Leba iliyozuiliwa inaweza kukingwa. Moja wapo ya majukumu yako makuu kama mhudumu wa kuzalisha mwenye ujuzi ni kukinga leba iliyozuiliwa kwa wanawake katika jamii yako. Leba iliyozuiliwa hutokea zaidi katika maeneo ya vijiji vya Afrika, hasa miongoni mwa wanawake wanaokaa na leba nyumbani kwa muda mrefu.
Leba iliyozuiliwa inahusishwa na vifo wakati wa kuzaa na magonjwa. (Vifo wakati wa kuzaa ni vifo vya fetasi au mtoto mchanga. Ugojwa ni hali ya kuugua na ulemavu unaotokea wakati huo wa kuzaliwa. Leba iliyozuiliwa inachangia kati ya asilimia 10- 25 ya vifo vya kina mama Sahara ya Afrika. Kwa kweli, takwimu hii inayoshangaza ni kupuuza ya tatizo. Vifo vinavyosababishwa na leba iliyozuiliwa mara nyingi vinaainishwa chini ya matatizo mengine (kama vile sepsisi, kuvuja damu baada ya kuzaa, au uterasi iliyopasuka).
Katika Kipindi hiki, utajifunza kutambua dalili za kawaida za leba za muda mrefu na zilizozuiliwa. Utajifunza kutambua njia bora zaidi ya udhibitishaji. Udhibitishaji uliochelewa wa leba iliyozuiliwa mara nyingi husababisha nasuri kwa wanawake wanaoishi. Ikiwa fistula haitatibiwa, kina mama wanaweza kutengwa na jamii.
Baada ya Kipindi hiki cha, utaweza:
9.1 Kufafanua na kutumia kwa ufasaha maneno yote muhimu yaliyochapishwa kwa herufi nzito. (Maswali ya Kujitathmini 9.2 na 9.3)
9.2 Kuorodhesha visababishi vikuu vya leba iliyozuiliwa. Kuelezea jinsi kila hali inachangia kwa ukuwaji wa leba iliyozuiliwa. (Swali la Kujitathmini 9.1)
9.3 Kuelezea dalili za kawaida za leba iliyozuiliwa. Kuelezea matatizo ya kawaida kwa mama na fetasi yanayotokana na leba iliyozuiliwa. (Swali la Kujitathmini 9.3)
9.4 Kuelezea udhibitishaji wa leba iliyozuiliwa. Kuelezea njia za kukinga leba iliyozuiliwa. (Swali la Kujitathmini 9.3)
9.5 Kueleza jinsi mabadiliko ya kijamii katika jamii inaweza kupunguza nafasi ya kuwa na leba iliyozuiliwa inaweza kutokea (Swali la Kujitathmini 9.4)
Leba iliyozuiliwa ni kushindwa kwa fetasi kuteremka kupitia njia ya uzazi kwa sababu kizuizi kinazuia kuteremka. Leba iliyozuiliwa hutokea hata na mikazo mikali ya uterasi. Kwa kawaida uzuiliaji hutokea ukingoni mwa pelvisi. Inaweza kutokea katika tundu au mlangoni mwa pelvisi. Wakati leba inapokaa kwa muda mrefu kwa sababu ya kukosa kuendelea kukua, kuna hatari kubwa hivi kwamba ushukaji wa fetasi itazuiliwa. Leba iliyokaa kwa muda mrefu haina ufafanuzi mmoja. Inayobainishwa kama “muda mrefu” inatofautiana kulingana na hatua ya leba (Jedwali 9.1).
Jedwali 9.1 Ni wakati upi leba itasemekana kuwa imedumu muda mrefu katika hatua tofauti za leba?
Leba inaweza kuainishwa kuwa “iliyorefushwa” katika hatua yoyote. Hata hivyo, kumbuka kuwa leba iliyozuiliwa kawaida hutokea baada ya leba kuingia hatua ya pili.
