Katika Kipindi hiki, utajifunza kuhusu huduma maalum na ya ziada inayohitajika na watoto waliozaliwa kabla ya kuhitimu muhula na waliozaliwa wakiwa na uzani wa chini. Tutaleleza kwa kina sababu za watoto hawa kuhitaji utunzaji maalum, na jinsi unavyoweza kuwahudumia. Pia tutaeleza jinsi ya kuwashauri kina mama na watu wengine wa familia kuhusu kuwahudumia watoto hawa. Lengo letu ni kudhibiti matatatizo yanayohusiana na kuwalisha watoto waliozaliwa kabla ya kuhitimu muhula na waliozaliwa wakiwa na uzani wa chini, na jinsi ya kuwapasha joto. Utajifunza hasa kuhusu njia mwafaka na inayochukuliwa kuwa ya kisasa ya kudhibiti jotomwili la mtoto mkembe au mwenye kimo kidogo sana. Njia hii hujulikana kama Utunzaji wa Mama wa aina ya Kangaruu.
Baada ya somo hili, unatarajiwa:
8.1 Kufasili na kutumia kwa usahihi maneno yote muhimu yaliyoandikwa kwa herufi nzito. (Swali la Kujitathmini 8.2 )
8.2 Kueleza ni kwa nini watoto waliozaliwa kabla ya kuhitimu muhula au wakiwa na uzani wa chini wanahitaji utunzaji maalum, kisha uorodheshe matatizo yanayoweza kuwakumba mara nyingi. (Swali la Kujitathmini 8.1 )
8.3 Kutoa uainisho wa watoto waliozaliwa kabla ya kuhitimu muhula kwa kurejelea umri wa ujauzito na uzani wa wakati wa kuzaliwa, na ueleze mikakati mwafaka ya kudhibiti hali hizi katika kila kauli. (Swali la Kujitathmini 8.2 )
8.4 Kueleza jinsi unavyoweza kumshauri mama kuhusu jinsi ya kumlisha mtoto aliyezaliwa kabla ya kuhitimu muhula au akiwa na uzani wa chini. (Swali la Kujitathmini 8.3 )
8.5 Kueleza jinsi ya kuwakinga watoto waliozaliwa kabla ya kuhitimu muhula au wakiwa na uzani wa chini kutokana ha hipothemia, ukijumuisha kumshauri mama na familia yake kuhusu Utunzaji wa Mama wa aina ya Kangaruu. (Swali la Kujitathmini 8.4 )
Watoto waliozaliwa kabla ya kuhitimu muhula au wakiwa na uzani wa chini wako katika hatari zaidi ya kufa kutokana na hipothemia, maambukizi, matatizo ya kupumua na kutokomaa kwa viungo muhimu. Kinachofuatia ni kuwa watoto hawa hushindwa kukabiliana na maisha nje ya uterasi. Sababu kuu zinazowafanya wahitaji utunzaji maalum zimeandikwa kwa muhtasari katika Jedwali 8.1
Mfano mmoja wa sababu inayowafanya watoto waliozaliwa kabla ya kuhitimu muhula au wakiwa na uzani wa chini kuhitaji utunzaji maalum ni kuwa wana uwezo mdogo kupindukia wa kukabiliana na maradhi ambukizi. Hii ni kwa sababu kingamwili yao haijakomaa vyema. Kwa hivyo, kando na linalohitajika kwa watoto wote, wewe na mama mnafaa kuwa waangalifu kuhusu usafi na hatua za kuzuia maambukizi (kama ilivyoelezwa katika Kipindi cha 6). Yeyote anayemshika mtoto anafaa kwanza anawe mikono vyema kabisa, kisha amshike kwa uangalifu. Ngozi ya mtoto aliyezaliwa kabla ya kuhitimu muhula au akiwa na uzani wa chini inaweza kuchibuka kwa urahisi, hivyo kusababisha maambukizi kuingilia mle.
Jinsi mtoto mzawa alivyo na uzani wa chini na umri mdogo ndivyo alivyo katika hatari kuu ya kukumbwa na matatizo, na hata kufa, na ndivyo anavyohitaji utunzaji maalum zaidi. Utunzaji anaohitaji unafaa kuzingatia uainishaji wa watoto waliozaliwa kabla ya wakati na wakiwa wadogo sana kama ilivyoelezwa hapa chini.
