Kuraruka kwa uterasi hutokea uterasi inaporaruka au kupasuka kutokana na shinikizo litokanalo na leba iliyozuilika. Urarukaji wa uterasi hutokea sana katika nchi zinazoendelea barani Afrika. Barani Afrika, asilimia 94 ya uzazi hufanyika nyumbani na bila kushughulikiwa na mtaalamu wa afya mwenye ujuzi. Leba ikikamilika kwa kuraruka kwa uterasi, mwanamke huyo anaweza kufariki. Ikiwa mwanamke huyo ataongoka, anaweza kumpoteza mtoto au uterasi yake.
Takribani visa vyote vya urarukaji wa uterasi hutokea kwa wanawake waliozaa zaidi ya mara moja hapo awali ambao wamezaa angalau mara moja baada ya ujauzito wao kutimiza umri wa majuma 28. Urarukaji wa uterasi unaweza pia kutokea kwa wanawake walio na kovu kwenye uterasi. Uterasi huraruka tishu ya kovu hili inapofunguka. Hata hivyo, katika nchi zinazostawi, karibu visa vyote vya urarukaji wa uterasi hutokea kwa wanawake wasio na kovu kwenye uterasi ambao leba yao ilizuilika palipokosa utatuzi. Katika kipindi hiki, utasoma kuhusu mambo ya hatari na ishara za kitabibu za uterasi iliyoraruka. Utasoma kuhusu athari kwa mama na mtoto. Utasoma pia jinsi ya kuanza utatuzi unaoweza kuokoa mama na mtoto wake.
Baada ya kipindi hiki, utaweza:
10.1 Kufasili na kutumia kwa usahihi maneno yote muhimu yaliyo kwenye herufi nzito. (Maswali ya kujitathmini 10.1 na 10.2)
10.2 Kueleza mambo yanayoongeza hatari ya urarukaji wa uterasi. Kufafanua ni kwa nini wanawake waliozaa zaidi ya mara moja wamo katika hatari kubwa zaidi kuliko wale wanaozaa kwa mara ya kwanza. (Swali la kujitathmini 10.2)
10.3 Kueleza ishara za hatari na ishara za kitabibu za urarukaji wa uterasi. Kueleza matatizo yanayotokea sana kutokana na urarukaji wa uterasi. (Maswali ya kujitathmini 10.3 na 10.4)
10.4 Kufafanua jinsi ya kufanya utatuzi kwa wanawake wanaoraruka uterasi ili kuokoa maisha yao. Kueleza hatua utakazochukua ili kupunguza hatari ya urarukaji wa uterasi katika leba. (Swali la kujitathmini 10.4)
Ikiwa uzazi umezuilika huku uterasi ikiendelea kunywea, inaweza kuraruka. Tayari unajua kuhusu matatizo ya leba na kuzaa kutoka kwa Vipindi vya 8 na 9. Unapaswa uweze kujibu swali hili.
Je, ni mambo yapi yanayoongeza hatari ya urarukaji wa uterasi?
Ikiwa leba imezuilika kutokana na visababishi hivi, uterasi inaweza kuraruka:
Mwisho wa jibu
Visababishi vinne vya kwanza vimeshajadiliwa kwa kina katika vipindi vya hapo awali. Kipindi hiki kinaeleza kutokea kwa kovu kwenye uterasi na visababishi vingine vya urarukaji wa uterasi.
Mwanamke aliyefanyiwa upasuaji kwenye uterasi ana tishu ya kovu mahali ambapo ukuta wa uterasi umepona. Kwa mfano, upasuaji kwa ajili ya kuzaa mtoto au kutoa tyuma kwenye uterasi huacha tishu ya kovu. Tishu ya kovu si nyumbufu kikamilifu kama sehemu ya ukuta wa uterasi isiyo na kovu. Tishu ya kovu haiwezi kutanuka kulingana na minyweo ya leba. Leba ikizuilika kwa muda mrefu, minyweo ya misuli kwenye ukuta wa uterasi inaweza kusababisha kuraruka kwa tishu ya kovu. Uterasi inaweza pia kuwa na kovu ikiwa ilitobolewa katika utoaji wa mimba hapo awali.
