Skip to main content
Printable page generated Wednesday, 8 May 2024, 1:08 PM
Use 'Print preview' to check the number of pages and printer settings.
Print functionality varies between browsers.
Unless otherwise stated, copyright © 2024 The Open University, all rights reserved.
Printable page generated Wednesday, 8 May 2024, 1:08 PM

4. Maandalizi ya Utunzaji wa baada ya Kuzaa

Kipindi cha 4 Maandalizi ya Utunzaji wa baada ya Kuzaa

Utangulizi

Unafahamu kuhusu mambo haya kutoka kwenye moduli ya Utunzaji wa Wajawazito na Utunzaji katika Leba na Kuzaa

Mara nyingi, utaanza kujadiliana na mama na familia yake kabla hajazaa kuhusu jinsi atakavyojitunza baada ya kuzaa. Ni katika kuwazuru wajawazito ambapo utakusanya habari kuhusu mama, familia na hali zao za kijamii. Pia unaweza kuwapa anwani yako na uwaarifu kuhusu namna ya kukufikia wanapohitaji usaidizi wako. Wakati wa ujauzito, pia unawahimiza kina mama wote wazalie katika kituo kikuu cha afya, kama itawezekana, ingawa zaidi ya 94% ya wanawake wa mashinani mwa Afrika huzalia nyumbani. Katika kauli kama hizo, ishauri familia yake kukufahamisha punde leba inapoanza.

Ikiwa utakuwepo mwanamke akizaa, tayari unafahamu kwamba unapaswa kukaa naye kwa angalau saa 6 za kwanza baada ya kuzaa. Hata hivyo, ikiwa alizaa wakati hukuwepo, mtembelee haraka iwezekanavyo, hususan katika saa chache baada ya kuzaa, wala usichelewe hata kwa siku moja.

Kabla ya kumzuru mama kwa mara ya kwanza baada ya kuzaa, andaa vifaa na dawa unazohitaji ili kumpa huduma bora. Katika Kipindi hiki, utajifunza kuhusu vifaa, ratiba na malengo ya kumzuru mama baada ya kuzaa. Pia utajifunza kuhusu hatua za maandalizi muhimu yanayofanywa kabla ya kuondoka, na yale utakayofanya ukiwa nyumbani mwa mama.

Malengo ya Somo la Kipindi cha 4

Baada ya kukamilisha Kipindi hiki unapaswa:

4.1 Kufasili na kutumia kwa usahihi maneno yote yalioandikwa kwa herufi zito (Swali la Kujitathmini 4.1)

4.2 Kueleza ni kwa nini ziara za nyumbani ni fursa muhimu ya kutoa huduma ya utunzaji baada ya kuzaa. Pia, eleza kuhusu mambo yanayozuia kuitolea huduma hii katika kituo cha afya barani Afrika. (Swali la Kujitathmini 4.2)

4.3 Kueleza kuhusu ratiba inayopendekezwa unapofanya ziara za nyumbani ili kutoa huduma ya utunzaji baada ya kuzaa katika kauli zisizo na utata na zile zinazohitaji utunzaji spesheli. (Swali la Kujitathmini 4.1)

4.4 Kueleza kuhusu maandalizi, vifaa na dawa unazopaswa kuwa nazo kabla ya kumzuru mama. (Swali la Kujitathmini 4.3)

4.5 Kueleza kuhusu hatua muhimu za kufuata katika ziara ya nyumbani, ikiwemo namna ya kushawishi familia yake wawe na imani na taaluma na uwezo wako. (Swali la Kujitathmini 4.3)

4.6 Kueleza kuhusu umuhimu wa kutumia ustadi katika ushauri ili kuwasilisha ujumbe wa afya kuhusu utunzaji baada ya kuzaa. Pia, ufahamu namna ya kuthibitisha kama mama ameelewa. (Swali la Kujitathmini 4.3)

4.1 Ziara za nyumbani: fursa nzuri ya kutoa utunzaji wa baada ya kuzaa

Njia bora ya kutoa huduma ya mama na mtoto ni inapotolewa katika kituo cha afya na mhudumu wa afya aliyehitimu. Hata hivyo, barani Afrika mna changamoto nyingi zinazozuia kulitimiza lengo hili, kama vile uhaba wa vituo, wahudumu wa afya waliohitimu, na pia ugumu wa kufikia vituo vya afya kwa watu wa vijijini.

