Skip to main content
Printable page generated Friday, 19 April 2024, 1:23 AM
Use 'Print preview' to check the number of pages and printer settings.
Print functionality varies between browsers.
Unless otherwise stated, copyright © 2024 The Open University, all rights reserved.
Printable page generated Friday, 19 April 2024, 1:23 AM

6. Husika kwa Utendeti katika Kudhibiti Awamu ya Tatu ya Leba

Kipindi cha 6 cha Somo Husika kwa Utendeti katika Kudhibiti Awamu ya Tatu ya Leba

Utangulizi

Katika kipindi kilichopita, ulijifunza zaidi kuhusu kuvuja damu baada ya kuzaa. Hali hii ni mojawapo ya visababishi vikuu vya vifo vya kina mama vinavyo husiana na kuzaa. Kuvuja damu baada ya kuzaa husababisha 1/4 ya vifo vyote vya kina mama vinavyo husiana na kuzaa. Duniani kote, takriban wanawake 127,000 hufa kila mwaka kutokana na kuvuja damu baada ya kuzaa. Vingi vya visa hivi vya kuvuja damu kwa wingi hutokea katika saa 24 za kwanza baada ya kuzaa. Vifo hivi husababishwa na matatizo katika awamu ya tatu ya leba. Ili kupunguza hatari ya kuvuja damu baada ya kuzaa, wahudumu wote wa kuzalisha wanafaa kufuata mseto wa hatua maalum zilizowekwa. Hatua hizi hujulikana kama udhibiti tendeti la awamu ya tatu ya leba (UTATL). Utaratibu wa UTATL unapofanywa inavyofaa, hatari ya kuvuja damu baada ya kuzaa hupunguzwa kwa zaidi ya 60%.

Katika kipindi hiki, utajifunza kuhusu UTATL na mambo ya kufanya katika hatua zote 6. Maarifa haya yatakusaidia kutambua na kuyadhibiti kikamilifu matatizo yanayoweza kutokea katika awamu ya tatu ya leba.

Matokeo ya Masomo ya Kipindi cha 6

Baada ya kipindi hiki, unatarajiwa:

6.1 Kufasili na kutumia kwa usahihi maneno yote muhimu yaliyo andikwa kwa herufi nzito. (Swali la Kujitathmini 6.1 )

6.2 Kueleza utaratibu halisia wa kifisiolojia wa kutolewa kwa plasenta. (Swali la Kujitathmini 6.1 )

6.3 Kueleza hatua zote 6 za udhibiti tendeti wa awamu ya tatu ya leba (UTATL). (Swali la Kujitathmini 6.2 )

6.4 Kuandika kwa muhtasari taratibu zote za kila dawa ya uterasi inayotumiwa katika UTATL. (Swali la Kujitathmini 6.2 na 6.3)

6.5 Kueleza jinsi ya kuchunguza plasenta na membreni ili kubaini kama zimetoka zingali nzima. (Swali la Kujitathmini 6.3 )

6.6 Kueleza dalili hatari zinazoashiria matatizo yanayoweza kutokea katika awamu ya tatu ya leba. (Swali la Kujitathmini 6.4 )

6.1 Awamu ya tatu ya leba

Awamu ya tatu ya leba huanza kwa kuzaliwa kwa mtoto na kuisha kwa kutolewa kwa plasenta na membreni za fetasi. Kwa kawaida, uatratibu huu unafaa kuchukua chini ya dakika 30.

6.1.1 Taratibu za asilia katika awamu ya tatu ya leba

Katika leba ya kawaida, awamu ya tatu ni wakati taratibu asilia za kifisiolojia huusababisha kutolewa kwa ghafla kwa plasenta na membreni za fetasi. Ni sharti seviksi ibakie wazi na uterasi kukazana vyema ili mama asikumbwe na matatizo. Katika kauli nyingi, taratibu hizi hutokea katika mfululizo ufuatao.

  1. Kutengeka kwa plasenta:Plasenta hutengana na pembeni mwa uterasi (Mchoro 6.1a na b)Plasenta inapobambuka, damu iliyo ndani ya vishipa vidogo kwenye mzizi wa plasenta huanza kugandia katikati mwa plasenta na misuli ya pembezoni mwa uterasi. (Pembezo hii ya uterasi hujulikana kama miometriamu).
  2. Kushuka kwa plasenta:Baada ya kutengeka, plasenta hushukia chini ya njia ya uzazi hadi kupitia seviksi iliyopanuka (Mchoro 6.1c).
  3. Kutolewa kwa plasenta:Plasenta hutolewa kabisa kutoka kwenye njia ya uzazi (Mchoro 6.1d).

Utaratibu huu wa kutolewa kwa plasenta huashiria awamu ya tatu ya leba. Misuli ya uterasi huendelea kukazana kwa kishindo hivyo kuigandamiza mishipa ya damu iliyochibuka. Tuko hili pamoja na kuganda kwa damu husitisha kuvuja kwa damu baada ya kuzaa.