Seviksi inaweza kuwa na jeraha kutoka katika uzazi wa awali. Kwa mfano, labda fosepsi zilitumika kusaidia katika uzazi wa mtoto ambaye hakuendelea kutoka baada ya kichwa kujichomoza kwenye vulva. Au uharibifu wa seviksi unaweza kutokea ikiwa vyombo vya upasuaji viliingizwa ndani ya uterasi kupitia ukeni. Wakati mwingine vyombo hutumiwa kudhibiti kutoka kwa damu baada ya kuzaa au kutibu tatizo kwenye uterasi. Matatizo kama haya yanaweza kuwa inflamesheni kwenye bitana ya uterasi. Katika hali hizi, seviksi iliyojeruhiwa hupata tishu ya kovu inayoweza kupasuka na kufunguka katika leba iliyozuilika.
Je, unakumbuka majina ya rusu ya misuli kwenye uterasi na bitana ya ndani ya uterasi kutoka katika Moduli ya Utunzaji katika Ujauzito? (Bitana ya ndani ni ambapo plasenta hukua.)
Rusu hiyo ya misuli huitwa miometriamu nayo bitana ya ndani ni endometriamu.
Mwisho wa jibu
Ulisoma kuhusu fistula katika Kipindi cha 9. Fistula ni mojawapo ya matatizo makali ya leba iliyozuiliwa. Fistula imeenea sana katika maeneo ya mashambani barani Afrika. Wakati mwingine, mwanamke hupata fistula katika leba ya hapo awali na kisha ikarabatiwe kwa njia ya upasuaji. Fistula inapopona, kovu kubwa zinaweza kutokea na kuzuia kuzaliwa kwa mtoto atakayefuata.
Je, ni sehemu ipi ya njia ya uzazi inayopata kovu kutokana na ukarabati wa fistula?
Uke. Fistula ni mwanya unaopasuka katikati ya uke na labda kibofu cha mkojo, rektamu, urethra, au ureta.
Mwisho wa jibu
Washauri kwa dhati wanawake walio na kovu kwenye uterasi, seviksi, au uke kuzaa mtoto wao atakayefuata katika kituo cha afya. Mwanamke huyu anaweza kuhitaji damu na vyombo vya upasuaji, pamoja na ujuzi wa kufanya upasuaji wa kuzaa.
Mwanamke aliyezaa mara mbili au zaidi amezaa angalau mtoto mmoja baada ya majuma 28 ya ujauzito. Umri wa ujauzito ni muhimu. Baada ya majuma 28, fetasi hutimiza ukubwa na uzani halisi. Uterasi ya mwanamke huyu tayari imetanuka. Kuzaa kunatarajiwa kuwa rahisi katika ujauzito utakaofuata. Licha ya ukweli huu, ikiwa leba zao zitazuilika, wanawake waliozaa mara mbili au zaidi wana uwezekano mkubwa wa kukumbwa na urarukaji wa uterasi kuliko wale wanaozaa mara ya kwanza.
Je, unaweza kupendekeza sababu ya tokeo hili lisilotarajiwa?
Sababu moja ni kuwa kina mama wa mara ya kwanza hawana historia ya hapo awali ya matatizo ya ujauzito. Mwanamke aliyezaa mara mbili au zaidi anaweza kuwa na kovu kwenye uterasi au sehemu zingine za njia ya uzazi. Kovu hizi ni visababishi vya hatari ya urarukaji wa uterasi.
Mwisho wa jibu
Sababu nyingine ya wanawake waliozaa mara mbili au zaidi walio na leba iliyokaa kwa muda mrefu au iliyozuilika kuwa katika hatari zaidi ya urarukaji wa uterasi ni kuwa wana minyweo mikali ya leba kwa muda mrefu zaidi kuliko wale wanaozaa kwa mara ya kwanza.