Kwa kuzingatia uzani wa wakati wa kuzaliwa, watoto wengi huzaliwa wakiwa na uzani wa chini au uzani wa chini sana, kama ilivyoainishwa hapa chini:
Uzani wa chini wa wakati wa kuzaliwa Watoto wanaozaliwa wakiwa na uzani wa gramu 1,500-2,499. Watoto hawa wanaweza kuhudumiwa vyema nyumbani kwa kuzingatia utunzaji na usaidizi zaidi.
Uzani wa chini sana wa wakati wa kuzaliwa Watoto wanaozaliwa wakiwa na uzani wa chini ya gramu 1,500. Tatizo lililo hatari kwa usalama wa watoto wadogo kiasi hiki ni kuwa hawawezi kunyonya, kumeza na kupumua kwa wakati mmoja. Kwa hivyo, watoto hawa huhitaji uangalifu maalum ili kuwalisha kwa njia ifaayo na salama. Watoto hawa pia wanakumbwa na ugumu wa kudhibiti kiwangojoto cha mwili, hivyo wako katika hatari zaidi ya kuambukizwa hipothemia. Watoto hawa huhitaji usaidizi wa kimaisha wa hali ya juu, hivyo wanafaa kupewa rufaa ya dharura hadi katika hospitali iliyo na vifaa maalum vya kuwatunza watoto walio wadogo kupindukia. Hata hivyo, kwa sasa, inawezekana kuwa vifaa kama hivi havipatikani katika familia zinazoishi baadhi ya sehemu za mashinani mwa Afrika.
Mtoto aliyezaliwa kabla ya kuhitimu muhula ni aliyezaliwa kabla ya wiki 37 za ujauzito kuisha. Kwa kuzingatia umri wa ujauzito, watoto waliozaliwa kabla ya kuhitimu muhula wameainishwa zaidi kama ifuatavyo:
Mtoto aliyezaliwa kabla ya kuhitimu muhula: Watoto waliozaliwa katika umri wa ujauzito wa wiki 32 - 36, kama ilivyokokotolewa kutokana na tarehe ya mwisho ya kipindi cha hedhi ya mama. Watoto hawa wanaweza kuhudumiwa vyema nyumbani kwa kuzingatia utunzaji na usaidizi zaidi. Utajifunza kuhusu haya baadaye katika Kipindi hiki.
Mtoto aliyezaliwa siku nyingi kabla ya kuhitimu muhula: Watoto waliozaliwa katika umri wa ujauzito wa wiki 28-31, kama ilivyokokotolewa kutokana na tarehe ya mwisho ya kipindi cha hedhi ya mama. Watoto hawa wana matatizo ya kula na kudhibiti kiwangojoto cha mwili wao kama watoto waliozaliwa kabla ya kuhitimu muhula, na kwa sababu sawa na zao. Ikiwezekana, wanafaa kupewa rufaa mara moja ili kupewa utunzaji maalum hospitalini.
Jedwali 8.1 inaainisha kwa muhtasari yale ambayo tumeeleza, pamoja na hatua unazo hitaji kuchukua.
Uzani wa wakati wa kuzaliwa na umri wa ujauzito | Uainishaji | Hatua |
---|---|---|
Uzani wa chini ya gramu 1,500. | Uzani wa chini sana wa wakati wa kuzaliwa | Mpe rufaa ya DHARURA hadi hospitalini, na uhakikishe amepashwa joto wakati wa kusafiri |
Umri wa ujauzito wa chini ya wiki 32 | Mtoto aliyezaliwa siku nyingi kabla ya kuhitimu muhula: | Hakikisha mtoto huyu amepashwa joto na umpe rufaa mara moja. |
Uzani wa gramu 1,500 - 2,500. | Uzani wa chini wa wakati wa kuzaliwa | Iwapo hakuna tatizo lingine, mshauri mama kuhusu kunyonyesha mwafaka, kuzuia maambukizi na kumpasha mtoto joto. |
Umri wa ujauzito wa wiki 32- 36 | Mtoto aliyezaliwa kabla ya kuhitimu muhula | Ni kama ilivyoelezwa kuhusu mtoto aliyezaliwa na uzani wa chini wa wakati wa kuzaliwa |
Uzani ulio sawa na au zaidi ya gramu 2,500 na umri wa ujauzito ulio sawa na au zaidi ya wiki 37 | Uzani wa kawaida na kipindi cha kuzaliwa kilichokamilika | Ni kama ilivyoelezwa kuhusu mtoto aliyezaliwa kabla ya kuhitimu muhula na akiwa na uzani wa chini wa wakati wa kuzaliwa. |
Maziwa ya matiti yanayotolewa na mama wa mtoto aliyezaliwa kabla ya kuhitimu muhula yana virutubishi zaidi ya yale yanayotolewa na mama aliyezaa katika kipindi cha kawaida. Kwa hivyo, maziwa ya mama aliyezaa kabla ya kuhitimu muhula au aliyezaa mtoto mwenye uzani wa chini ndiyo bora. Hivyo basi, hayafai kutupwa kwa sababu hakuna maziwa mengine yanayoweza kuchukua nafasi yake.
