au mimba ya zaidi ya mtoto mmoja, mpe mwanamke huyo rufaa kabla ya leba kuanza.
Mwisho wa jibu
Katika Kipindi cha 8 cha somo, ulijifunza mambo haya:
Kwa kuwa umekamilisha Kipindi hiki cha somo, jibu maswali haya ili kutathmini ulivyojifunza. Linganisha majibu yako na Muhtasari juu ya Maswali ya Kujitathmini mwishoni mwa Moduli hii.
Je, ni maelezo yapi yaliyosahihi na yasiyosahihi? Andika maelezo sahihi kwa yale unayoona kuwa si kweli.
Mwisho wa jibu
Je, tofauti kuu kati ya mlalo wa kawaida na usio wa kawaida wa fetasi ni zipi? Tumia istlahi sahihi za kitiba zilizo katika herufi nzito kwenye maelezo yako.
Katika mlalo wa kawaida, veteksi (sehemu ya juu kabisa ya kichwa cha fetasi) huwa ya kwanza kufika kwenye ukingo wa pelvisi ya mama. Kisogo (sehemu ya nyuma ya fuvu la kichwa cha fetasi) huangalia sehemu ya mbele ya pelvisi ya mama (kwenye simfisisi ya kinena).
Mlalo usio wa kawaida hutokea wakati ambapo veteksi haipo kwenye nafasi yake ya kawaida au mlalo mbayaukitokea. (Katika hali ambapo veteksi haipo kwenye nafasi yake ya kawaida katika mlalo wa kutanguliza veteksi, kisogo cha fetasi huangalia upande wa nyuma wa mama badala ya simfisisi ya kinena. Katika mlalo mbaya, sehemu yoyote ile isipokuwa veteksi hutangulia.) Kwa mfano, mlalo wa kutanguliza matako (matako kwanza), mlalo wa kutanguliza uso (uso kwanza), mlalo wa kutanguliza paji la uso (paji la uso kwanza), na mlalo wa kutanguliza bega (fetasi kulala kingamo).
Mwisho wa jibu
Mwisho wa jibu
Mwanamke mjamzito amehamia kwenye kijiji chako. Tayari amefikisha majuma 37 ya ujauzito. Hujawahi kumuona. Anakueleza kuwa alizaa pacha miaka mitatu iliyopita na anataka kujua ikiwa ana pacha tena.
Mwisho wa jibu