Kwa wanawake wanaozaa kwa mara ya kwanza, minyweo ya uterasi huwa mikali kwa takribani saa 24 za kwanza za leba. Baada ya saa 24, minyweo hii hufifia kwa ukali na kuwa mifupi. Baada ya takribani saa 36, uterasi imeishiwa nguvu. Wanawake hawa wanaozaa kwa mara ya kwanza hupata inesha ya uterasi. Ukali wa minyweo hii hufifia kabisa. Minyweo hii hudumu kwa muda mfupi na kutenganishwa na muda mrefu baina ya mnyweo mmoja na mwingine. Kwa kina mama hawa wa mara ya kwanza, minyweo ya uterasi imekaribia kuisha na kwa hivyo urarukaji wa uterasi ni nadra. Kwa upande mwingine, minyweo ya uterasi kwa wanawake waliozaa zaidi ya mara moja hubaki mikali, thabiti na ya mara kwa mara kwa muda mrefu zaidi. Wanawake waliozaa zaidi ya mara moja wanapokuwa katika leba, kuna uwezekano mkubwa wa kuraruka kwa uterasi.
Wanawake wanaozaa kwa mara ya kwanza hukumbwa na matatizo mengine makali. Inesha ya uterasi humaanisha kusalia kwa kichwa cha fetasi kwenye pelvisi ya mama kwa muda mrefu. Hatari ya hipoksia ya fetasi huongezeka, ambayo ni uhaba wa oksijeni kwa fetasi. Hatari ya kutokea kwa fistula huongezeka, ambayo husababisha ubakizaji wa mkojo na maambukizi kwenye kibofu cha mama kilichozuilika.
Katika sehemu fulani za Afrika, usingaji wa fumbatio katika leba ni tendo la kawaida la kijamii. Usingaji wa fumbatio hufanywa sana leba inapokaa kwa muda mrefu. Wakunga au wanawake wa kijiji hutumia siagi na mafuta ya kulainisha kusugua fumbatio. Wao huminya fandasi ya uterasi ili kujaribu kumsukuma mtoto upande wa chini. Kitendo hiki cha kijamii ni cha kudhuru sana. Usingaji wa fumbatio unaweza kusababisha urarukaji wa uterasi hasa kwa wanawake waliozaa zaidi ya mara moja.
Ili kudhibiti kipindi cha tatu cha leba, unaweza kutumia dawa ya toni ya uterasi, ambayo huifanya uterasi kunywea. (Dawa hizi ni misoprostol, oxytocin au ergometrine. Zote zimeelezewa kwa kina katika Kipindi cha 6.) Kabla ya kupeana dawa ya toni ya uterasi, hakikisha kuwa uterasi haina fetasi nyingine. Ukimpa dawa ya toni ya uerasi kukiwa na fetasi ndani ya uterasi, uterasi hii inaweza kuraruka na mtoto kupata asfiksia.
Je, kwa nini kina mama waliozaa zaidi ya mara moja wamo katika hatari zaidi ya kuraruka kwa uterasi kuliko wenzao wanaozaa mara ya kwanza?
Kovu kwenye uterasi ni kisababishi kikuu cha hatari kwa urarukaji wa uterasi. Tishu ya kovu si nyumbufu sana na inaweza kuraruka minyweo inapotokea. Mwanamke aliyezaa zaidi ya mara moja anaweza kuwa na kovu kutokana na upasuaji wa kuzaa au uzazi wenye matatizo ulioijeruhi njia ya uzazi. Uterasi yake pia hunywea kwa muda mrefu. Mwanamke huyu hapati inesha ya uterasi hata ikiwa leba imezuilika.
Mwisho wa jibu
Urarukaji wa uterasi unaweza kuzuilika ikiwa leba iliyokaa sana itadhibitiwa vyema na hatua ifaayo kuchukuliwa kabla ya uterasi kuraruka.
Jedwali 10.1 linaonyesha ishara za hatari zinazotokea sana uterasi inapoelekea kuraruka. Ishara hizi ndivyo viashiria bora zaidi kuwa leba imezuilika na kuwa uterasi inaweza kuraruka karibuni. Urarukaji unaweza kutokea ila mtoto azaliwe haraka kwa njia ya upasuaji.
Je, patografu inawezaje kukusaidia kujua kuwa uterasi inaelekea kuraruka?
Tumia patografu kuchora idadi ya marudio na muda ambao minyweo itadumu. Chora mabadiliko kwa kiwango cha mpigo wa moyo wa fetasi. Kwa hivyo utagundua haraka ikiwa mojawapo ya idadi hizo zipo katika eneo la hatari lililoonyeshwa katika Jedwali 10.1.