Kwa kawaida, leba iliyozuiliwa hutokea katika hatua ya pili ya leba kwa wanawake ambao leba yao hurefushwa. Kwa nini leba huwa ya muda mrefu au iliyozuiliwa, hii inaweza kuwa ni sababu ya “nguvu”, “abiria”, na “njia”.
Jedwali 9.1 Inatoa muhtasari wa visababishi vya ukosefu wa “abiria” and “njia”.
Abiria | Njia |
Kichwa: ● Kichwa cha fetasi kikubwa (kikubwa kwa hicho fetasi) ● Hidrosefalasi (kukusanyika kwa maji ndani ya kichwa, inayosababisha uvimbe wa fuvu) Kitangulizi na mkao: ● Paji la uso, uso, bega ● Uendelefu wa kukaa vibaya kwa fetasi Mimba ya mapacha: ● Mapacha waliofungiana (kufungiana kwa shingo) ● Mapacha walioshikana (walioshikana na kutumia baadhi ya viungo pamoja) | Mifupa ya pelvisi: ● Upungufu (kwa sababu ya utapia mlo) ● Iliyoumbuka (kwa sababu ya jeraha au polio) Tishu nyororo: ● Uvimbe kwenye pelvisi ● Maambukizi ya virusi kwenye uterasi au fumbatio ● Kovu (kutokana na ukeketaji) |
Vizuizi vinavyosababisha leba ya muda mrefu na leba iliyozuiliwa katika jedwali 9.1 vinaweza kuwekwa kwa vikundi: kichwa kisicholingana na pelvisi; kitangulizi na mtoto kukaa vibaya; au fetasi ambaye si wa kawaida au mama ambaye analeba iliyozuiliwa kwa njia ya uzazi. Kila aina imeelezwa kwa undani.
Kutolingana kinakueleza kwamba ukubwa wa kichwa cha fetasi ni tofauti na ukubwa wa ukingo wa pelvisi ya mama.
Kutolingana kwa kichwa na pelvisi inamaanisha kuwa fetasi haiwezi kupita kwa usalama pelvisi ya mama. Aidha pelvisi ni nyembamba sana kwa kichwa cha fetasi au kichwa ni kubwa mno ukilinganisha na pelvisi. (Mchoro 9.1) Kumbuka anatomi ya pelvisi ya wajawazito na fuvu ya fetasi ambayo ulijifunza katika Kipindi cha 6 cha Somo la Moduli ya Huduma ya wajawazito). Wanawake katika nchi zinazoendelea wanaweza kuwa na pelvisi ndogo au imepunguka. Hali hii inasababishwa na utapia mlo utotoni unaoendelea hadi kufikia utu uzima. Kutolingana kwa kichwa na pelvisi kwa kawaida haiwezi kutambulika kabla wiki ya 37 ya ujauzito. Kabla ya wakati huo, kichwa cha mtoto hakijapata ukubwa wa kuzaliwa.
Ukaaji wa kitangulizi au kukaa vibaya ni sababu zingine kuu za leba iliyozuiliwa.
Je, unaweza kutofautisha kati ya maneno haya mawili na kukumbuka baadhi ya vitangulizi vya fetasi visivyokuwa vya kawaida na kutokuwa katika mkao wa kawaida katika uterasi kutoka Kipindi cha 8 cha Somo?
Kitangulizi kisicho cha kawaida ni kitangulizi chochote bali sio kipeo, ambayo ni wakati fuvu la kichwa cha mtoto hutangulia kwanza. Kawaida vitangulizi visivyokuwa vya kawaida huwa makalio na bega itakapotoka “bega kwanza”. (Kitanguliza cha makalio ni wakati makalio ya mtoto na/au miguu hutoka kwanza.) Mkao mbaya in wakati mtoto huwa “kichwa chake kiko chini” (kichwa ndio–kitangulizi) lakini kipeo kiko pahali hapafai ikilinganishwa na pelvisi ya mama. Aina mbili za kawaida zaidi za mkao wa fetasi usiofaa husababisha utangulishi wa uso na paji la uso.
