Utunzaji wa baada ya kuzaa ni utunzaji anaopewa mama na mtoto wake mchanga mara tu baada ya kuzaa na kwa wiki sita ya kwanza ya maisha (Picha 1.1). Kipindi hiki hudhihirisha kuanzishwa kwa awamu mpya ya maisha ya kifamilia kwa wanawake na wenzi wao na mwanzo wa rekodi ya kiafya maishani mwa watoto wachanga (au watoto waliozaliwa - jina linalotumiwa mara nyingi na madaktari, wauguzi na wakunga).
Ingawa kipindi cha baada ya kuzaa hakina utata kwa wanawake na watoto wengi, utunzaji bora wa baada ya kuzaa pia inahusu kutambua mchepuko wowote dhidi ya upataji nafuu unaotarajiwa baada ya kuzaa, na kutathmini na kutatua ipasavyo kwa wakati ufaao. Ni jambo la kusikitisha kuwa katika nchi nyingi za Sahara ya Afrika chini ya asilimia 37 ya wanawake ndio huzalia kwenye vituo vya afya na chini ya asilimia 10 hupokea utunzaji wowote baada ya kuzaa katika muda wa siku mbili baada ya kuzaa. Kwa hivyo, jukumu lako kama mhudumu wa afya nje ya hospitali ni muhimu katika kuboresha hali hii, kutambua dalili za hatari na kupunguza athari mbaya kwa kina mama na watoto wachanga.
Katika kila nchi barani Afrika, kipindi cha baada ya kuzaa mara nyingi hutambulika kwa vitendo maalumu vya kitamaduni. Kuelewa imani na asasi za kijamii katika jamii yako ni jambo la kimsingi katika kuhakikisha utunzaji bora wa baada ya kuzaa. Katika Kipindi hiki cha kwanza cha somo, utajifunza kuhusu ni kwa nini huduma katika kipindi cha baada ya kuzaa ni muhimu sana na kuhusu umuhimu wa kushiriki na kujihusisha kwa jamii katika kutimiza utunzaji bora wa baada ya kuzaa. Tunatoa muhtasari wa baadhi ya mbinu za uhamasishaji wa jamii kwa kifupi na kujadili jinsi ya kujenga ubia na watu mashuhuri wanaoweza kukusaidia kuwatunza kina mama na watoto wao.
Baada ya kusoma katika Kipindi hiki, unapaswa kuwa na uwezo wa:
1.1 Kufafanua na kutumia kwa usahihi maneno yote muhimu yaliyochapishwa kwa herufi nzito. (Swali la kujitathmini 1.1)
1.2 Kueleza umuhimu wa utunzaji baada ya kuzaa kwa kuzingatia wakati ambapo kina mama wengi na watoto wachanga hufariki na visababishi vikuu vya vifo hivi. (Swali la kujitathmini 1.2)
1.3 Kueleza kwa kifupi mabadiliko makuu ya kifiziolojia kwa mama na mtoto mchanga katika kipindi cha baada ya kuzaa. (Swali la kujitathmini 1.3)
1.4 Kueleza dalili kuu za hatari kwa mama na mtoto mchanga katika kipindi cha baada ya kuzaa. (Swali la kujitathmini 1.3)
1.5 Kueleza umuhimu wa kujihusisha kwa jamii katika utunzaji wa baada ya kuzaa na kuelezea jinsi utakavyojenga ushirikiano na watu mashuhuri katika jamii hiyo. (Swali la kujitathmini 1.2)
Utunzaji bora baada ya kuzaa unaweza kuleta tofauti zaidi kwa afya na maisha ya kina mama na watoto wachanga mwanzoni mwa kipindi cha uchanga na siku saba za kwanza za maisha. Hata hivyo, kipindi hiki cha uchanga, tangu kuzaliwa hadi siku 28 baada ya kuzaliwa ni wakati wa kiwango cha juu cha hatari. Vifo vya watoto wachanga waliozaliwa wakiwa hai vitokeavyo katika kipindi cha siku 28 za kwanza huripotiwa na nchi zote ulimwenguni kama kiwango chavifo vya watoto wachanga kwa kila watoto 1,000 wanaozaliwa wakiwa hai. Vile vile, ripoti za vifo vya kina mama vitokanavyo na ujauzito ni vifo vya wanawake vitokanavyo na matatizo yanayohusiana na matatizo ya baada ya kuzaa na sio tu yale yanayotokea wakati wa kuzaa. Viwango hivi vyote ni viashiria muhimu vya ubora wa utunzaji baada ya kuzaa.