Mchoro 6.1 (a) Plasenta bado haijatengeka mwanzoni mwa awamu ya tatu. (b) Plasenta inaanza kutengeka huku vidonge vya damu vikianza kugandia chini yake. (c) Plasenta inashukia seviksini. (d) Plasenta imetolewa kabisa, ikiashiria mwicho wa awamu ya tatu. Uterasi inakazana kwa kishindo. (Rejeo: Shirika la Afya Duniani, 2008, {1} Moduli ya Elimu ya Ukunga: Kudhibiti Kuvuja kwa Damu baada ya Kuzaa, Vielelezo 1.5 hadi 1.7, uk 22-23)

6.1.2 Matatizo katika awamu ya tatu ya leba

Kipindi cha 11 kinaelezea kwa kina kuhusu kuvuja kwa damu baada ya kuzaa na uterasi isiyo na mikazo. Istilahi zingine zilizo kwenye Kisanduku 6.1 zimeelezwa katika kipindi hiki.

Wanawake wanaozaa bila usaidizi wa mhudumu wa afya aliyehitimu wako katika hatari kuu zaidi ya kukumbwa na matatizo katika awamu zote za leba. Kisanduku 6.1 kinaorodhesha matatizo yanayoweza kutokea katika awamu ya tatu. Matatizo yanaweza kutokea hata wakati plasenta imepandikika vyema katika sehemu ya 2/3 ya uterasi. Matatizo yanaweza kutokea wakati leba haijaendelea kwa muda mrefu na wakati utaratibu wa kuzaa ni wa kawaida. Katika leba ya kawaida, plasenta inatarajiwa kutolewa kwa utaratibu wa kawaida na unaojianzisha wenyewe katika awamu ya tatu ya leba. Hata hivyo, matatizo yanaweza kutokea. Jiweke tayari kwa jambo lolote la dharura lisilotarajiwa.

Kisanduku 6.1 Matatizo yanayotokea mara nyingi katika awamu ya tatu ya leba

Matatizo yafuatayo yanaweza kutokea iwapo hutatumia utaratibu wa UTATL kudhibiti awamu ya tatu.

Plasenta iliyosalia

Plasenta inasalia ndani ya uterasi kwa zaidi ya dakika 30 baada ya mtoto kuzaliwa. Plasenta husalia kufuatia sababu zifuatazo:

  • Mikazo ya uterasi ni hafifu sana, hivi kwamba haisukumi plasenta nje.
  • Seviksi ilirejea upesi sana huku ikifungika nusu. Plasenta imekwama ndani ya uterasi.
  • Kibofu kimejaa hivyo kuzuia kutolewa kwa plasenta.
Kuvuja damu kwa wingi

Kuvuja damu baada ya kuzaa ni hali ambapo mama anavuja zaidi ya mililita 500 za damu baada ya kuzaa. Damu nyingi huvujia katika sehemu ambapo plasenta ilikuwa imeshikamana na uterasi. Damu ni ng’avu au nzito na yenye kunata. Damu nyingi huvuja iwapo uterasi haikazani ifaavyo, hasa kufuatia sababu hizi:

  • Plasenta iliyotengeka nusu huku ikibaki imejipandikiza kwenye pembezo mwa uterasi.
  • Plasenta iliyotengeka kabisa lakini inayosalia ndani ya uterasi.
  • Uterasi isiyo na mikazoMisuli ya pembezo mwa uterasi haikazani kwa nguvu za kutosha kusitisha damu kuvuja baada ya plasenta kutengeka.
Kugeuka kwa uterasi

Sehemu ya ndani ya uterasi huvutika hadi kuja juu mtoto au plasenta inapotolewa. Sehemu ndogo ya uterasi hutokezea ukeni.

6.2 Udhibiti tendeti katika hatua ya tatu ya leba (UTATL)

Mkunga anapotumia udhibiti tendeti katika hatua ya tatu ya leba (UTATL), hatari ya matatizo kama yalivyoorodheshwa katika Kisanduku 6.1 hupunguzwa. Neno ’’udhibiti tendeti’’ linaashiria kuwa hautasubiri hadi plasenta ijitoe yenyewe. Badala yake, unafaa kusaidia kwa namna iliyopangwa kwa utaratibu kama ifuatavyo:

  • Punde mtoto anapozaliwa, mlaze juu ya fumbatio la mama, huku miili yao ikiguzana. Wafunike wote kwa blanketi.
  • Ifinye kamba kitovu ya mtoto katika sehemu mbili ukitumia klempu, kisha ukate katikati, kama ulivyojifunza katika Kipindi cha 5.
  • Fuata hatua zilizo katika Kisanduku 6.2. Kitengo kinachofuata kinaelezea hatua hizi kwa kina.

Kisanduku 6.2 Hatua 6 za UTATL kwa mpangilio maalum

  1. Chunguza kama uterasi ina mtoto wa pili.
  2. Kwa muda wa chini ya dakika 1, mpe mama dawa ya kudungwa ndani ya uterasi, ambayo ni kemikali aina ya homoni inayofanya uterasi kukazana kwa nguvu zaidi.
  3. Tumia njia ya kuvuta kitovu taratibu.
  4. Ipapase uterasi punde tu baada ya plasenta kutolewa.
  5. Ichunguze plasenta. Hakikisha kuwa plasenta yote imetoka, wala hakuna sehemu yake iliyosalia ndani ya uterasi.
  6. Chunguza uke, periniamu na sehemu ya nje ya uke wa mama ili kutambua kama kuna mchibuko au damu inayovuja.