Mwisho wa jibu
Ishara ya kwanza kuwa uterasi imeraruka ni kukoma kabisa kwa minyweo ya uterasi. Dalili zingine hufuata haraka.
Maumivu haya huhisika unapoligusa fumbatio. Fumbatio lina maumivu kwa sababu ya kuraruka kwa uterasi na kero lisababishwalo na damu inayojikusanya kwenye kaviti ya fumbatio. Fumbatio linaonekana kuwa lililofura kwa sababu uterasi imejifunga kwa mwili wa fetasi na damu kumwagika ndani ya kaviti ya fumbatio. Kusonga kwa utumbo kumepungua au kumekoma, na kwa hivyo huwezi kusikia sauti za kusonga kwa utumbo kwa stethoskopu. (Kusonga kulikopungua au kulikokoma kwa utumbo huitwa enteroflejia.) Kibofu pia kinaweza kuzuilika, hali inayochangia kufura na maumivu. Muda unaposonga, maambukizi yanaweza kukua kwenye fumbatio na kusababisha kufura zaidi.
Fetasi haiwezi kuishi kwa muda mrefu ndani ya uterasi iliyoraruka. Kwanza, uterasi hujifunga kwa mkazo kwenye mwili wa fetasi. Kisha sehemu fulani za fetasi zinaweza kupita kwenye mikato. Au fetasi nzima iweze kupita hadi kwenye kaviti ya fumbatio. Ukitomasa fumbatio, ni ukuta wa fumbatio tu ulio katikati ya mkono wako na fetasi. Kwa hivyo, unaweza kuhisi sehemu za fetasi kwa urahisi. Ikiwa mtoto amefariki, mama hawezi kumhisi akisonga na huwezi kusikia mpigo wa moyo wake.
Athari za kuraruka kwa uterasi kwa mama hutegemea mambo matatu. Mambo haya ni kiasi cha damu iliyopotea, muda uliopita baada ya mraruko kutokea, na ikiwa kaviti ya fumbatio na mfumo wake wa mzunguko wa damu vimeambukizwa.
Kuraruka kwa uterasi ni kero linalorarua misuli ya uterasi na mishipa ya damu. Ikiwa mraruko huo utahusisha mishipa mikuu ya damu, hasa ateri za uterasi, damu inayopotea ni nyingi sana. Pasipofanyika utatuzi wa dharura haraka, upotezaji huo wa damu unaweza kusababisha kufariki kwa fetasi. Mama naye atakumbwa na mshtuko kutokana na upotezaji wa damu na kisha afariki. Mraruko ukitokea katika eneo la uterasi ambapo mishipa mikuu ya damu haijahusishwa, mwanamke ana nafasi kubwa ya kuongoka.
Wakati mwingine, wanawake hawatokwi na damu sana wala kuwa na hali inayohatarisha maisha. Wanawake hawa hubaki nyumbani kwa saa na hata siku kadhaa baada ya uterasi kuraruka. Hata hivyo, jinsi mwanamke anavyokawia kutibiwa kwa ajili ya uterasi iliyoraruka, ndivyo kiwango cha kupoteza damu , kutofanya kazi kwa figo na maambukizi yanayoenea mwilini mwake yanavyoendelea kuongezeka.
Uterasi iliyoraruka hutoa mwingiliano wa moja kwa moja kati ya njia ya uzazi na kaviti ya fumbatio. Viungo vingine vya ndani vinaweza kujeruhiwa na kuvuja ndani ya fumbatio. (Sehemu za matumbo, rektamu na kibofu zinaweza kujeruhiwa.) Kutokana na haya, viini huenea kwa urahisi kwenye kaviti ya fumbatio. Viini hivi huingia kwenye mzunguko wa damu kupitia kwenye mishipa ya damu iliyoraruka. Ukuaji wa maambukizi kwenye kaviti ya fumbatio huitwa peritonitisi. Maambukizi yanayosambazwa mwilini kwenye mzunguko wa damu huitwa septisemia. Wakati mwingine, mwanamke hustahimili mraruko wa kwanza, bali hatibiwi kwa zaidi ya saa 6. Hatari ya kutokea kwa moja au matatizo haya yote yapo juu sana. Kwa hivyo, unafaa kutambua mapema kuwa mraruko umetokea. Ni lazima umpe mwanamke huyu rufaa haraka. Hatua hizi mbili ni muhimu sana kwa kuokoa maisha ya mama huyo.