Kipindi baada ya kuzaa ni wakati muhimu kwa mama na mtoto wake mchanga. Hii ndiyo sababu ya kwanza ya kukufanya ulenge utunzaji zaidi na mazingatio kwa kipindi hiki. Afrika, uwiano wa vifo vitokanavyo na ujauzito ni miongoni mwa wiano za juu zaidi ulimwenguni. Kina mama 673 hufariki kwa kila watoto 100,000 wanaozaliwa wakiwa hai. Vile vile, kiwango cha vifo vya watoto mwanzoni mwa kipindi cha uchanga piakilikuwa juu sana ambapo watoto 39 walifariki katika juma la kwanza la maisha kwa kila watoto 1,000 waliozaliwa wakiwa hai. Afrika ni mojawapo ya bara ambako nusu ya jumla ya vifo vya watoto wachanga hutokea.
Kipindi hiki chenye hatari ya juu pia ndio wakati ulio na kiwango cha chini cha matumizi ya huduma za kiafya kwa kina mama na watoto barani Afrika. Hii ndiyo sababu ya pili inayokulazimu kuzingatia sana utunzaji baada ya kuzaa.
Ikiwa watoto wote wachanga watapokea utatuzi bora na kwa gharama nafuu katika kipindi cha baada ya kuzaa, imekadiriwa kuwa vifo vya watoto wachanga vinaweza kupunguzwa kwa asilimia 10-27. Hii ina maana kuwa, kiwango cha juu cha matumizi ya utunzaji wa baada ya kuzaa kinaweza kuokoa maisha ya watoto wachanga 60,000 kila mwaka barani Afrika na kuisaidia nchi hiyo kutimiza Lengo la Milenia la Maendeleo la kupunguza vifo vya watoto walio chini ya umri wa miaka mitano kwa theluthi mbili kufikia mwaka wa 2015.
Kwa kweli, utunzaji wa baada ya kuzaa ni bora ukitolewa katika kituo cha afya. Hata hivyo, kutokana na sababu nyingi za kijamii, kiuchumi na kitamaduni kama vile umbali na gharama ya kwenda kuhudumiwa, kina mama wengi vijijini huzalia nyumbani. Kwa hivyo, njia halisi zaidi ya kutoa utunzaji baada ya kuzaa katika siku za usoni barani Afrika huenda iwe ni kwa mhudumu wa afya kama wewe kuwatembelea nyumbani.
Kina mama na watoto wao wachanga wamo katika hatari zaidi ya kufariki mwanzoni mwa kipindi cha uchanga, hasa saa 24 za kwanza baada ya kuzaa na katika siku saba za kwanza baada ya kuzaa (tazama Jedwali 1.1). Jinsi unavyoweza kuona katika jedwali, asilimia 45 hadi 50 ya vifo vya kina mama na watoto wachanga hutokea katika saa 24 za kwanza baada ya kuzaa. Asilimia 65 hadi 75 ya vifo vya kina mama na watoto wachanga hutokea katika muda wa juma moja baada ya kuzaa. Huu ni ushahidi unaolazimu utoaji wa utunzaji bora na kikamilifu kwa kina mama na watoto wachanga katika siku chache za kwanza baada ya kuzaa.
Vifo baada ya kuzaa | Saa 24 za kwanza (%) | Siku saba za kwanza (%) |
---|---|---|
Vifo vya kina mama | 45 | 65 |
Vifo vya watoto wachanga | 50 | 75 |
Kwa hali fulani zinazohatarisha maisha ya mama na mtoto mchanga, utunzaji bora baada ya kuzaa hutolewa katika saa na siku chache za kwanza au baadaye kwa kuchelewa. Hali hizi za kiafya zinapotambulika mapema ndivyo zinavyoweza kuthibitiwa kikamilifu; ndivyo mama na mtoto wanavyopewa rufaa ya kupata matibabu spesheli kwa haraka na ndivyo matokeo yatakavyokuwa mazuri. Nyingi za tatuzi hizi hutegemea sana wakati. Unapaswa kuzingatia haya unapotoa utunzaji kwa kina mama na watoto wao siku chache za kwanza za maisha baada ya kuzaa.