Mwisho wa jibu
Pia ulijifunza kuhusu kupata mimba nyingi katika Kipindi cha 8 cha Somo. Leba inaweza kuzuiliwa na mapacha waliofungiana au mapacha walioshikana. Mapacha waliofungiana ni watoto wawili “waliofungana” pamoja kwa shingo wakati pacha wa kwanza akiwa katika kutanguliza tako na wa pili yuko katika kutanguliza kichwa mwanzo. Mapacha walioshikana huwa wameungana kwa kifua, kichwa, au eneo lingine lolote lile.
Baadhi ya ulemavu wa fetasi usiokuwa wa kawaida husababishwa na fetasi ambaye ana kichwa mkubwa ambayo usiokuwa wa kawaida. Mfano mmoja ni hidrosefalasi, ambayo inasababishwa na viowevu kukusanyika katika ubongo wa mtoto.
Leba iliyozuiliwa inaweza kusababishwa na njia ya uzazi ya mama isiyokuwa ya kawaida. Mama anaweza kuwa na tyuma (ukuwaji au uvimbe wa tishu) katika kaviti ya pelvisi. Au mama anaweza kuwa na kovu katika njia ya uzazi sababu ya njia kali ya ukeketaji. Au anaweza kuwa na msamba ambayo imebana, usio panuka ili kupitisha mtoto. (Msamba ni ngozi iliyo katikati ya ufa wa uke na mkundu.)
Ukeketaji ndio lengo la Kipindi cha 5 Somo katika moduli ya Balehe na afya ya uzazi ya vijana.
Ishara ya uhakika wa leba iliyozuiliwa ni wakati kipenyo pana ya fuvu ya fetasi hubaki bila kusonga juu ya ukingo wa pelvisi sababu haiwezi kushuka. Ili kutambua kizuizi hiki, papasa fumbatio ya mama kwa makini kama uterasi inatulia na kuwa nyororo kati ya mikazo. Hata hivyo, uterasi inaweza kuwa na mikazo toni (inaendelea kuwa ngumu) na inakaa na inafinyilia fetasi. Ni vigumu kuhisi kama fetasi inateremka kwa njia ya uzazi. Kupapasa uterasi pia inamfanya mama kuhisi maumivu makali. Katika hali hii, tegemea dalili zingine kwa utambuzi wako.
Kuna uwezekano zaidi ya leba iliyozuiliwa kutokea iwapo taarifa hizi ni za kweli:
Tathmini mwanamke aliye na historia hii ya leba kwa kupima uke wake. Yoyote kati ya dalili hizi inaonyesha kuwa kuna leba iliyozuiliwa:
Bandl’s ring ni jina linalopewa mbonyeo katikati ya uterasi ya juu na chini, karibu na kitovu. Haufai kuona au kuhisi Bandl's ring ukipima fumbatio ya mama katika leba ya kawaida (Mchoro 9.2a). Unapoona au kuhisi Bandl's ring (Mchoro 9.2b), ni ishara ya mwisho ya leba iliyozuiliwa. Juu ya mbonyeo hiuu kuna sehemu ya juu ya uterasi ambayo ni nene mno. Sehemu hii ya juu imevutwa kwa upande wa juu (kurudi ndani) kuelekea kwenye mbavu za mama. Chini ya Bandi's ring ni uvimbe (uliofura), mkonde hatari, sehemu ya chini ya uterasi. Sehemu ya chini ya fumbatio inaweza zaidi kuvimbishwa na kibovu kilichojaa na gesi ndani ya matumbo.