Inaweza kuchukua miaka mingi kutatua changamoto hizi. Kwa hivyo, unapoendelea kufanya juhudi ili kuboresha mfumo wa afya na ufikikaji katika vituo vya afya humo mashinani, jukumu lako sasa kama Mhudhumu wa Afya Ugani ni kulenga ziara za nyumbani ili kutoa huduma ya utunzaji wa baada ya kuzaa.

4.1.1 Changamoto za utunzaji wa baada ya kuzaa unaofanyiwa kituoni

Kabla ya kuanzisha huduma ya utunzaji wa baada ya kuzaa katika jamii yako, kwanza unapaswa kufahamu kuhusu changamoto zake. Pia unapaswa kuelewa kwa kina sababu zinazofanya ziara za nyumbani kubakia kama njia kuu za kutoa huduma ya utunzaji mle mashinani. Changamoto kuu zinazozuia utunzaji wa baada ya kuzaa unaofanyiwa kituoni ni:

Mchoro 4.1: Umbali wa kituo ni changamoto kuu kwa wanawake wanaotaka utunzaji wa baada ya kuzaa.
  • Changamoto za kijamii na kimila: tambiko na tamaduni za jamii kama vile kumfungia mama na Kipindi nyumbani kwa siku chache baada ya kuzaa, katika kipindi cha kutengwa huwazuia kina mama kutembelea kituo kupata huduma. Unapaswa kuchunguza changamoto hizi pole pole katika eneo lako ukishirikiana na viongozi wa jamii ili kubadilisha desturi hizi.
  • Changamoto za kijiografia: kupanda milima, kuvuka mito isiyo na madaraja katika msimu wa mvua na ukosefu wa barabara ni baadhi ya changomoto za kijiografia zinazowazuia wanawake kukifika kituo ili kuhudumiwa. (Mchoro 4.1).
  • Umbali wa kituo: Hata ingawa baadhi ya wanawake wangependelea kwenda kituoni au hospitalini, kituo kilicho karibu hakifikiki kwa mguu au kwa kutumia chombo cha usafiri kilichoko.
  • Changamoto za kifedha. Katika sehemu fulani za afrika, watu huamini kuwa huduma za afya zinazohusu leba, uzazi na utunzaji baada ya kuzaa hutolewa bila malipo. Ukweli ni kwamba ni sharti familia igharamie nauli ili mama afike kituoni, na pia ilipie vifaa vinavyotumika kama vile dawa na glavu. Gharama hii ya ziada ni changamoto kuu kwa huduma ya baada ya kuzaa inaayotolewa kituoni.
  • Changamoto za ubora wa huduma: Wanapofika kituoni, mama na mtoto Kipindi wanaweza kukosa huduma bora walizotarajia kwa sababu za ukosefu wa wahudumu wa afya waliohitimu vyema au upungufu wa vifaa au dawa. Huduma duni hupunguza imani ya baadhi ya wanawake, hivyo wanaweza kupunguza juhudi zao za kufikia kituoni.
  • Lengo la pili muhimu la ziara ya nyumbani ili kutoa huduma za utunzaji baada ya kuzaa ni kutafiti baadhi ya changamoto za kijamii na kimila zilizotajwa hapo juu, kisha uungane na viongozi wa jamii kujaribu kuzibadilisha. Kipindi cha 1 cha moduli hii kilieleza njia nyingi unazoweza kutumia ili kufanya hivi. Kwa kurejelea maswala hayo, andika ratiba fupi ya hatua utakazojaribu kufanya.

  • Kuna hatua nyingi ambazo huenda ulijumuisha. Rejelea Kipindi cha 1, Kifungu cha 1.6, na ulinganishe majibu yako na maoni yaliyoko.