Lengo kuu la kutoa utunzaji bora baada ya kuzaa ni kuzuia vifo vya kina mama na watoto wachanga na vile vile matatizo ya muda mrefu. Unapaswa kujua visababishi vikuu vya vifo katika kipindi cha baada ya kuzaa ili uweze kutoa utunzaji bora wa baada ya kuzaa na kwa wakati ufaao pale nyumbani na katika kituo cha afya.
Kujua ni nini hasa kinachosababisha vifo vya kina mama na watoto wachanga ni muhimu kwa kutambua hatua muhimu zinazowezakutatuavisababishi vikuu vya vifo katika kipindi baada ya kuzaa. Jedwali 1.2 linaonyesha asilimia ya vifo vya kina mama na visababishi vikuu vya vifo hivi kwa wanawake barani Afrika.
Ulijifunza kuhusu anemia, matatizo yanayosababisha shinikizo la damu, na uavyaji mimba katika vikao vya18, 19 na 20 vya somo katika Moduli ya utunzaji katika ujauzito. Vizuizi na kutokwa na damu nyingi wakati wa kuzaa vilifundishwa katika Vikao vya 9 na 11 vya moduli ya utunzaji katikauchungu wa kuzaa na kuzaa.
Visababishi vya vifo vya kina mama | Asilimia (%) |
---|---|
Kutokwa na damu nyingi baada ya kuzaa | 34 |
Maambukizi ya sehemu fulani au yaliyosambaa (Sepsisi) | 16 |
Matatizo yanayosababisha shinikizo la damu katika ujauzito (ugonjwa wa ujauzito, eklampsia) | 9 |
VIRUSI VYA UKIMWI/ UKIMWI | 6.2 |
Vizuizi katika kuzaa | 4 |
Uavyaji mimba | 4 |
Anemia | 4 |
Visababishi vingine vya vifo | 30 |
Jedwali 1.3 linaonyesha visababishi vya vifo vya watoto wachanga barani Afrika. Utajifunza kuhusu utunzaji maalum kwa watoto waliozaliwa kabla ya muda wa ujauzito kuisha na waliozaliwa na uzani wa chini katika Kipindi cha 8 cha somo cha Moduli hii.
Maambukizi, yakiwemo magonjwa ya kuhara na pepopunda, yameelezewa kwa undani katika Moduli juu ya magonjwa ya kuambukiza. Asifiksia ya kuzaliwa na uhaisho (urejeshaji uhai wa mtu mahututi) wa mtoto mchanga yaliangaziwa katika Kipindi cha 7 cha somo cha moduli juu ya utunzaji katika uchungu wa kuzaa na kuzaa.
Visababishi vya vifo vya watoto wachanga | Asilimia (%) |
---|---|
Maambukizi: | 47 |
| 3 7 37 |
Asifiksia ya kuzaliwa | 25 |
Kuzaliwa kabla ya muda wa ujauzito kuisha na kuzaliwa na uzani wa chini | 25 |
Ulemavu wa kuzaliwa | 4 |
Visababishi vingine vyote | 7 |
Je, kwa nini ni muhimu sana uelewe visababishi vikuu vya vifo vya kina mama na watoto katika kipindi cha baada ya kuzaa?
Huenda ulifikiria sababu nyingi, lakini iliyo bayana zaidi ni tofauti kubwa inayoweza kuletwa na utoaji wa utunzaji bora wa baada ya kuzaa na kwa wakati ufaao kwa kiwango cha vifo vya watoto wachanga barani Afrika: kupungua kwa asilimia 10 hadi 27 ya vifo vya watoto wachanga au kuokoa maisha ya takribani watoto wachanga 60,000.
Mwisho wa jibu
Fikiria kuhusu visababishi vikuu vya vifo vya kina mama na watoto wachanga. Je, ni vipi unavyotarajia kukumbana navyo unapotekeleza jukumu lako kama mhudumu wa afya nje ya hospitali?