Kumbuka kutoka Kipindi 4 cha Somo kwamba patografu ni chombo muhimu cha kutambua leba usiokuwa wa kawaida au ya muda mrefu. Leba iliyozuiliwa inaonyeshwa na rekodi ya patografu ya kiwango cha utanuzi wa seviksi na kiwango cha kuteremka kwa kichwa cha fetasi. (Kumbuka kwamba seviksi inapaswa kutanuka angalau sentimita 1 kwa saa) Mchoro 9.3 (a) kinaonyesha rekodi ya patoghraph ya kawaida na utanuzi unaoendelea kuteremka kwa kichwa cha fetasi. Hata hivyo katika Mchoro 9.3 (b) unaweza kuona ushahidi wa leba ya muda mrefu katika hatua ya leba ya kwanza au ya pili. Kipimo cha utanuzi wa seviksi kimepita “Mstari wa Tahadhari”. Iwapo hatua haitachukuliwa, itapita mstari wa Hatua. Licha ya mikazo mikali ya uterasi, kichwa cha fetasi haki shuki.
Rekodi ya utanuzi wa seviksi kwenye patografu haipaswi kupita mstari wa Tahadhari na/au wa Hatua. Iwapo aidha ya mstari itapitwa, leba hii ni ya muda mrefu na pengine iliyozuiliwa. Fanya rufaa wa haraka.
Katika Mchoro 9.3 (b), ni masaa ngapi baada ya kuanza kurekodi patografu ndipo maendeleo ya utanuzi wa seviksi ulipokoma?
Seviksi ilikoma kutanuka masaa 4 baada ya kuanza kurekodi patografu.
Mwisho wa jibu
Katika patografu inayoonyeshwa katika Mchoro 9.3(b), ni saa ngapi imepita tangu kuwe na ishara yoyote ya utanuzi wa seviksi?
Patografu inaonyesha kwamba kipenyo cha seviksi hakijaongezeka kwa masaa mawili na nusu yaliyopita.
Mwisho wa jibu
Iwapo rekondi ya utanuzi wa servikisi imefika mstari wa Tahadhari kwa patografu, jaribu kuondoa kizuizi kabla haijafikia mstari wa hatua. Ulijifunza taratibu hizi katika Moduli ya huduma za ujauzito (Kipindi cha 22 cha Somo) na ujuzi wako kwa mafunzo ya vitendo. Zimeelezewa hapa kwa ufupi:
Mpeleke mama haraka kwa kituo cha afya ambapo huduma ya upasuaji inapatikana (Mchoro 9.4). Anaweza kuhitaji uzalishaji wa dharura kwa operesheni ya upasuaji ilikutoa mtoto akiwa hai na kuokoa maisha yake. (Operesheni ya siza ni wakati fumbatio yake na uterasi hufunguliwa kwa kukatwa ili kutoa mtoto.)
Matatizo ya uterasi iliyozuiliwa kwa mama na fetasi au mtoto mchanga yanaweza kuwa hatari sana. Kumbuka kwamba vizuizi vya uterasi hutokea hasa kwa sababu ya leba ya muda mrefu nyumbani ambayo haijafuatiliwa vizuri na rufaa haikupeanwa kwa haraka. Matatizo ya kawaida zaidi ambayo huathiri mama ni ukuaji wa fistula.
Fistula ni ufunguzi usiokuwa wa kawaida (kwa kawaida hutokea kwa sababu ya tishu kukatika) kati ya:
Fistula inapitisha mkojo au kinyesi ndani ya uke na kisha hutokea kwa njia isiyozuilika. Mwanamke aliye na fistula anaweza kutoa mkojo au kinyesi wakati anapotembea au kufanya shughuli yoyote ya kila siku. Uchafu huu uchafua nguo zake na huleta harufu mbaya (Mchoro 9.5). Kwa sababu ya athari hizi, mume wake na familia wanaweza kumshutumu au kumtenga. Unaweza kufikiria kuendelea kuvuja kwa mkojo au kinyesi ina maana gani kwa mtu binafsi. Matokeo mengine ya fistula ni pamoja na mfadhaiko kila mara, magonjwa ya mwili na maambukizi ya njia ya uzazi, kibofu na figo. Wakati mwingine mwanamke hujiua.