4.1.2 Ushahidi unaoonyesha kuwa ziara ya nyumbani huimarisha ubora wa utunzaji wa baada ya kuzaa

Kinachosikitisha ni kuwa hakuna utafiti wa kutosha kuhusu ziara ya nyumbani katika bara la Afrika ili kuwa kielelezo kinachoweza kuigwa katika kila eneo. Hata hivyo, kuna ushahidi na mifano kutoka Asia Kusini inayoonyesha matokeo muhimu katika kuimarisha utunzaji baada ya kuzaa na kupunguza kima cha vifo vya kina mama na watoto wachanga kwa kipindi kifupi kupitia mtazamo wa ziara ya nyumbani. Bila shaka, kuna tofauti za kimila katika nchi mbalimbali, ingawa matokeo yanatia moyo. Kwa mfano, utafiti uliofanywa nchini India, Bangladesh na Pakistan umeonyesha kuwa ziara za nyumbani zinaweza kupunguza vifo vya watoto wachanga kwa 30-61% katika nchi zinazostawi, ambapo vifo vingi hutokea. Ziara za nyumbani hasa huimarisha utimizaji wa maswala ya watoto wachanga yenye umuhimu mkuu na yenye gharama ya chini.

Maswala haya ni kama:

  • Kuanza kumnyonyesha mtoto mapema.
  • Kuguzana kwa ngozi ya mama na ya mtoto (Mchoro 4.2).
  • Kuchelewesha kumuosha mtoto Kipindi hadi angalau saa 24 baada ya kuzaliwa.
  • Kusisitiza kanuni za usafi, kama vile kunawa mikono kwa sabuni na maji safi.
  • Kuzingatia usafi wa kitovu cha mtoto.
Mchoro 4.2 Kuguzana kwa ngozi ya mama na ya mtoto husaidia kuimarisha mapenzi kati yao na kudhibiti jotomwilini la mtoto.

Tutarejelea maswala hayo baadaye katika Kipindi hiki, au baadaye katika moduli hii. Ingawa hatuna utafiti unaotoka Afrika ili kulinganisha, utafiti huu kutoka Asia Kusini unaonyesha vipengele vikuu vinavyohitajika ili kutoa huduma mwafaka ya utunzaji wa mtoto na mama nyumbani.

4.2 Ratiba ya ziara za nyumbani kutekeleza utunzaji wa mtoto na mama baada ya kuzaa

Kwa sasa kuna ushahidi wa na maafikiano ya kutosha kuhusu vipengele vya kimsingi vya utunzaji wa baada ya kuzaa, ili kuimarisha afya na uhai wa kina mama na watoto wachanga. Hata hivyo, bado ni vigumu kupata mapendekezo yanayozingatia utafiti ambayo yanaweza kutumiwa kama kipimo kwa kiwango cha nyakati na marudio ya ziara za nyumbani. Mataifa mbali mbali ya Asia Kusini yameona nyakati tofauti za kufanya ziara, lakini yote yalitambua kuwa kina mama walitembelewa angalau mara 2 – 3 katika wiki ya kwanza baada ya kuzaa. Katika kauli zote, ziara ya kwanza ilikuwa katika saa 24 baada ya mtoto kuzaliwa.

Kama ulivyojifunza katika Kipindi cha 1 cha Moduli hii, saa 24 na siku saba za kwanza baada ya kuzaa ni muhimu ambapo kina mama na watoto wachanga mara nyingi hufa. Kulingana na habari zilizoko ambazo zinatokana na matukio ya nchi zingine, na uwezekano wa kutekeleza kila kauli katika bara Afrika, Shirika la Afya Duniani limependekeza ratiba ya ziara ya nyumbani ili kutoa huduma ya baada ya kuzaa. Kwa wanawake wasiokumbwa na matatizo, na walizaa mtoto aliyepevuka na mwenye uzito wa kawaida wakati wa kuzaliwa, ziara ya nyumbani imependekezwa ifanywe kama ifuatavyo:

  1. Ziara ya kwanza inapaswa kufanyika katika saa 24 za kwanza. Ikiwa inawezekana, mzuru mama haraka iwezekanavyo.
  2. Ziara ya pili iwe siku ya tatu baada ya mama kuzaa.
  3. Ziara ya tatu iwe siku ya saba baada ya mama kuzaa.
  4. Ziara ya nne ni katika wiki ya sita baada ya mama kuzaa.

Moduli inayohusu Udhibiti unaojumuisha Maradhi ya Utotoni na ya Watoto wachanga itakufunza kwa kina kuhusu ziara hizi za ziada za nyumbani.