Ukitumia takwimu zilizo kwenye Jedwali 1.2 na 1.3, basi huenda ulitaja kutokwa na damu nyingi baada ya kuzaa kwa kina mama, na aina fulani ya maambukizi kwa watoto na kina mama. Huenda pia ulichagua eklampsia na asifiksia ya watoto wachanga.
Mwisho wa jibu.
Saa 4-6 za kwanza baada ya kuzaa ndicho kipindi ambapo mama anaweza kuathiriwa sana na matatizo yatokanayo na kutokwa na damu nyingi. Visababishi huwa kupoteza damu nyingi kupitia katika eneo ambapo plasenta ilikuwa imejishikiza kwenye uterasi ya mama au kupasuka kwa uterasi wakati wa uchungu wa kuzaa na kuzaa. Kutokwa na damu kabla ya kuzaa pia kunaweza kuhatarisha maisha ya mtoto kwa kumkosesha oksijeni na virutubishi.
Mama pamoja na mtoto wamo katika hatari kubwa ya kukumbwa na matatizo mengine ikiwa marekebisho ya kifiziologia yanayotokea katika miili yao hayatatokea ifaavyo baada ya kuzaa. Hii inaweza kusababisha ukosefu wa utendaji kazi au ukatizaji wa usambazaji wa mahitaji muhimu ya oksijeni na virutubishi vinavyohitajika kudumisha maisha.
Kuna kupoteza damu na viowevu vingine vya mwili (kwa mfano kupitia kutapika na kutokwa na jasho) kusikoweza kuepukika wakati wa uchungu wa kuzaa. Hata hivyo, wanawake wengi wanaweza kustahimili haya. Upotezaji huu wa viowevu ni kawaida kwa kiwango fulani. Aidha, wanawake wengi hubaki katika uchungu wa kuzaa kwa saa nyingi bila kula wala kunywa, jambo ambalo linaweza kuwafanya wakose maji mwilini. Wasipopewa maji mwilini kwa haraka baada ya kuzaa, wana uwezekano wa kupata matatizo ya kifiziolojia
Katika ujauzito, shughuli hubadilika katika karibu mifumo yote ya mwili wa mama, ikiwemo moyo, mapafu, kiasi cha damu na vilivyo kwenye damu, mfumo wa uzazi, matiti, mfumo wa kingamwili na homoni. Katika kipindi baada ya kuzaa, mifumo hii yote ya mwili yenye kubadilika sharti ibadilike kutoka katika hali ya ujauzito hadi hali ilivyokuwa kabla ya ujauzito. Kuna uwezekano wa hatari ya matatizo marekebisho haya yanapotendeka. Mifano ya matatizo yanayotokea sana ni maambukizi ya matiti na mivilio ndani ya vena (vibonge vya damu ndani ya vena za miguu), ambayo yameelezewa katika Kipindi cha 3 cha somo kwenye Moduli hii. Kipindi ambapo marekebisho haya ya kifiziologia hufanyika katika mwili wa mama aliyezaa huitwa puperiamu. Utajifunza kuhusu haya yote katika Kipindi cha 2 na cha 3 cha somo.
Aidha, uchungu wa kuzaa ni tukio lenye maumivu kwa wanawake wengi, hasa wale wanaozaa kwa mara ya kwanza. Wanawake pia hupata fadhaa na mhangaiko kuhusu jinsi matokeo ya uchungu wa kuzaa utakavyokuwa. Kuwa na mtoto ni furaha (Picha 1.1), lakini pia inaweza kuwa chanzo cha wasiwasi. Wanawake walio katika kipindi cha baada ya kuzaa mara nyingi hukabiliana na hali ya mfadhaiko na hivyo wanahitaji usaidizi wa kisaikolojia.
Akiwa kwenye uterasi, mtoto huwa amelindwa vizuri na membreni za fetasi na kiowevu kizuia-bakteria cha amnioni ambamo fetasi hiyo huwa, vile vile na antibodi za mama zinazopitia kwenye plasenta na kuilinda dhidi ya maambukizi ambayo mama huyu ashakabiliana nayo. Antibodi kwenye kolostramu (maziwa ya kwanza ya mama) na maziwa komavu ya mama pamoja na vizuizi asilia kama vile ngozi ya mtoto humpa mtoto mchanga kiasi kikubwa cha kinga dhidi ya maambukizi anayopata mara tu anapozaliwa. Mfumo wa kingamwili wa mtoto huyu utachukua miezi kadhaa kabla ya kukua kikamilifu.