Matatizo yanategemea kiasi cha damu iliyopotea, muda uliopita baada ya uterasi kuraruka na hali ya maambukizi yoyote yale. Mwanamke aliye na uterasi iliyoraruka anaweza kukumbwa na baadhi au matatizo haya yote.
Mshtuko utokanao na upotezaji wa damu unaua kwa haraka sana. Mama huwa anahisi dalili hizi:
Mshtuko wa sepsisi hutokea iwapo mraruko au kutokwa na damu kumesababisha septisemia. Ishara zinafanana na zile za mshtuko utokanao na upotezaji wa damu, bali pamoja na kiwango cha juu sana cha joto mwilini (zaidi ya sentigredi 38).
Je, ni nini kinachofanyika kwa fetasi uterasi inapoelekea kuraruka na punde baada ya kuraruka?
Kabla ya mraruko, kiwango cha mpigo wa moyo kiko zaidi ya mipigo 160 kwa dakika au chini ya mipigo 120 kwa dakika. Baada ya mraruko, uterasi hujifunga kwenye mwili wa fetasi. Damu humiminika kwenye kaviti ya fumbatio na fetasi kufariki haraka ila upasuaji wa haraka uitoe.
Mwisho wa jibu
Tumia miongozo hii ili kuzuia au kupunguza hatari ya kuraruka kwa uterasi kwa wanawake walio katika leba:
Usiache mwanamke akawie katika kipindi cha kwanza au cha pili cha leba kwa muda mrefu. Wape wanawake hawa rufaa haraka.
Je, ni lini unapopaswa kumpa rufaa mwanamke aliyezaa zaidi ya mara moja au anayezaa kwa mara ya kwanza ambaye leba yake imekaa kwa muda mrefu? (Kumbuka Kipindi cha 9.)
Wape rufaa wanawake walio na ishara hizi za leba iliyokaa sana:
Mwisho wa jibu
Wajibu wako mkuu ni uzuiaji wa kimsingi. Hakikisha kuwa iwapo leba itazuilika, unaweza kumpeleka mwanamke huyu katika kituo cha afya apate utunzaji wa dharura kwa wakati unaofaa ili kuzuia kuraruka kwa uterasi. Hata hivyo, sababu nyingi zinaweza kuhitaji kuwa umpe mwanamke aliye na uterasi iliyoraruka utunzaji wa dharura. Kisha jukumu lako ni uzuiaji wa baadaye wa maambukizi yanayohusiana na urarukaji wa uterasi.
Kumbuka ulichosoma katika moduli ya utunzaji katika ujauzito (Kipindi cha 13) na majadiliano kuhusu jinsi ya kutoa rufaa. Je, ni nini unachopaswa kukumbuka kufanya?
Fanya mambo haya unapotoa rufaa:
Mwisho wa jibu
Mwanamke aliye kwenye mshtuko anahitaji usaidizi wa haraka. Mtibu haraka ili kuokoa maisha yake.
Mshtuko ni athari isiyoepukika ya uterasi iliyoraruka. Mpe rufaa haraka aende katika kituo cha afya kilicho karibu chenye huduma zinazofaa za utunzaji wa dharura. Njiani, hakikisha kuwa mwanamke amelala miguu yake ikiwa juu kidogo kuliko kichwa chake na kichwa chake kimekunjwa kuelekea upande mmoja (Mchoro 10.2). Hakikisha anapata joto na ametulia.
Ikiwa umefundishwa kufanya haya, anza kwa kumpa viowevu mishipani. Ulisoma jinsi ya kufanya hivi katika Moduli ya utunzaji katika ujauzito, Kipindi cha 22 na katika mafunzo yako ya ujuzi tendaji. Ikiwa ana fahamu, anaweza kunywa maji au viowevu vya kumwongezea maji (chumvi za mdomoni za kuongeza maji). Ikiwa hana fahamu, usimpe kitu chochote mdomoni. Usimpe dawa, kinywaji au chakula.