Ziara nyongeza huitajika katika siku ya tano na ya kumi baada ya kuzaa, hasa katika hali spesheli kama vile katika:

  • Watoto waliozaliwa kabla ya wakati (wale waliozaliwa kabla ya wiki 37 ya ujauzito)
  • Watoto waliozaliwa na uzito wa chini (wenye uzani wa chini ya kilogramu 2.5)
  • Watoto na kina mama wote wagonjwa.
  • Kina mama wanaoishi na VVU.

Watu wa familia pia wanapaswa kuomba uende haraka ikiwa mtoto au mama ana tatizo wakati wowote baada ya kuzaa. Watu wa familia zingine wanaweza kusita kukuhusisha, hivyo basi, ni muhimu kwako kila wakati kumuhakikishia kila mmoja kuwa ni bora kukuarifu ikiwa wanatilia shaka afya ya mama au mtoto.

4.3 Maandalizi ya ziara ya nyumbani

4.3.1 Usafi wa kibinafsi

Mchoro 4.3 Wajihi wako unafaa kumhimiza mama akuamini katika usatadi wako.

Kabla ya kuanza ziara, hakikisha umeshughulikia usafi wako binafsi, hususan kwa kuzingatia nywele, kucha na nguo zako. Maagizo haya yanaweza kuwa rahisi na ya kimsingi, lakini wajihi na usafi duni unaweza kuathiri vibaya uusiano wako na jamii na familia, na pia kuaminika kwa kazi yako. Vaa nguo za kawaida. Lakini zilizo safi unapokuwa ziarani kupeana huduma ya utunzaji baada ya kuzaa. (Mchoro 4.3)

  • Ni sababu gani nyengine inayofanya iwe muhimu kusisitiza usafi? Rejelea uliyojifunza katika baadhi ya vikao vya mbeleni katika moduli hii.

  • Kutilia maanani usafi na unadhifu wakati mama anapozaa na katika ziara za kutoa huduma ya utunzaji wa baada ya kuzaa husadia kuzuia maambukizi baada ya mtoto kuzaliwa. Ukizingatia usafi wako binafsi, itakuwa rahisi kumshawishi mama na familia yake kuhusu umuhimu wa usafi iwapo atazalia nyumbani katika siku zijazo.

4.3.2 Vifaa

Kisanduku 4.1 Vifaa vinayohitajika katika ziara ya baada ya kuzaa
  • Mizani ya Salter ili kumpimia mtoto.
  • Kifaa cha kupimia shinikizo la damu Stethoskopu

  • Kipimajoto

    Saa ya mkono au kipima wakati, ili kukusadia kupima kima cha mpwito wa damu na cha upumuo.

  • Sabuni ya kunawia mikono yako.
  • Taulo safi ya kukausha mikono yako.
  • Kapsuli ya vitamini A.
  • Tembe za Iron na folate.
  • Dawa za kupaka macho aina ya Tetracycline.
  • Kadi ya ushauri na ya uchunguzi wa utunzaji ya baada ya kuzaa.
  • Kitabu cha kuweka rekodi, fomu ya rufaa na kalamu.

Utapewa kadi ya ushauri na ya uchunguzi na fomu ya rufaa ya eneo lako. Kuna uwezekano wa kadi hizi kutofautiana kimaneno na umbo katika maeneo tofauti, lakini kimsingi zote huzingatia maswala sawa.

4.4 Hatua kuu za kufuata unapomzuru mama nyumbani

Ili kuleta hali ya kumjali mama na kuifanya familia yake ikwamini, unapaswa kuzingatia mambo yafuatayo:

  • Fahamu na udhiirishe kuwa unaheshimu imani, mila na desturi zao mnapozungumza.
  • Mwamkue kila mmoja ukitumia maneno yanayofahamika kwao.
  • Eleza sababu za ziara hiyo kwa mama na familia, ukitumia maneno ya lugha yao yanayoeleweka.
  • Tenga nafasi kubwa ya mazungumzo ya kijumla na kuleta imani baina yenu.
  • Onyesha ujasiri katika mazungumzo yako kwa kutumia sauti ya upole, na pia kuteleka wajibuwako kwa ujasiri.
  • Mheshimu kila mtu katika familia.