Mfumo wa mzunguko wa damu wa mtoto huyu mchanga ni mkumbwa na marekebisho kadhaa anapopumua kwa mara ya kwanza nje ya uterasi. Kiasi kidogo cha damu huenda kwenye mapafu mtoto akiwa ndani ya uterasi kwa sababu hapumui hewa. Mapafu ya fetasi hayawezi kutekeleza mbadilishano wa gesi (kufyonza oksijeni na kutoa dioksidi ya kaboni) unaofanyika tangu kuzaliwa na kuendelea.
Je, mbadilishano wa gesi hufanyika wapi kwa mtoto akiwa kwenye uterasi?
Oksijeni hufyonzwa katika damu ya fetasi kutoka kwa damu ya mama mifumo hii inapokaribiana katika plasenta; dioksidi ya kaboni kutoka kwa fetasi huingia katika damu ya mama na kutolewa kutoka kwa mwili wake kupitia katika pumzi yake.
Ulijifunza kuhusu mbadilishano wa gesi kwenye plasenta katika Kipindi cha 6 cha somo kwenye moduli ya Utunzaji katika Ujauzito.
Mwisho wa jibu
Mara tu baada ya kuzaliwa, mishipa ya damu inayopita kwenye mapafu hufunguka na kisha damu yote katika mzunguko wa mtoto iweze kupita kwenye mapafu, ambapo mbadilishano wa gesi hufanyika. Ni wakati muhimu sana kwa mtoto mchanga mapafu yanapoanza kufanya kazi. Kutopumua ni sababu ya kawaida ya asfiksia ya kuzaliwa. Pia watoto waliozaliwa kabla ya muda wa ujauzito kuisha, mara nyingi huwa na ugumu wa kupata oksijeni ya kutosha kwa sababu mapafu yao hayajakomaa kikamilifu na kwa hivyo mbadilishano wa gesi hautafanyika ifaavyo.
Utajifunza mengi kuhusu ugonjwa wa manjano kwa watoto wachanga katika Kipindi cha 6 cha na pia kwenye moduli juu ya Udhibiti Unganifu wa Maradhi ya Watoto Wachanga na ya Utotoni.
Mtoto akiwa kwenye uterasi, kemikali nyingi zenye sumu au uchafu huondolewa mwilini mwake na plasenta inayozielekeza kwenye ini ambapo huharibiwa (mchakato unaoitwa uzimuaji sumu). Baada ya kuzaliwa, ini la mtoto hulichukua jukumu hili na kuzimua sumu kwenye uchafu wa kemikali unaotengenezwa mwilini au kuingiziwa mdomoni. Mojawapo ya majukumu yanayotekelezwa na ini ni kuizimua sumu kwenye protini iitwayo bilirubini. Protini hii hutolewa kwa seli zee nyekundu za damu zinapoharibiwa. Seli nyekundu za damu huishi kwa muda mfupi tu na kuharibiwa na kisha seli nyekundu mbadala kutolewa. Ini la mtoto lisipoweza kustahimili kiwango cha seli zee nyekundu zinazofaa kuharibiwa, bilirubini hulimbika katika mwili wa mtoto na kuifanya ngozi yake iwe na umanjano. Hali hii huitwa ugonjwa wa manjano kwa watoto wachanga na ni hatari sana hasa ngozi ya viganja vya mikono na nyayo za miguu inapoonyesha umanjano.
Figo za mtoto mchanga pia huchangia pakubwa katika uondoaji wa kemikali zenye sumu zinazoondolewa mwilini kupitia kwa mkojo. Uchanga katika utendakazi wa figo pia unaweza kusababisha matatizo kwa watoto wachanga kemikali zenye sumu zinapolimbika mwilini.