Katika wiki ya kwanza ya maisha ya mtoto, mama anahitaji usaidizi wako na wa familia yake. Hii ni ili kumhimiza aanze kumnyonyesha mtoto bila kumpa vyakula vingine na kuendelea kunyonyesha hadi mtoto wake aliye mdogo kupindukia aweze kunyonya bila tatizo. Watoto wanaozaliwa katika wiki ya 34 - 36 ya ujauzito wanaweza kunyonya vyema, lakini wale waliozaliwa siku nyingi kabla ya kuhitimu muhula wanaweza kukumbwa na tatizo la kunyonya. Kumnyonyesha mtoto aliyezaliwa mapema sana kabla ya kuhitimu muhulanhuwa changamoto. Mtoto huyu anafaa kunyonya kila baada ya saa 2, ikiwa ni pamoja na usiku.
Iwapo watoto waliozaliwa kabla ya wiki 34 hawawezi kunyonya vyema, wanaweza kupewa maziwa yaliyokamuliwa, kwa kutumia kikombe safi kabisa. (Tutaeleza jinsi ya kufanya hivi katika kifungu kijacho.) Watoto wadogo kwa kimo au waliozaliwa kabla ya kuhitimu muhula ambao wanaweza kunyonya pia wanaweza kuhitaji kupewa maziwa kwa kikombe ili kuhakikisha kuwa wanapata lishe la kutosha. Watoto wote wanaopewa maziwa kwa kikombe wanafaa kupewa takriban ml/kilo 60 kwa siku (yaani mililita 60 kwa kila kilo ya uzani wa mtoto kila siku). Kiwango hiki kinafaa kuongezwa kwa ml/kilo 20 jinsi mtoto anavyohitaji kulishwa zaidi.
Watoto waliozaliwa baada ya wiki 32 za ujauzito huenda wasiweze kunyonya hata kidogo, hivyo wanahitaji kuanzishiwa kupewa vinywaji vinavyotiwa kwa mipira. Hii ni sababu mojawapo wa zinazosababisha mtoto aliyezaliwa kabla ya wiki 32 za ujauzito anafaa kupelekwa rufaa hadi katika kituo cha afya mara moja.
Kamulia matone machache ya maziwa midomoni mwake ili kumsaidia kuanza kunyonya. Ili mtoto anyonye kwa mafunda makubwa, mpe titi lote, wala sio chuchu tu (Mchoro 8.1). Mpumzishe kwa kifupi anaponyonya. Kunyonya huwa jambo gumu kwa mtoto aliyezaliwa kabla ya kuhitimu muhula au aliye mdogo kupindukia.
Iwapo mtoto atakohoa, kutapika au kutema maziwa anapoanza kunyonya, huenda maziwa yanachuruza kwa kasi sana hivi kwamba hawezi kuyadhibiti. Mfunze mama kumwondolea mtoto titi iwapo jambo hili litafanyika. Mshikilie mtoto ukimuegeza kifuani mwa mama hadi aanze kupumua vyema tena, kisha umpe titi tena baada ya funda la kwanza la maziwa kupita.
Iwapo mtoto aliyezaliwa kabla ya kuhitimu muhula hana nguvu za kunyonya kwa muda mrefu, nfunze mama jinsi ya kukamua maziwa yake kisha amnyweshe mtoto kwa kikombe.
Inaweza kumchukua mama dakika 20-30 kukamua maziwa ya titi, au hata muda zaidi mwanzoni, lakini mama huongeza kasi ya kukamua pindi anavyopata uzoefu. Kwanza mshauri mama anawe mikono na kuosha matiti kwa sabuni na maji, kisha aikaushe kwa taulo taulo safi kabisa. Kiandae kikombe safi kilichochemshwa au chupa iliyo na mdomo mkubwa. Iwapo hawezi kuchemsha kikombe chote, kitie maji yanayochemka na uyaache mle hadi muda mchache kabla ya kutia maziwa. Kisha yamwage yale maji. Maziwa hukingwa dhidi ya bakteria kwa kufanya hivi.