Hatua ya 1 Chunguza kama uterasi ina mtoto wa pili

Chunguza kama uterasi ina mtoto wa pili punde tu baada ya mtoto kuzaliwa. Papasa uterasi kupitia fumbatio la mama. Hakikisha kuwa uterasi haina mtoto wa pili. Kwa kutumia mikono, chunguza kama uterasi imerejea kimo kama cha umri wa wiki 24 za ujauzito. Baada ya kufanya hivi, nenda katika hatua ya 2. Chunguza kwa makini sana kwa sababu dawa unayompa mama kaatika hatua ya 2 hufanya uterasi ikazane kwa nguvu sana. Iwapo mtoto yuko ndani ya uterasi, anaweza kujeruhiwa. Iwapo kuna mtoto wa pili ndani ya uterasi, mpe mama dawa ya kukazisha uterasi baada ya mtoto huyu kuzaliwa.

Hatua ya 2 Mpe mama dawa ya kukazisha uterasi ili kuiwezesha kukazana

Dawa hizi za kukazisha uterasi mara nyingi hutumika katika taaluma ya ukunga:

  • misoprostol (tembe)
  • oxytocin (dawa ya kudungwa)
  • ergometrine (dawa ya kudungwa)

Dawa hizi huisaidia uterasi kukazana kwa nguvu na utaratibu maalum baada ya mtoto kuzaliwa. Dawa hizi husaidia katika kutolewa kwa plasenta na pia kuzuia damu kuvuja kwa wingi kutokana na uterasi isiyokazana. Dawa hizi tatu zinapatikana hata katika maeneo ya mapato ya chini, kama vile vijijini mwa Afrika. Hata hivyo, misoprostol inaweza kuwa dawa pekee unayoweza kutumia. Oxytocin ndiyo dawa iliyopendekezwa na Shirika la Afya Duniani, lakini haiwezi kutumika kwa sababu:

Vituo vya afya husambaziwa friji na sanduku la barafu ambazo hutumiwa kusafirishia dawa vijijini, kama ilivyoelezwa kwenye Moduli ya Chanjo

Ni sharti oxytocin na ergometrine zihifadhiwe katika kiwangojoto cha nyusi 2 -8. Dawa hizi haziwezi kutolewa katika nyumba zisizokuwa na friji au una sanduku la kubeba la barafu. Ni sharti pia dawa hizi zikingwe kutokana na mwangaza.

Vipimo vya dawa za kukazisha uterasi

Chini ya dakika moja baada ya mtoto kuzaliwa na umefinya kamba kitovu kwa klempu kisha kukata kamba kitovu, mpe mama mojawapo ya dawa zifuatazo:

  • misoprostol mikrogramu 600 (µg), yaani, tembe 3 za 200 µg za kunywewa kwa maji.

AU

  • oxytocin vipimo 10 vya kimataifa (IU) zinazodungwa ndani ya misuli ya paja la mama. Dawa hizi hujulikana kama dawa za kudungia ndani ya misuli.

AU

  • ergometrine miligramu (mg) 0.4–0.5 inayodungwa ndani ya misuli ya paja la mama.

Uterasi huwa ngumu inapokazana ifaavyo. Mabadiliko haya hutokea dakika 2 -7 baada ya kundunga dawa hii. Dawa hizi hutenda kazi kwa muda tofauti.

Ergometrine haipendekezwi kutumiwa na Wahudumu wa Afya Ugani.

Manufaa na mathara ya dawa za kukazisha uterasi

Misoprostol haina nguvu za kutenda kazi kama oxytocin. Misoprostol ina madhara zaidi ya ziada Hata hivyo, katika hali nyingi mle vijijini, ni sharti utumie misoprostol kwa sababu ni lazima oxytocin ihifadhiwe ndani ya friji au sanduku la barafu. Mshauri mama kuwa dawa hii huzuia kuvuja kwa damu, hata ingawa nafaa kutarajia madhara machache ya ziada. Dawa zote za kukazisha uterasi zina madhara ya ziada. Hata hivyo, misoprostol husababisha madhara kwa wanawake wengi zaidi. Yafuatayo ndiyo madhara ya misoprostol:

  • Mama anaweza kuanza kutetemeka saa 1 baada ya kupewa msoprostol . Kutetema huisha baada ya saa 2-6. Ishauri familia kumpa mama blanketi na chai ya “atmit” au iliyoashwa joto.
  • Ingawa ni nadra kupata kiwangojoto cha juu cha mwili, kinaweza kuanza mama anapokoma kutetema. Kiwangojoto cha juu hakiashirii ugonjwa kila kinapotambulika. Kiwangojoto cha juu huisha masaa 2-8 baada ya dawa hii kupeanwa.
  • Kuharisha hudumu kwa chini ya siku 1.
  • Kichefuchefu na kutapika huisha baada ya saa 2-6.
  • Je, manufaa makuu zaidi ya misoprostol ni yapi ikilinganishwa na dawa zingine za kukazisha uterasi.