Dhania kuwa unazungumza na mama wa mtoto mchanga kisha akuambie kuwa mtoto alizaliwa kabla ya muda wa ujauzito kuisha. Je, ni nini unachopaswa kutilia shaka na kushughulikia mara moja?
Kwanza chunguza ikiwa mtoto anakula vizuri. Fikiria kuhusu uchanga wa mapafu ya mtoto aliyezaliwa kabla ya muda wa ujauzito kuisha na uchunguze ikiwa mtoto huyu anaonyesha dalili zozote za matatizo ya kupumua. Pia zingatia uchanga wa figo na ini kisha uchunguze ikiwa ana dalili za ugonjwa wa manjano.
Mwisho wa jibu
Hauwezi kusadiki kuwa kufanikiwa kwa mama katika kuzaa na ubora wa afya yake na ya mtoto wake mchanga mwanzoni mwa kipindi cha baada ya kuzaa ni kigezo kuwa wataendelea katika hali njema. Matatizo yanaweza kutokea kutokana na marekebisho ya kifiziolojia kwa mama na mtoto mchanga yaliyoelezewa hapo awali (ambayo tutajadili kikamilifu katika Kipindi cha baadaye kwenye moduli hii) na mabadiliko ya haraka ambayo sharti yafanyike kwa mtoto ili azoee maisha katika mazingira ya nje. Kwa hivyo, unafaa uchunguze kwa makini dalili za hatari mwanzoni na katika muda wa mwisho wa kipindi cha baada ya kuzaa. Kabla hujamruhusu mama na mtoto kwenda nyumbani (iwapo alizalia kwenye Kituo cha Afya) au kabla ya kuwaacha nyumbani kwao baada ya mama kuzaa, wachunguze kwa muda wa saa sita za kwanza baada ya kuzaa. Ikiwa haukuweza kuhudumia uzazi huo, watembelee mapema uwezavyo katika saa 24 za kwanza, na hasa katika saa sita za kwanza.
Katika saa sita za kwanza, mkague mama huyo kwa dalili za hatari zifuatazo:
Mpe mama rufaa mara tu unapoona dalili zozote za hatari peleka mtoto pia.
Unapaswa kumkagua mtoto mchanga kwa dalili zifuatazo katika saa sita za kwanza:
Unyonyeshaji umeelezewa kikamilifu katika Kipindi cha 7 cha somo.
Uzuiaji wa hipothemia kwa kutumia ‘kanuni ya msisimko fululizi’ umeelezewa kikamilifu katika Kipindi cha 7 cha somo.
Kiasi kamili cha damu kwa mtoto mchanga mwenye uzani wa wastani ni milimita 240 pekee; hata kupoteza milimita 30 za damu kunatosha kusababisha mshtuko.
Katika safari ya kwanza ya utunzaji baada ya kuzaa, unapaswa kukumbuka:
Watoto waliozaliwa kabla ya muda wa ujauzito kuisha na waliozaliwa na uzito wa chini ndio mada ya Kipindi cha 8 cha somo.
Uhamasishaji wa jamii hufasiliwa kama shughuli zinazoanzishwa na jamii au watu wengine ambazo hupangwa, hutekelezwa na kutathminiwa na wanajamii, mashirika au vikundi ili kusuluhisha matatizo ya kiafya katika jamii. Katika Kipindi hiki cha somo tunalengo matatizo ya kiafya yanayotokea katika kipindi cha baada ya kuzaa. Uhamasishaji wa jamii ni mchakato endelevu na limbikizi wa mawasiliano, elimu na mpangilio ili kujenga nafasi za uongozi na utekelezaji.
Kisanduku 1.1 linatoa muhtasari wa mbinu kuu za uhamasishaji wa jamii. Hapa tunaziangazia kwa kifupi kwa sababu ushakumbana na mbinu zote katika moduli juu ya Elimu ya Afya, Utetezi na Uhamasishaji wa Jamii.
Mabango: Mabango yaliyobuniwa vizuri na kuwekwa mahali panapofaa yanaweza kuwasilisha jumbe ili kuwakumbusha watu mara kwa mara kuhusu suala husika.
Uandikaji barua: Hii ni njia moja ya kuwasilisha jumbe za kiafya kwa wanajamii wasomi. Barua hutoa ujumbe sahihi na inaweza kuwekwa ili kurejelewa baadaye.
