10. Uterasi Iliyoraruka

Kipindi cha 10 Uterasi Iliyoraruka

Utangulizi

Kuraruka kwa uterasi hutokea uterasi inaporaruka au kupasuka kutokana na shinikizo litokanalo na leba iliyozuilika. Urarukaji wa uterasi hutokea sana katika nchi zinazoendelea barani Afrika. Barani Afrika, asilimia 94 ya uzazi hufanyika nyumbani na bila kushughulikiwa na mtaalamu wa afya mwenye ujuzi. Leba ikikamilika kwa kuraruka kwa uterasi, mwanamke huyo anaweza kufariki. Ikiwa mwanamke huyo ataongoka, anaweza kumpoteza mtoto au uterasi yake.

Takribani visa vyote vya urarukaji wa uterasi hutokea kwa wanawake waliozaa zaidi ya mara moja hapo awali ambao wamezaa angalau mara moja baada ya ujauzito wao kutimiza umri wa majuma 28. Urarukaji wa uterasi unaweza pia kutokea kwa wanawake walio na kovu kwenye uterasi. Uterasi huraruka tishu ya kovu hili inapofunguka. Hata hivyo, katika nchi zinazostawi, karibu visa vyote vya urarukaji wa uterasi hutokea kwa wanawake wasio na kovu kwenye uterasi ambao leba yao ilizuilika palipokosa utatuzi. Katika kipindi hiki, utasoma kuhusu mambo ya hatari na ishara za kitabibu za uterasi iliyoraruka. Utasoma kuhusu athari kwa mama na mtoto. Utasoma pia jinsi ya kuanza utatuzi unaoweza kuokoa mama na mtoto wake.

Malengo ya Somo la Kipindi cha 10