Ulizia kuhusu hali ya mama na mtoto na ukadirie kama kila mmoja wao ana tatizo lolote la kiafya, au kama kuna ugumu wa kukaribisha ‘mtoto mgeni’ katika familia. Tumia mtazamo wa kuchunguza uliokubalika: uliza, chunguza, orodhesha na uchukue hatua. Jambo muhimu zaidi ni kutumia kadi za uchunguzi ili kukusaidia kubaini hali yoyote inayohatarisha maisha au dalili zozote hatari kwa kina mama na watoto wachanga. Tayari umejifunza namna ya kufanya hivi katika Kipindi cha 1 na 3.

Ukitumia kadi za ushauri, mshauri mama kuhusu afya yake na hali na afya ya mtoto. Kila wakati, kadiria baadaye kama alielewa ushauri huo. (Rejelea kifungu Kifungu cha 4.5 hapa chini).

Jaza fomu ya ziara ya nyumbani na upangie siku ya ziara nyingine. Mshukuru kila mmoja kwa kukukaribisha nyumbani.

4.5 Kuwashauri kina mama katika kipindi cha baada ya kuzaa

Ili kutimiza matarajio ya ushauri kwa mama kuhusu kipindi cha baada ya kuzaa kwa kuwazuru nyumbani, unapaswa kutumia kadi za ushauri zinazotolewa katika Shirika la Afya Mkoani. Unapowashauri kina mama, ni muhimu kutumia hatua za kiustadi zifuatazo:

  • Uliza na usikilize: Peleleza yale ambayo mama tayari anajifanyia mwenyewe, na mtoto wake kwa kumuuliza maswali yanayohusisha kufikiria, na uyasikilize kwa makini majibu yake. Hivyo, utafahamu yale mambo anayofanya kwa usahihi, na yale yanayohitaji kubadilishwa.
  • Msifu: Msifu mama kwa chochote cha dhamani alichokifanya. Kuna uwezekano kuwa kuna mambo ya dhamani kwake na kwa mtoto ambayo amefanya. Kwa mfano, anaweza kuwa anakula chakula bora, anamnyonyesha mtoto bila kumpa vyakula vya ziada, na kuzingatia usafi wake na wa mtoto. Hakikisha kuwa umemsifu bila unafiki, na kuwa umemsifu kwa mambo yatakayomfaidi yeye na mtoto wake kiafya.
  • Mshauri: Mshauri tu kuhusu mambo yaliyo muhimu kwake wakati huo pekee. Mawaidha mengi, au yanayotolewa wakati usiofaa yanaweza kumkanganya, hivyo anaweza kuyafutilia mbali. Tumia lugha anayoielewa. Ikiwezekana, tumia picha, kadi za uchunguzi, au vielelezo ili kumwelezea bayana yale anayohitajika kufanya, kufahamu au kuelewa.
Mchoro 4.4 Peleleza kwa umakini ili kubaini kama mama ameelewa ujumbe wako wa kiafya
  • Peleleza kama ameelewa: Ukimwelezea mama chochote, mwulize maswali ili kubaini anachoelewa na anachohitaji afafanuliwe zaidi (Mchoro 4.4). Usimwulize maswali elekezi (yaani, maswali yanayomwashiria jibu sahihi hata ikiwa haelewi). Pia usiulize maswali yanayojibiwa kwa ndio au la, kwa sababu hayasaidii kubaini kwa kina kile ambacho mama ameelewa.

Maswala muhimu ya kiafya unayopaswa kuzingatia unamposhauri mama baada ya kuzaa ukiwa katika ziara ya nyumbani yameonyeshwa katika Kisanduku 4.2.

Kisanduku 4.2 Maswala ya kiafya unayofaa kuzingatia unapomshauri mama

  • Kubaini dalili za kijumla za hatari
  • Usaidizi wa kihisia
  • Usaidizi wa lishe kwa mama
  • Kuimarisha kipeo cha kunyonyesha
  • Usafi na udhibiti maambukizi
  • Usaidizi wa upangaji uzazi
  • Huduma spesheli kwa kina mama walioambukizwa VVU
  • Mama na mtoto Kipindi kutafuta matibabu wakati unaofaa ikiwa matatizo yatatokea
  • Utunzaji wa kila mara kwa mtoto mwenye hali ya kawaida ya afya

Utajifunza zaidi kuhusu maswala haya katika vikao vijavyo vya moduli hii.

  • Ni mara ya pili umemtembelea mama aliyezalia nyumbani. Anakufahamisha kuwa mtoto wake analia sana, na alilala kwa muda mfupi na anajihisi kama ambaye amefura na mchovu sana. Je, utafanya nini?