Kurasa zenye vielelezo: Picha ni njia nzuri ya kufikisha ujumbe kwa watu wasioweza kuelewa barua kutokana na ujuzi wao haba wa kusoma(Picha1.3).
Kuwatembelewa nyumbani: Hii ndio njia bora zaidi ya kuihamasisha jamii kwa sababu unaweza kuwa na hakika kuwa ujumbe umewasilishwa.
Msingi wa uhamasishaji wa jamii ni kushiriki pakubwa kwa jamii ambako hufanyika wanajamii wanaposhiriki katika kutambua matatizo na mahitaji na kisha wapange, watekeleze, wasimamie na kutathmini shughuli za jamii ili kutatua tatizo hilo.
Kanuni ya kimsingi unayofaa kukumbuka ni kuwa hauko pale ‘kushurutisha’ ushiriki wa jamii. Wajibu wako ni kuchunguza, kujifunza kutoka kwa hekima ya jamii na kuelimisha na kuwarai wanajamii kuleta mabadiliko yatakikanayo - katika muktadha huu, kuboresha matokeo baada ya kuzaa. Neno na uamuzi wa mwisho huwa ya jamii.
Watu huwajibika wanapohusika na kushiriki katika shughuli fulani. Hii husaidia kwa kudumisha ari, shughuli na mipango. Pia ina manufaa haya:
Watu wa kwanza kulenga kwa utunzaji wa baada ya kuzaa ni mama, mtoto wake mchanga na baba. Hata hivyo kuna watu wa kulenga baadaye ambao ni watu mashuhuri katika jamii wanaoweza kushawishi uamuzi unaoathiri afya ya mama na mtoto. Unahitaji kuwahusisha watu hawa kutoka mwanzo unapotanguliza huduma za utunzaji wa baada ya kuzaa katika jamii yako. Zingatia kuhusisha:
Bila ushirikiano wa watu binafsi na vikundi hivi, itakuwa vigumu kutoa utunzaji bora baada ya kuzaa. Hasa ni muhimu kuimarisha uhusiano bora na upatanishe juhudi zako na za wakunga wa kienyeji. Shughuli zifuatazo zitakusaidia kutimiza haya (Kisanduku 1.2)
Je, kwa nini unafikiri ni muhimu kuwahusisha wakunga na madaktari wa kienyejii jinsi ilivyoelezewa hapo awali?
Wao ni wambia muhimu kwa sababu wanajua desturi za mahali pale, wanaheshimiwa na wanajamii na wana uzoefu mwingi wa kukabiliana na mengi ya matatizo ya kijamii yanayotokea katika kipindi baada ya kuzaa.
Mwisho wa jibu
Dhania kuwa wewe ni mkunga wa kienyenji mwenye uzoefu wa miaka mingi. Muhudumu wa afya nje ya hospitali anaanza kufanya kazi katika kijiji chako kisha aombe usaidizi wako. Je, ni mambo gani yanayoweza kukufanya uweze kushirikiana naye kusaidia kazi yake?
Kwa kweli jibu sahihi si moja tu kwa swali hili jinsi tu ilivyo kwamba majibu yote hayatamfaa mkunga mmoja kwa usawa. Hata hivyo huenda ulitaja pia yafuatayo:
Mwisho wa jibu
Ulijifunza jinsi ya kukagua wasifu wa jamii katika Kipindi cha 1 cha somo cha utunzaji katika ujauzito.
Unapaswa kujua idadi kamili ya watu unaoenda kuhudumia na jinsi ya kukusanya takwimu muhimu kama vile za uzazi, vifo na habari kuhusu uhamaji na uhamiaji wa watu katika sehemu hiyo. Unahitaji pia kuweka kumbukumbu ya wanawake wote walio katika umri wa uzazi (takribani miaka 15 hadi 45) ambao wanaweza kupata ujauzito siku za baadaye na iadadi ya wanawake wajawazito wakati huo na wanapotarajiwa kuzaa
Unapaswa kuandika majina na anwani za wakunga wote wa kienyeji, madaktari wa kienyeji, wanaouza dawa vijijini na madaktari wengineo wa kibinafsi. Sajili mifumo yote ya kijamii inayoweza kukusaidia kwa uhamasishaji wa raslimali za kibinadamu, kifedha na kiusafiri iwapo rufaa za dharura zitahitajika kwa mama na mtoto. Utajifunza kuhusu mfumo wa rufaa katika Kipindi cha mwisho cha somo katika moduli hili. Habari hii yote inafaa kutengenezwa na kuboreshwa zaidi kila baada ya miezi minne hadi sita.