  • Misoprotol ni tembe, hivyo hauhitaji sirinji na sindano. Misoprotol haihitaji kuhifadhiwa ndani ya friji, hivyo inaweza kutumika katika sehemu ambapo dawa zingine haziwezi kuhifadhika.

    Mwisho wa jibu

Oxytocin ndiyo dawa ya kukazisha misuli iliyopendekezwa iwapo kuna friji. Oxytocin hutenda kazi zaidi kuliko dawa zingine, na ina madhara machache zaidi. Oxytocin ni homoni inayopatikana kiasilia katika mwili wa mwanamke. Oxytocin huhusishwa kuanzia mwanzo wa mikazo ya uteras wakati wa leba, na pindi inavyoendelea. Mpe mama oxytocin ya kutengenezewa viwandani akishazaa. Dawa hii huiwezesha uterasi kuendelea kukazana taratibu, kama katika njia ya kiasili. Hata hivyo, hali hii haidumu kwa muda mrefu, hivyo ni sharti oxytocin ihifadhiwe ndani ya friji na kukingwa dhidi ya mwangaza.

Ergometrine haitumiki mara nyingi kwa sababu hii ni dawa ya kukazisha misuli yenye nguvu zaidi. Dawa hii inaweza kusababisha kufungika kwa seviksi kabla ya plasenta kutolewa. Ergometrine huchukua muda mrefu zaidi kufanya kazi kuliko oxytocin. (Baada ya kudungwa ndani ya misuli, ergometrine huchukua dakika 6-7 kufanya kazi.) Ergometrine husababisha mishtuko ya uterasi ambayo hukazana upesi huku mikazo hii ikidumu kwa muda, kinyume na mikazo ya kiasili. Hata hivyo, athari ya ergometrine hudumu kwa muda mrefu, saa 2-4.

Usitumie ergometrine katika Huduma ya Afya Ugani.Usimpe mama mwenye prieklampsia, eklampsia au shinikizo la damu. Ergometrine hufinya mishipa ya damu huku ikisababisha ongezeko la shinikizo la damu.

Hatua ya 3 Tumia njia ya kuvuta kitovu taratibu kwa msukumo pinzani.

Uterasi huwa ngumu inapokazana ifaavyo. Badiliko hili hufanyika dakika 2-3 baada ya kudunga dawa uterasini. Baada ya hatua hii, tumia njia ya kuvuta kitovu taratibu kwa msukumo pinzani ili kuitoa plasenta (Mchoro 6.2 na Kisanduku 6.3).

Unapotumia njia ya kuvuta kitovu taratibu, kumbuka KILA MARA kusuma fumbatio kwenda upande pinzani. Jambo hili hufanywa ili kuzuia kugeuka kwa uterasi. (Uterasi inapogeuka hupinduka hata sehemu yake ya ndani kuja juu kisha kutokezea ukeni.)

Mchoro 6.2 Kuvuta kitovu taratibu. Mkono wa kiume huvuuta kambakitovu iliyobanwa kwa klempu, kisha kuivuta. Wakati huo huo, mkono wa kushoto husukuma kwa msukumo pinzani kwenye sehemu ya chini ya fumbatio, juu ya mfupa wa kinena. (Rejeo: Shirika la Afya Duniani, 2008, {1} Moduli ya Elimu ya Ukunga: Kidhibiti Kuvuja Damu baada ya Kuzaa, Mchoro 1.18, uk 33)
Kisanduku 6.3 Jinsi ya kutumia njia ya kuvuta kitovu taratibu kwa msukumo pinzani
  1. Subiri hadi mishipa ya damu iliyo katika kambakitovu cha mtoto mzawa zisite kudunda. Ibane kambakitivu karibu na msamba, kisha uishika kambakitovu kwa mkono mmoja.
  2. Uweke mkono wa pili juu ya mfupa wa kinena wa mama. Lisukume fumbatio kwa msukumo pinzani ili kuiimarisha uterasi.
  3. Ikaze kambakitovu taratibu ukisubiri mkazo dhabiti wa uterasi. (Kwa kawaida, mikazo hutokea kila baada ya dakika 2-3.)
  4. Mhimize mama kusukuma sawa na mkazo dhabiti wa uterasi. Ivute kambakitovu taratibu ukiielekeza chini ili kuitoa plasenta. Endelea kuisukuma uterasi kwa msukumo pinzani.
  5. Mkazo mmoja unapokoma, ishike kambakitovu taratibu ukisubiri mkazo mwingine.
  6. Katika mkazo unaofuata, rudia utaratibu wa kuvuta kitovu taratibu kwa msukumo pinzani.
  7. Iwapo plasenta haishuki baada ya kuivuta kambakitovu taratibu kwa sekunde 30-40, usiendelee kuivuta kambakitovu.