  • Ni wazi kwamba unafaa umchunguze zaidi. Je, mama anaona shida kumlisha mtoto - anaweza kuwa na mastitisi? Je, mama na mtoto wanaweza kuwa na maambukizi fiche, kama vile matatizo kwenye kitovu cha mtoto ama maambukizi ya kindonda katika msamba wa mama? Je, mama anapata lishe bora analohitaji, na familia na jamii yake wanamasidia? Ikiwa maswali ya kwanza (na ikiwezekana uchunguzi) yanakuridhishia kwamba hakuna jambo la hatari kubwa, basi unaweza kumshauri ifaavyo. Ikiwa unafikiria ana matatizo, basi mpe rufaa.

    Mwisho wa jibu

Muhtasari wa Kipindi cha 4

  1. Changamoto kuu katika utoaji huduma za Utunzaji wa baada ya Kuzaa katika vituo vya afya ni changamoto za kijamii, kitamaduni, kimaumbile, kijografia, kidhamani na kifedha. Mtazamo wa kuwatembelea wateja nyumbani ndio unaotumika kushughulikia matatizo haya ifaavyo katika jamii za mashinani.
  2. Utaratibu wa kutoa huduma za Utunzaji wa baada ya Kuzaa za kuwatembelea nyumbani wanawake wasio na matatizo na watoto wachanga ni: ziara ya kwanza katika saa za 24 kwanza baada ya kujifungua, kisha umtembelee tena siku ya tatu, ya saba na wiki ya sita.
  3. Ni sharti pia uwatembelee siku ya tano na ya kumi kina mama wote wagonjwa na watoto wachanga, kina mama walioambukizwa virusi vya UKIMWI, watoto wenye uzito wa chini na waliozaliwa kabla ya wakati.
  4. Unapomtembelea mteja nyumbani kwa huduma za Utunzaji wa baada ya Kuzaa, hakikisha kuwa umevaa mavasi ya kadri lakini yaliyo safi, nawe uzingatie usafi mwenyewe.
  5. Usisahau kubeba vifaa na dawa muhimu zinazohitajika wakati wa kutoa huduma za Utunzaji wa baada ya Kuzaa.
  6. Waheshimu watu wote nyumbani. Kuwa na ujasiri na uwasiliane vyema kwa lugha na istilahi zinazoeleweka.
  7. Tumia kadi na fomu zilizoko ili kuhakikisha umeshughulikia vipengee vyote vya uchunguzi na ushauri, hasa kutambua dalili hatari kwa mama na mtoto Kipindi.
  8. Unapomshauri mama unafaa kumuuliza na kumsikiliza, uzisifu hatua bora alizochukua, umpe ushauri anaohitaji kujua kwa wakati huo pekee, na upeleleze kama ameelewa ushauri huo.

Maswali ya Kujitathmini ya Kipindi cha 4

Sasa kwa kuwa umemaliza Kipindi hiki, jibu maswali haya ili kukadiria uliyojifunza. Swali la Kujitathmini 4.1(litathmini Malengo ya Somo la 4.1 na 4.3)

Unapangia utunzaji baada ya kuzaa kwa mama aliyezaa kabla ya wakati, na mtoto yuko na uzito wa chini ya kawaida. Eleza uainishaji huu, kisha uweke ratiba yako ya utunzaji ukieleza jinsi gani (na kwa nini) ratiba hii ya utunzaji inatofautiana na ile ya mtoto mwenye uzito wa kawaida, aliyezaliwa wakati ufaao.

Answer

Mtoto aliyezaliwa kabla ya wakati ni -aliyezaliwa kabla ya wiki ya 37 ya ujauzito. Mtoto mwenye uzito wa chini ya kawaida ni aliye na uzito wa chini ya gramu 2500. Kwa kawaida, tukichukulia kuwa huyu mtoto alizaliwa kabla ya wakati, unatumai kuwa jamii ingekuharifu mapema ili uwepo mtoto anapozaliwa. La si hivyo, basi unafaa kufika hapo haraka iwezekanavyo katika saa 24 za kwanza baada ya mtoto kuzaliwa. Baadaye, utahitaji kupanga jinsi utawatembelea siku ya tatu, tano, saba na ya kumi, halafu katika wiki ya sita baada ya kuzaa. Ziara za siku ya sita na ya kumi ni za ziada ukilinganisha na ratiba unayoweza kumpangia mtoto aliyezaliwa wakati ufaao. Hii ni ishara ya hatari kubwa ya vipindi vya mwanzo vya utotoni (siku saba za kwanza) ikiwa mtoto amezaliwa kabla ya wakati ama yuko na uzito mdogo.