Huenda usihitaji kuendesha umahasishaji wa jamii kivyake kwa utunzaji wa baada ya kuzaa. Uhamasishaji huu unapaswa kufanywa kwa pamoja na wa huduma za afya kwa kina mama, watoto wachanga na watoto katika jamii. Kisanduku 1.3 Ni muhtasari wa shughuli za uhamasishaji wa jamii ili kuendeleza utunzaji wa baada ya kuzaa.
Katika Kipindi cha 1 umejifunza kuwa:
Kwa kuwa umekamilisha Kipindi hiki cha somo, unaweza kutathmini ni kwa kiwango kipi umeweza kuyatimiza malengo ya somo hili kwa kujibu maswali yafuatayo. Andika majibu yako katika shajara yako kisha ujadiliane na mkufunzi wako katika mkutano saidizi wa masomo utakaofuata. Unaweza kulinganisha majibu yako na muhtasari juu ya maswali ya kujitathmini yaliyo mwishoni mwa moduli hii.
Ifuatayo ni orodha ya maneno muhimu yaliyotumiwa katika Kipindi hiki cha somo. Kila neno na ufafanuzi. Ni ufafanuzi upi hapa chini ulio (i) sahihi kabisa (ii)sahihi kwa kiasi fulani na (iii) si sahihi. Andika sentensi fupi kwa kila mmoja wa ufafanuzi ulio sahihi kwa kiasi fulani au usio sahihi kwa kulitumia neno hilo kwa usahihi.
Mwisho wa jibu
Dhania kuwa unajaribu kumshawishi Waziri wa Fedha wa bara Afrika kuweka pesa zaidi kwa utunzaji wa kiafya baada ya kuzaa na anataka ushahidi kuhusu sababu zake kufanya hivyo. Andika barua fupi ukieleza kwa muhtasari hoja kuu utakazosisitiza.
Kuna hoja nyingi unazoweza kumtolea Waziri huyo wa Fedha. Zifuatazo ni baadhi ya zile muhimu:
Mwisho wa jibu
Umefanya kazi nzuri kumshawishi Waziri wa Fedha. Hata hivyo, amemtaka Waziri wa Afya achunguze na kuthibitisha ikiwa kweli unafahamu unachokizungumzia. Anakutaka uorodheshe dalili kuu za matatizo yanayoweza kutokea unazopaswa kuchunguza kwa mama aliyezaa na dalili kuu za hatari kwa mtoto mchanga. Je, utaandika nini katika orodha yako?
Dalili za hatari kwa mama aliyezaa:
Dalili kuu za kuchunguza ni ukosefu wa maji mwilini, uterasi isiyopungua ipaswavyo, kutokwa na damu upya, kupungua kwa shinikizo la damu na kupanda kwa mpwito wa ateri. Dalili za hatari za muda mrefu unazopaswa kujua ni kuganda kwa damu na dipresheni.
Dalili za hatari kwa mtoto mchanga
Unayopaswa kuchunguza kwanza ni: je, mtoto ananyonya vizuri, rangi ya ngozi ni ya kawaida au ni ya manjano, kuna joto la juu mwilini, mtoto ni baridi au vuguvugu sana akiguswa, kupumua ni kwa kawaida, kuna kutokwa na damu, vigubiko vya macho ya mtoto ni vyekundu au vimevimba? Pia utachunguza ikiwa mtoto alizaliwa kabla ya muda wa ujauzito kuisha ili kutambua ikiwa yuko katika hatari zaidi ya kupata matatizo mengine. Huenda ulipata mengi ya haya. Ikiwa haukupata mengi ya haya au hauwezi kukumbuka yanayoashiria, soma tena sehemu 1.5.2 ‘kumtathmini mtoto mchanga’
Mwisho wa jibu.