Leba iliyozuiliwa husababisha karibu 20% ya kesi zote za ukuaji wa fistula (Mchoro 9.6).
Katika hali chache, mambo haya yanaweza kusababisha fistula:
Ikiwa leba iliyozuliwa haitadhibitiwa vizuri, inaweza kusababisha matatizo haya mengine kwa mama:
Leba iliyozuiliwa inaweza kusababisha matatizo haya kwa mtoto mchanga:
Unaweza kujifunza kuhusu matatizo yanayowaathiri watoto wachanga katika Moduli ya Utunzaaji baada ya kuzaa na Moduli ya Huduma Sawa kwa watoto wachanga na Magonjwa ya watoto
Mkunga mwenye ujuzi anaweza kufanya mambo kadhaa ili kuzuia leba ya muda mrefu. Zaidi ya hayo, baadhi ya mabadiliko ya kitamaduni huleta tofauti kubwa kwa hali zinazoongezea hatari ya leba iliyozuliwa. Sasa tuangalie kwa kifupi hali hizi.
Leba iliyozuliwa ni sababu kubwa ya vifo vya kina mama kote duniani na hasa katika nchi zinazoendelea barani Afrika. Hatua muhimu zaidi inayoweza kuzuia vifo hivi na ulemavu ni kuwa na huduma ya mkunga mwenye ujuzi wakati wa kuzaa. Jukumu lako muhimu kama mfanyakazi wa afya vijijini ni kuwafundisha watu katika jamii yako umuhimu wa kupata huduma yenye bora wakati wa kuzaa kila wakati. Hamasisha wanawake kuja kwenu kwa ushauri. Dumisha uhusiano wa karibu na vituo vya afya au hospitali (kama ipo) katika eneo lako. Unahitaji rufaa kwa haraka na inayofaa wakati wa hali za dharura.
Chombo bora zaidi kwa utambuzi wa leba ya muda mrefu ni kuandika hatua za leba kwenye patografu. Wakati huo huo, mara kwa mara tathmini hali ya fetasi na ya mama (Kipindi cha 4). Rekodi iliyo kwa patografu inakupa onyo mapema kuwa leba inaweza kuwa ya muda mrefu kwa hakika ambapo uwezekano wa uzuizi wa uterasi inaonekana kuwa na rufaa ni muhimu. Daima tumia patografu wakati unapotoa huduma ya kuzaa.
Ni mambo gani mawili lazima uyafanye kuzuia mwanamke ambaye yuko katika leba kupata fistula?
Fanya mambo haya mawili:
Mwisho wa jibu
Kama ulivyojifunza katika Moduli ya huduma za ujauzito (Kipindi cha 13), maandalizi ya kuzaa na kuwa tayari kwa matatizo ni muhimu kwa ajili ya leba na kuzaa kwa usalama. Hivyo saidia jamii yako kujipanga katika vikundi vya maandalizi ya kuzaa. Vikundi hivi lazima viwe na uongozi, elimu, fedha, na namna ya usafiri. Iwapo hali ya dharura kama vile leba iliyozuiliwa inatokea, vikundi hivi lazima vipeleke mama kwenye kituo cha afya kilicho karibu.
Ni muhimu kuwaelezea hali zinazoongeza hatari za leba iliyozuiliwa. Sababu kuu ya leba iliyozuiliwa ni pelvisi iliyo ndogo. Mara nyingi, pelvisi ndogo ni matokeo ya lishe duni katika utotoni inayoendelea katika utu uzima. Boresha lishe utotoni kwa njia ya elimu ya afya, hasa kwa wasichana. Lishe bora kwa wasichana hupunguza hatari ya leba ya muda mrefu na leba iliyozuliwa katika maisha ya baadaye.
Ndoa ya mapema ndio suala la Kipindi cha somo katika Moduli juu ya Vijana Waliobaleghe na Afya ya Uzaaji wa Vijana.