Unafaa kuwa ulishatimiza matayarisho haya:
Hatimaye jaribu kupunguza kuchelewa, jambo linaloweza kuwa ndilo tofauti kati ya uhai na mauti. Wanawake wengi waafrika hufariki kutokana na urarukaji wa uterasi kwa sababu wanasita kutafuta usaidizi maalum wakati wa kuzaa. Kisha wanachelewa kutafuta usaidizi wa kimatibabu baada ya urarukaji wa uterasi. Matibabu yanacheleweshwa zaidi kwa sababu ya umbali wa kituo cha afya au ukosefu wa vifaa na wahudumu mwanamke anapofika kwa utunzaji wa dharura.
Kumbuka mambo haya yote ili kuhakikisha kuwa mwanamke huyu amepewa rufaa ya kwenda katika kituo mwafaka haraka kwa utatuzi na utunzaji wa dharura.
Katika Kipindi cha 10, ulisoma yafuatayo:
Kwa kuwa umekamilisha kipindi hiki, jibu maswali haya ili kutathmini ulivyosoma. Unaweza kulinganisha majibu yako na Muhtasari juu ya Maswali ya Kujithmini mwishoni mwa Moduli hii.
Ni mambo yapi yanayoweza kumfanya mwanamke apate urarukaji wa uterasi?
Mambo haya yanaongeza hatari ya kuraruka kwa uterasi: (Maneno muhimu yako kwenye herufi nzito.)
Mwisho wa jibu
Kwa nini wanawake waliozaa zaidi ya mara moja wako katika hatari kubwa ya urarukaji wa uterasi kuliko wale wanaozaa mtoto wa kwanza?
Wanawake wanaozaa mtoto wa kwanza wanazaa kwa mara ya kwanza. Katika uzazi wa kwanza, kuna uwezekano wa leba kuwa ndefu. Hata hivyo, kwa wanawake hawa, inesha yauterasi hutokea baada ya takribani saa 36. Minyweo huwa dhaifu na mifupi, na yenye muda mrefu baina yake. Inesha ya uterasi hupunguza hatari ya urarukaji wa uterasi kwa kiwango kikubwa .
Kwa upande mwingine, wanawake waliozaa zaidi ya mara moja wamepata angalau mtoto mmoja baada ya majuma 28 ya ujauzito. Uterasi ya wanawake hawa hunywea mno kwa muda mrefu zaidi kuliko uterasi ya wale wanaozaa kwa mara ya kwanza. Ikiwa uzuio utazuia kuzaa kwa muda mrefu, hasa ikiwa kuna kovu kutokana na matatizo ya uzazi wa hapo awali, kuna uwezekano mkubwa wa uterasi kuraruka.
Mwisho wa jibu
Kamilisha Jedwali 10.1. Ongeza maelezo ya dalili za hatari za urarukaji wa uterasi unaoweza kutokea.
Hatua | Dalili za hatari |
---|---|
Pima muda wa vipindi vya leba | |
Pima minyweo ya uterasi | |
Chunguza kiwango cha mpigo wa moyo wa fetasi | |
Chunguza fumbatio | |
Chunguza uke |
Jedwali 10.1 lililokamilishwa ndilo hili hapa.
Hatua | Dalili za hatari |
---|---|
Pima muda wa vipindi vya leba | Leba ndefu sana: kipindi cha kwanza cha awamu fiche kinadumu zaidi ya saa18; kipindi cha kwanza cha awamu ya leba dhahiri kinadumu zaidi ya saa 12; kipindi cha kinadumu zaidi ya saa 1 kwa wanawake waliozaa zaidi ya mara moja, au zaidi ya saa 2 kwa wanawake wanaozaa kwa mara ya kwanza |
Pima minyweo ya uterasi | Minyweo ya uterasi inayoendelea kutokea inayodumu kwa muda wa sekunde 60 - 90 au zaidi, inayotokea zaidi ya mara 5 kwa kila dakika 10 |
Chunguza kiwango cha mpigo wa moyo wa fetasi | Kiwango cha mpigo wa moyo wa fetasi kinaendelea kuwa zaidi ya mipigo 160 kwa dakika au chini ya mipigo 120 kwa dakika |
Chunguza fumbatio | Sehemu ya chini ya uterasi ni nyororo ukitomasa; kizingo cha Bandl kipo |
Chunguza uke | Kunaweza kuwa na kutokwa na damu |
Mwisho wa jibu
Mwisho wa jibu