Mwisho wa jibu

Swali la Kujitathmini 4.2 (linatathmini Malengo ya Somo la 4.2)

Ingetarajiwa kuwa kina mama wote barani Afrika wangepata huduma za hali ya juu katika vituo vya afya. Ni sababu gani kuu zinazopelekea hali hii isitimilike kwa sasa, na ni kwa nini ziara za nyumbani ni muhimu sana?

Answer

Changamoto kuu za huduma ya baada ya kuzaa katika vituo vya afya zimeorodheshwa katika Kifungu cha 4.1.1. Linganisha majibu yako na vidokezo vilivyoorodheshwa hapo. Je, ulifikiri kuhusu changamoto zingine, labda kutokana na matukio uliyoshuhudia mwenyewe? Ikiwa ni hivyo, basi ni vyema.

Kuwazuru kina mama nyumbani katika kipindi cha baada ya kuzaa ni muhimu kwa sababu ziara hizi huchangia pakubwa katika kuendelea kuishi kwa watoto wachanga kwa kijumla. Utafiti wa ule mfano wa Asia Kusini unaonyesha upungufu wa visa vya vifo vya kina mama kwa kati ya 30% na 61% kwa sababu ya ziara za nyumbani. Hatua mbali mbali zimeorodheshwa katika Kifungu cha 4.1.2.

Mwisho wa jibu

Maswali ya Kujitathmini 4.3 (yanathmini Malengo ya Somo la 4.4, 4.5 na 4.6)

Unapangia kumtembelea Naomi. Yeye ni mama aliyezaa kifungua mimba chake siku kumi zilizopita. Umemtembelea hapo awali, lakini ana haya sana hivyo inakuchukua muda mrefu kumfahamu yeye na familia yake. Unajitayarisha kuondoka kwenda kwake, na unashangaa jinsi utakavyowafanya wakuamini.

  • a.Unapoendelea kufunga virago vyako, unafikiria kuhusu kupeleleza iwapo una vyote unavyohitaji katika ziara ya baada ya kuzaa, kisha unaandika kumbusho la kutumia wakati ujao. Umeandika nini?
  • b.Baadaye, unaandika vidokezo zaidi kuhusu mambo muhimu ya kukumbuka utakapokutana na Naomi wakati mwingine umeandika nini?
Answer

Yafuatayo ni baadhi ambayo huenda umeyaandika:

Mfuko wa vifaa

Ninahitaji kudhibitisha kuwa vifaa vifuatavyo havijaisha – kapsuli za Vitamini A, vidonge vya iron, lihamu ya tetracycline nk., na sabuni!

Taulo safi? Saa ya mkono? Kadi za ushauri na uchunguzi za kutosha? Kitabu cha kurekodi, kalamu, na fomu za rufaa?

Vifaa vyote vya kawaida vinavyobakia mfukoni: mizani, stethoskopu, vifaa vya kupima shinikizo la damu, kipimajoto nk.

Kisha nitahitaji kujiangalia kama niko safi na mnadhifu!

Lakini nitachukua hatua gani ili kumpunguzia hofu Naomi? Haya ni baadi tu ya maswali machache ninayoweza kujiuliza:

‘Labda situmii istilahi mwafaka kikamilifu, kwa hivyo familia yake pengine inafikiria kuwa siheshimu desturi zao. Sijui kama ushauri wangu unasikika kama wenye ufidhuli au ukali- inanilazimu kukumbuka kuwa mpole na kumpa muda wa kutosha kwa mazungumzo ya kijumla ili kumtuliza. Utaratibu huu ni mgumu sana kwa sababu kuna mengi ya kufanya, hivyo inanibidi kujiharakisha kila mara. Najua yeye hunisikiza lakini pengine ninampa ushauri mwingi. Nitajaribu zaidi kumsifu na kumsikiza wakati huu na labda hatua hizi zitasaidia’.

Mwisho wa jibu