Suala lingine ni ndoa ya mapema. Utafiti katika Sahara ya Afrika imeonyesha kuwa 50% ya wanawake, hasa wale wa vijijini, huolewa katika wastani ya miaka karibu 16. Wengi wa wanawake wadogo hupata mimba haraka. Kikuundi hiki cha kina mama wadogo sana kiko katika hatari hasa ya leba iliyozuiliwa. Pelvisi ya mama wa umri mdogo haijakomaa vilivyo ili kutoshea kichwa cha mtoto. Katika mazungumzo yako na wanawake, wenzio, na viongozi wa jamii, sisitiza hatari za ndoa ya mapema. Jaribu kuwashawishi kuchelewesha kuzaa mtoto wa kwanza mpaka baada ya mwanamke kufikia miaka 18. Kuza njia za kupanga uzazi ili kuchelewesha mimba ya kwanza miongoni mwa wanawake hawa wadogo sana. Ikiwa mimba isiyotarajiwa itatokea, ni muhimu pia kuwashauri kuhusu huduma salama ya utoaji wa mimba (Moduli ya Utunjazi katika Ujauzito, Sehemu ya 2, Kipindi cha 20).
Katika Kipindi cha 9, umejifunza mambo haya:
Sasa kwa kuwa umekamilisha Kipindi hiki cha somo, jibu maswali haya ilikutathmini uliyojifunza. Linganisha majibu yako na Vidokezo juu ya maswali ya kujitathmini mwishoni wa moduli hii.
Andika maana ya hali tatu na jinsi zinasababisha leba iliyozuiliwa.
Hizi hali tatu (nguvu, msafiri, na njia) ni njia fupi ya kuelezea sababu kuu za leba iliyozuiliwa. Baada ya kukagua majibu yako ukilinganisha na haya, soma sehemu ya 9.2 tena ili kupata mengi zaidi kuhusu sababu hizi.
Mwisho wa jibu
Andika maana ya maneno haya:
Mwisho wa jibu
Soma Uchunguzi Kifani 9.1 kisha ujibu maswali ambayo yanayofuatia.
Tadelech anaishi MekitWoreda. Safari kutoka kijijini hadi mjini inaweza kuchukua siku nyingi, na anaishi mbali na hata kituo ndogo cha afya. Tadelech ana umri wa miaka 25 na tayari amezaa watoto wawili salama kijiji. Ujauzito huu wake ni wa tatu. Mikazo ilianza katika wiki ya 40 ya ujauzito. Baada ya siku mbili za leba, Tadelech anabebwa kwenye machela hadi kwa kituo chako ndogo cha afya. Wakati unamchunguza Tadelech, unapata uvimbembili juu ya fumbatio na mbonyeo kati yao karibu na kitovu (kifungo kwa fumbatio). Pia unapata kuwa kichwa cha mtoto hakijaingia kwenye pelvisi. (Iko tu juu ya ukingo wa pelvisi). Uchunguzi wa uke, unakadiria kuwa seviksi ya Tadelech ina upanuzi wa sentimeta 8 na kituo cha kichwa cha fetasi ni -3. Uke wa Tadelech una moto na mkavu na ana edema kwa valva.
Kichwa cha mtoto kiko katika -3, haijaingia kwa pelvisi, na inabakia juu ya ukingo wa pelvisi. Hali hii inaonyesha kwamba hakishuki inavyotarajiwa kwa sababu Tadelech amekuwa kwa leba kwa siku mbili.
Uke una moto na mkavu na edema ya valva ni ishara zaidi ya uwezekano wa iliyozuiliwa. (Edema ni uvimbe kutokana na ukusanyikaji wa maji katika tishu.)
Mwisho wa jibu
Jinsi gani unavyoweza kupunguza hatari ya leba ya muda mrefu na iliyozuliwa kwa wanawake ambao wanazalia nyumbani?
Ili kupunguza hatari za leba iliyozuiliwa, fanya haya:
Mwisho wa jibu