Plasenta inapotoka, ishike kwa mikono yote kwenye vulva. Hii ni ili kuzuia membreni kuraruka, jambo ambalo linaweza kupelekea sehemu za membreni kusalia ndani ya mwili wa mama. Ishike plasenta kwa mikono yote miwili kisha uigeuze taratibu hadi membreni zipindika (Mchoro 6.3). Ivute plasenta taratibu ili kuiondoa kabisa.

Mchoro 6.3 Kutolewa kwa plasenta

Kutolewa kwa plasenta huashiria mwisho wa awamu ya tatu ya leba. Sasa uterasi inafaa kuwa ngumu, ya duara na inayoweza kusonga uterasi inapopapaswa. Unafaa kuihisi ikiwa katikati mwa kitovu cha mama na mfupa wa kinena. Uke haufai kuwa ukivuja damu. Kibofu kinafaa kuwa kitupu.

Hatua ya 4 Papasa uterasi

Ipapase uterasi punde tu baada ya plasenta kutolewa ili kuikazisha na kusitisha damu kuvuja. Wanawake wengi huhitaji kupapaswa uterasi ili kuisaidia kukazana (Mchoro 6.4).

Mchoro 6.4 Ipapase uterasi punde tu baada ya mtoto kuzaliwa. Baada ya kufanya hivyo, ipapase kila baada ya dakika 15 kwa saa 2, kisha uipapase kila baada ya dakika 30. Mwonyeshe mwanamke huyu jinsi ya kujipapasa mwenyewe, au apapaswe na jamaa zake.

Hatua ya 5 Ichunguze plasenta na tando za fetasi

Ichunguze plasenta kwa makini kuhakikisha kuwa hakuna sehemu iliyosalia ndani.

  • Kumbuka anatomi ya plasenta kutoka Moduli ya Utunzaji wa kabla ya Kuzaa, Kipindi cha 5. Je, sehemu ya juu ya mama ni upande wa juu ambapo kambakitovu hutokezea, au ni upande wa chini wa plasenta?

  • Sehemu ya juu ya plasenta ni upande wa chini, iliyo mkabala na sehemu ambapo kambakitovu hutokeza.

    Mwisho wa jibu

Kipande cha sehemu ya juu ya mama (Mchoro 6.5) kinaweza kuwa kinakosekana. Au unaweza kuona membreni ambazo zimeraruka zilizo na mishipa ya damu. Vipande hivyo vya plasenta husalia ndani ya uterasi. Mpendekezee mama rufaa ya dharura.

Mchoro 6.5 Chunguza sehemu ya chini(sehemu ya juu ya mama) ya plasenta kuthibitisha kuwa haijararuka.
Mchoro 6.6 Sehemu ya juu ya plasenta ni ile inayokabiliana na mtoto.
  • Eleza ni kwa nini unafaa kumpendekezea rufaa mwanamke aliye na plasenta ambayo ina vipande vilivyosalia ndani ya uterasi.

  • Vipande vya plasenta vilivyosalia ndani ya uterasi huongeza hatari ya kuvuja damu baada ya kuzaa.

    Mwisho wa jibu

Sehemu za duara zisizo na umbo maalum zilizo chiniya plasenta huitwa ndewe. (Baadhi ya vitabu vya masomo huziitakotilidoni. )Kinyume na matarajio, sehemu ya juu ya plasenta ni nyororo na ng’avu. Kitovu hujipandikiza upande huu, kisha kusambaa kama mishipa ya rangi ya sanawati nzito mfano wa mizizi ya mti (Mchoro 6.6).

Chunguza ili kuthibitisha kuwa plasenta ni nzima

  1. Ishike plasenta mikononi mwako, huku sehemu ya mama ikielekea juu. Hakikisha kuwa ndewe zote zipo na kuwa zimeshikana.
  2. Ishike kambakitovu kwa mkono mmoja, kisha uinin’ginize plasenta na membreni.
  3. Uweke huo mkono mwingine ndani ya membreni. Vitandaze vidole vyako kuchunguza kama membreni ni nzima (Mchoro 6.7).
Mchoro 6.7 Zitandaze membreni kuchunguza kama ni nzima
  1. Hakikisha kuwa kambakitovu imejipandikizana na plasenta kwenye sehemu ifaayo. Chunguza sehemu ya mwisho ya kambakitovu iliyokatwa kisha utafute ateri mbili na veni moja (Mchoro 6.8).
Mchoro 6.8 Sehemu ya mwisho ya kambakitovu iliyokatwa ina ateri mbili na veni moja.
  1. Itupe plasenta kwa namna inayofaa. Izike mahali ambapo haiwezi kufukuliwa na wanyama au uiangamize kwa kuchoma iwapo una vifaa vya kuchoma.
  2. Iwapo membreni zimeraruka, chunguza sehemu ya juu ya uke na seviksi ya mwanamke. Vaa glavu zilizotakaswa na utumie fosepu za sponji kuondoa vipande vyovyote vya membreni.

Iwapo vipande vya plasenta au membreni zimesalia ndani ya uterasi, mama huyu yuko hatarini.

Picha 6.9 Chunguza sehemu ya juu ya plasenta. Mfano wa plasenta umeonyeshwa. Ndewe zake zinafaa kuwa nzima. Hakuna dalili ya kuraruka plasenta inapotandazwa mkononi mwa mhudumu wa afya.