Mama anafaa kuketi vyema kisha aegemee kikombe. Mwonyeshe jinsi ya kushika titi kwa ‘mshiko wa C’ (mkono wake ukichukua umbo la C kubwa; Kielelezo 8.2a). Finya nyuma kidole gumba na vidole vingine kuelekea kifuani (Kielelezo 8.1b), kisha ukizungushe kidole gumba kwenda mbele kana kwamba unatolesha alama za kidole. Hii ni ili kuyatoa maziwa kutoka sehemu zote za titi. Kamua titi moja kwa angalau dakika 3 - 4 hadi maziwa yapungue, kisha ukamue hilo lingine. Kuwaza kuhusu mtoto wake anapokamua kunaweza kufanya maziwa yachuruze kwa urahisi zaidi.
Maziwa yaliyokamuliwa kisha yakawa baridi au yaliyowekwa kwa saa 6 yanafaa kutupwa
Maziwa ya titi yanaweza kuhifadhiwa katika kiwango joto cha chumbani kwa saa 6 iwapo chumba hicho hakina joto jingi, na maziwa yamehifadhiwa ndani ya kifaa kilichotakaswa. Hata hivyo, maziwa haya yanaweza kuhifadhiwa kwa muda mrefu zaidi ndani ya friji, iwapo mama anayo. Popote yalipohifadhiwa, maziwa yanafaa kupashwa joto hadi kiwango cha joto la mwili kabla ya kumpa mtoto. Kitie ndani ya bakuli yenye maji moto kifaa kilicho na maziwa yaliyohifadhiwa ili kuyapasha joto. Usichemshe maziwa ya matiti ya mama! Virutubishi na antibodi za maziwa ya mama huharibiwa yanapochemshwa.
Mwonyeshe mama na watu wengine wa familia jinsi ya kumshika mtoto kwa karibu huku wakiwa wameketi wima. Shikilia kwenye mdomo wa chini wa mtoto kijikombe safi sana cha maziwa ya mama yaliyokamuliwa. Mtoto anapoamka na kufungua kinywa, shikilia kikombe midomoni mwake ukimwacha anywe kwa utaratibu. Mpe mtoto wakati wa kumeza na kupumzika kila baada ya kupiga funda. Mtoto anapokunywa vya kutosha na kukataa kunywa zaidi, muweke begani kisha umfanye apige mbweu kwa kumsugua mgongoni taratibu ili kuitoa hewa ambayo huenda aliimeza pamoja na maziwa.
Je, ni vidokezo na mitindo gani ya kunyonyesha unayofaa kumweleza au kumfunza mama aliyezaa kabla ya kuhitimu muhula?
Unafaa kumwarifu kuhusu:
Mwisho wa jibu
Watoto hawa hukumbwa na ugumu wa kudhibiti kiwangojoto cha mwili. Watoto hawa hupoteza jotomwili kwa urahisi, hivyo wapo katika hatari ya kupata hipothemia katika hali hii. Kila mara, fuata kanuni ya ’warm chain’ unapomhudumia mtoto yeyote, bila kuzingatia uzani au umri wake, kama ulivyojifunza katika Kipindi cha 7. Hata hivyo, watoto waliozaliwa muda mrefu kabla ya kuhitimu muhula na walio wadogo sana wanafaa kupewa huduma maalaum ifuatavyo:
Ni jabo gani unalofaa kuzingatia ili kuhakikisha kuwa mtoto amepashwa joto?
Unakumbuka kama tulivyo jifunza katika Kipindi cha 7 kuwa ni muhimu kumkinga mtoto kutokana na baridi - hivyo basi, hakikisha kuwa milango na madirisha yote yamefungwa.
Mwisho wa jibu
Utunzaji wa aina ya Kangaruu wa Mama kwa Mtoto (UKM) ni njia ya utunzaji iliyopewa jina kwa kurejelea jinsi kangaruu wanavyowatunza ndama wao. Njia hii imetambulika kuwa bora sana katika kuwatunza watoto waliozaliwa kabla ya kuhitimu muhula na waliozaliwa wakiwa na uzani wa chini. Njia hii huhusisha kumshika mtoto huku mwili wake ukiguzana na wa mama mchana na usiku. Mtu mwingine anaweza kuchukua nafasi ya mama iwapo hawezi kumshika namna hii wakati wote.