Hatua ya 6 Chunguza ili kutambua mikato, miraruko au kuvuja damu

Mchoro 6.10 Jeraha kubwa ukeni linaweza kusababisha kuvuja damu baada ya kuzaa.

Istilahi ya kimaumbile iliyo katika kifungu hiki ilielezwa na kufafanuliwa katika Kipindi cha 3 cha Moduli ya Utunzaji wa kabla ya Kuzaa, Sehemu ya 1 (Mchoro 3.2). Ili kuidhibti awamu ya tatu ya leba, fuata hatua zifuatazo:

  1. Kwa utaratibu, tenganisha labia kisha uichunguze sehemu ya chini ya uke na perineamu. Tafuta mejaraha yanayofaa kuzibwa ili kuzuia damu zaidi kuvuja (Mchoro 6.10)
  2. Kwa utaratibu, itakase vulva na perineamu kwa maji yaliyochemshwa na kupoeshwa au kiowevu hafifu cha antiseptiki.
  3. Finyilia padi au kitambaa safi kwenye sehemu inayovujia damu kwa dakika 10. Iwapo damu itaendelea kuvuja baada ya muda huu, mpendekezee mwanamke huyu rufaa mara moja. Endelea kufinya kwenye kidonda.
  4. Mfuatilie mwanamke huyu kwa dakika 15. Kadiria dalili zake muhimu, ipapase uterasi yake kuhakikisha imekazika na pia uchunguze kubaini damu inayovuja kuzidi kiasi.
  • Ni kwa nini ni muhimu kukamilisha hatua zote 6 za utaratibu wa UTATL? Utaratibu huu ni upi?

  • Ni muhimu kukamilisha hatua hizi katika utaratibu unaofaa. Utafiti unaonyesha kuwa iwapo UTATL inatumiwa vyema, inaweza kuounguza hatari ya kuvuja damu baada ya kuzaa kwa 60%. Kisanduku 6.2 kinaorodhesha hatua 6 kwa utaratibu maalum.

    Mwisho wa jibu

6.3 Usaidizi katika matatizo baada ya kutumia UTATL

6.3.1 Kuvuja damu kwa wingi

Katika Kipindi cha 11, utajifunza fasili ya kuvuja damu kwa wingi na hatua unazofaa kuchukua iwapo mwanamme anavuja damu baada ya kuzaa. Kipindi cha 11 pia kinaeleza hatua za kuingilia kati ambazo zinafaa kuchukuliwa katika awamu ya tatu ya leba na baada ya awamu hii ili kupunguza hatari ya Kuvuja Damu baada ya Kuzaa. Vidokezo vilivyo muhimu vimeandikwa kwa muhtasari hapa.

  • Ipapase uterasi (iwapo umehitimu kufanya hivyo) kwa kufinya kwa mikono miwili (Kipindi cha 11).
  • Mpe mama kipimo cha pili cha oxytocin 10IU kwa kumdunga ndani ya misuli au umpe kipimo cha pili cha misoprostol 400 µg. Mpe misoprostol kupitia kwenye rektamu. Zisukume kwa utaratibu tembe hizi ndani ya rektamu kupitia kinyeoni cha mwanamke huyu, au uziweke chini ya ulimi wake ili ziyeyuke.
  • Mhimize kuanza kunyonyesha punde baada ya kuzaa. Mikazo inayotoa maziwa hukazisha uterasi.

Usizidishe vipimo 1,000 µg za misoprostol (tembe 5). Iwapo mwanamke atatumia vipimo 600 µg (tembe 3) baada ya kuzaa na anavuja damu kwa wingi, usimpe zaidi ya 400 µg (tembe 2) kupitia rektamu Kipimo sahihi hakisababishi madhara. Iwapo hakutumia vipimo 600 µg vya misoprostol kupitia mdomoni baada ya kuzaa na anavuja damu kwa wingi, mpe vipimo 1,000 µg vya misoprostol kupitia rektamu kwa kipimo kimoja.

Iwapo oxytocin ilitumika mwanzoni, usimpe misoprostol zaidi.

Iwapo mwanamke huyu atavuja damu kwa wingi, mpeleke kwenye kituo cha afya mara moja. Kipindi cha 11 kitakufunza hatua za kuchukua wakati wa safari.

Iwapo damu haikomi kuvuja upesi baada ya kipimo cha pili cha misoprostol, mpendekezee rufaa ya dharura kwenda katika kituo cha afya kilicho karibu. Wakati mwingine, damu huvuja kutoka kwenye uke uliojeruhiwa, seviksi iliyojeruhiwa au uterasi iliyojeruhiwa. Kwa kawaida, damu hii huvuja kwa mchiririko wa polepole na usiokoma. Damu hii kwa kawaida huwa nyembamba na ya rangi nyekundu ng’avu. Hatua za kuchukua unaposubiri uchukuzi:

  • Mlaze mama huku miguu yake ikiwa imeinuka kuzidi kichwa, na kichwa chenyewe kikiegemea upande mmoja. Mpashe joto kwa kumfunika blanketi.
  • Ufunge vyema mpira wa kutilia viowevu kisha uanze kumtia kiowevu kwa kutumia kiowevu cha kawaida cha chumvi au Kiowevu cha Ringer. (Ulijifunza jinsi ya kuanza kuongeza kiowevu mwilini katika Kipindi cha 22 cha Moduli ya Utunzaji wa kabla ya kuzaa, na katika mafunzo yako ya kiutendaji.) Unaweza kufunzwa jinsi ya kuongeza kipimo kingine cha oxytocin katika viowevu vilivyo katika mfuko unaobebea mipira ya kuongeza viowevu mwilini. Hata hivyo, unaweza kumpa oxytocin iwapo tu unweza kuihifadhi ndani ya friji hadi utakapoihitaji.
  • Dumisha usafi kwenye vulva na msamba.
  • Ikwezekana, ambatana na mwanamke huyu hadi hospitalini.
  • Wahimize jamaa au rafiki zake kuandamana naye na kumtunza mtoto (na kuwatolea damu ikihitajika).

6.3.2 Plasenta iliyosalia

Plasenta iliyosalia ni wakati plasenta imesalia ndani ya uterasi kwa zaidi ya dakika 30 baada ya mtoto kuzaliwa. Iwapo plasenta itasalia ndani ya uterasi kwa zaidi ya dakika 30, fanya mambo yafuatayo:

  • Usijaribu kuivuta zaidi kambakitovu ukitaka kuitenganisha na plasenta.
  • Mtayarishe mwanamke huyu kusafirishwa hadi katika kituo cha afya kwa utunzaji wa dharura haraka iwezekanavyo. Fuata maagizo yaliyopeanwa katika kitengo kilichotangulia.

Muhtasari wa Kipindi cha 6 cha Somo

Katika Kipindi cha 6, ulijifunza yafuatayo:

  1. Udhibiti tendeti katika hatua ya tatu ya leba (UTATL) ndio njia bora zaidi ya kupunguza hatari ya Kuvunja damu baada ya Kuzaa kwa zaidi ya 60%. Kwa hivyo, tumia UTATL kwa kina mama wote wanaozaa.
  2. Mabadiliko mtawalia ya kifisiolojia yanayofanyika katika awamu ya tatu ya leba ni: kutengana kwa plasenta, kushuka kwa plasenta, kutolewa kwa plasenta na kudhibiti kuvuja kwa damu.
  3. Matatizo ya kawaida yanayoweza kutokea katika awamu ya tatu ya leba ni pamoja na plasenta iliyosalia, kuvuja damu baada ya kuzaa na kugeuka kwa uterasi.
  4. Njia ya UTATL ina vipengele vifuatavyo mtawalia: Chunguza kama kuna mtoto mwingine, mpe mama dawa za ndani ya uterasi zinazoikazisha, na utumie njia ya kuvuta kambakitovu taratibu. Ipapase uterasi baada ya kutolewa kwa plasenta, ichunguze plasenta kuona kama ni nzima, na uchunguze sehemu ya uke kutambua kama kuna majeraha na damu inayovuja kwa wakati huu.
  5. Oxytocin, ergometrine namisoprostol ni dawa za kukazisha uterasi zinazotumika mara nyingi. Ergometrine ni dawa yenye nguvu sana, hivyo haipendekezwi kutumiwa katika Huduma ya Afya Ugani. Ni sharti Oxytocin na ergometrine zihifadhiwe ndani ya friji hadi zitakapohitajika. Misoprostol huwa ni tembe.
  6. Tumia misoprostol au oxytocin kabla ya muda usiozidi dakika moja baada ya kuzaliwa kwa mtoto.
  7. Hakikisha kuwa uterasi imekazana ifaavya hadi kuwa ngumu. Uterasi inaonekana ikiwa imejichora juu ya fumbatio. Hauoni damu inayovuja, isipokuwa unaona miraruko au majeraha kwenye sehemu ya chini ya uke.
  8. Ikihitajika, andaa mpira wa kuongeza viowevu mwilini na ujitayarisha kupendekeza rufaa hadi katika kituo cha afya. Pendekeza rufaa iwapo utaona mojawapo ya dalili hizi: ndewe ya plasenta ambayo haipatikani, plasenta iliyosalia na uterasi nyororo, legevu na iliyopanuka. Pendekeza rufaa iwapo utatambua damu inayoendelea kuvuja hata baada ya kurudia utaratibu wa kumpa mama dawa ya ndani ya uterasi na kuipapasa uterasi.

Maswali ya Kujitathmini ya Kipindi cha 6

Kwa kuwa sasa umekamilisha kipindi hiki, jibu maswali yafuatayo ili kubaini jinsi ulivyojifunza. Unaweza kulinganisha majibu yako na uliyoandika kwenye Maswali ya Kujitathmini mwishoni mwa Moduli hii.

Swali la Kujitathmini 6.1 (linatathmini Malengo ya Somo la 6.1 na 6.2)

  • a.Fasili ya awamu ya tatu ya leba ni nini?
  • b.Ni mabadiliko gani ya kimwili yanayotokea katika awamu ya tatu ya leba ya kawaida isiyokuwa na matatizo?
Answer
  • a.Awamu ya tatu ya leba huanza kwa kuzaliwa kwa mtoto na kuisha kwa kutolewa kwa plasenta na membreni zilizoungana nayo.
  • b.Mabadiliko ya kimwili yafuatayo hutokea katika awamu ya tatu ya leba ya kawaida:
    • Plasenta inapobambuka kutoka pembezoni mwa uterasi, damu iliyo ndani ya vishipa vidogo kwenye mzizi wa plasenta huanza kugandia katikati mwa pembezoni mwa plasenta na miometriamu. (Miometriamu ni pembezo ya uterasi iliyoundwa kwa misuli.)
    • Plasenta hushukia chini ya njia ya uzazi hadi kupitia seviksi iliyopanuka. Baadaye, plasenta hutolewa.
    • Baada ya plasenta kutolewa, misuli ya uterasi hukazana. Misuli hii huifinya mishipa iliyopasuka ili kusitisha damu kuvuja baada ya kuzaa. Uterasi hugeuka kuwa ngumu na ya duara.

Mwisho wa jibu

Swali la Kujitathmini 6.2 (linatathmini Malengo ya Somo 6.1 na 6.3)

Alemitu ni Mhudumu wa Afya Ugani katika Kituo cha afya cha kijijini. Amemaliza kuzalisha katika kituo chake muda mfupi uliopita. Mama anayemhudumia yuko katika awamu ya tatu ya leba, na ameanza kunyonyesha. Alemitu amehitimu kutumia UTATL. Hatua 6 za UTATL, kwa kina, ni zipi?

Answer

Hatua 6 za UTATL ni kama ifuatavyo:

1: je, kuna mtoto wa pili?

2 Mpe mama dawa ya kukazisha uterasi ili kuiwezesha kukazana:

  • Tembe za misoprostol (mikrogramu) 600 μg zinazonywewa kwa maji.
  • Au umpe oxytocin 10 IU inayodungwa ndani ya misuli.
  • USIMPE ergometrine.

3 Itoe plasenta kwa kutumia njia ya kuvuta kitovu taratibu kwa msukumo pinzani (Kisanduku 6.3 kinaeleza kwa kina.)

4 Papasa uterasi

5 Ichunguze plasenta na membreni za fetasi kuhakikisha kuwa hakuna vipande vilivyosalia. Chunguza ndewe na sehemu ya juu ya mama. Tia mkono wako ndani ya membreni kuhakikisha kuwa membreni hizi ni nzima. Hakikisha kuwa hali ya kambakitovu ni ya kawaida.

6 Chunguza uke na sehemu ya nje ya uke wa mama ili kutambua kama kuna mchibuko au damu inayovuja.

Mwisho wa jibu

Swali la Kujitathmini 6.3 (linatathmini Malengo ya Somo 6.3)

Husika kwa Utendeti katika Kudhibiti Awamu ya Tatu ya Leba Ulitumia UTATL ifaavyo, lakini mwanamke huyu ameendelea kuvuja damu.

  • a.Je, utampa misoprostol zaidi? Kama ni hivyo, ni kipimo kipi cha dawa unachofaa kumpa, na dawa yenyewe inafaa kuwa katika aina gani?
  • b.Je, ni hatua ipi nyingine unayofaa kuchukua?
  • c.Unafaa kufanya nini iwapo mwanamke huyu ataendelea kuvuja damu?
Answer
  • a.Ndiyo, lakini usizidishe vipimo 1,000 µg za misoprostol kwa ujumla. Iwapo umeshampa vipimo 600 μg vya dawa, unaweza kumpa hadi vipimo 400 μg zaidi. Ili kumpa kipimo cha pili, zitie tembe hizi ndani ya rektamu ya mwanamke huyu.
  • b.Mama huyu ameshaanza kunyonyesha, hivyo ipapase uterasi yake kwa kusukuma kwa mikonno miwili ili kusisimua mikazo.
  • c.Iwapo damu haikomi kuvuja upesi baada ya kipimo cha pili cha misoprostol, mpendekezee rufaa ya dharura kwenda katika kituo cha afya kilicho karibu. Anza kumwongeza viowevu mwilini kabla ya kuondoka.

Mwisho wa jibu

Swali la Kujitathmini 6.4 (linatathmini Malengo ya Somo 6.6)

Je, dalili hatari zinazoashiria matatizo yanayoweza kutokea katika awamu ya tatu ya leba ni zipi?

Answer

Dalili hizi hatari ni ishara ya matatizo katika awamu ya tatu ya leba:

  • Plasenta iliyosalia au plasenta ambayo ni kipande kimoja tu kilichotolewa
  • Seviksi inayofungika kabla ya plasenta kutolewa
  • mikazo hafifu ya uterasi
  • Unapoipapasa uterasi, unatambua kuwa ni nyororo.
  • Awamu ya tatu ya leba inayodumu kwa dakika 30.
  • Kuchibuka kwa msamba, uke au seviksi
  • Kuvuja damu kwa wingi (kuvuja damu baada ya kuzaa)

Mwisho wa jibu