Utafiti unaonyesha kuwa njia ya UKM inapotumika, husaidia kudhibiti kima cha mdundo wa moyo na kupumua kwa watoto waliozaliwa kabla ya kuhitimu muhula na waliozaliwa wakiwa na uzani wa chini. Njia hii pia husaidia kupunguza maambukizi na kumwezesha mtoto kuongeza uzani ifaavyo. Njia hii humsaidia mama kwa kuzidisha utoleshaji wa maziwa, na pia kufanikisha kunyonyesha bila kutumia vyakula vya ziada.
Baada ya ya kumwelezea mama kuhusu utaratibu wa UKM (ama mhudumu mwingine kufanya hivyo) unafaa kufuata hatua zilizopeanwa katika jedwali 8.1
Mhakikishie mama kuwa mtoto anaweza kupokea utunzaji muhimu wa kila siku, ikiwa ni pamoja na kunyonyesha, wakati wa UKM. Mtoto huondolewa kutoka hali ya kuguzana na mama wakati wa kumbadilisha nepi, usafi wa jumla wa kimwili, utunzaji wa kitovu na uchunguzi wakati wa ziara. Mama anahitaji kulala kitandani siku 3 - 5 tu za kwanza baada ya kuzaa. Hali ya mtoto inapokuwa dhabiti, mama anaweza kutembea na kufanya kazi zake za kawaida huku mtoto akiwa katika UKM, na wanaweza kulala pamoja usiku wakifuata njia ya UKM.
Katika kila ziara ya baada ya kuzaa unafaa:
Njia ya UKM inaweza kuonekana kama njia isiyo ya kawaida ya kumtunza mtoto. Kwa hivyo, ni muhimu kuchukua muda unapomshauri mama, baba na familia kuhusuvipengele vya njia hii na manufaa yake. Mama (na familia) wanapaswa kushawishika na kukubali kutumia njia hii kwa siku nyingi mfululizo. Baba na watu wengine wa familia pia wanapaswa kuwa tayari kutoa usaidizi wa kimwili na kihisia kwa mama anapotumia njia ya UKM
Umuhimu wa UKM ni nini?
Kunyonyesha: UKM huimarisha kima cha unyonyeshaji na muda wa kunyonyesha.
Kwa kweli inaweza kuwa vigumu kwa kina mama wote kutumia UKM. Kwa hivyo, ni sharti uhakikishe kuwa mama hana matatizo au maradhi yoyote yanayoashiria kuwa anakosa nguvu za kutumia njia hii bila kusaidiwa. Ikiwa anakumbwa na matatizo haya, unapaswa kubaini kama baba au jamaa yeyote wa familia anaweza kushirikiana na mama kutoa utunzaji huu au kumtunza mtoto kwa njia hii wakati wote iwapo mama anaugua. Hatimaye, kina mama ambao wameweza kutoa utunzaji huu kikamilifu wana ujasiri mwingi mbali na kuridhika kuwa wanaweza kuwafanyia jambo spesheli watoto wao.
Ikiwa mama na mtoto wanaridhika kutumia njia hii, inafaa kueendelezwa kwa kipindi kirefu kama inavyowezekana au mpaka mtoto ahitimu muhula wa kuzaliwa (wiki 40) ama mpaka mtoto apate uzani wa gramu 2,500. Iwapo mtoto ana uzani unaozidi gramu 1 800 na kiwango chake cha jotomwili ni dhabiti, hana matatizo yoyote ya kupumua na ananyonya vizuri, anaweza kulishwa kupitia UKM kabla ya wiki 40. Mtoto anapotosheka na UKM humdhiirishia mama yake kupitia, kugaagaa, kuchezacheza, kuondoa miguu na mikono yake kutoka kwenye nguo zilizomfunika na kulia hadi afunuliwe.
Hatimaye, ukifuata maagizo haya na kuwasaidia familia zako kutunza watoto wao waliozaliwa kabla ya kuhitimu muhula au waliozaliwa wakiwa na uzani wa chini kama ilivyoelezwa katika Kipindi hiki, ni hakika kuwa utaokoa maisha ya watoto wengi wachanga. Kunalo jambo muhimu kuliko hili?
Katika Kipindi cha 8 umejifunza kuwa:
Kwa vile sasa umekamilisha Kipindi hiki, jibu maswali yafuatayo ili kutathmini jinsi ulivyojifunza.
Ni viashirio vipi muhimu vinavyoonyeshwa na watoto waliozaliwa kabla ya kuhitimu muhula na wale waliozaliwa wakiwa na uzani wa chini ambavyo hudhiirisha kuwa wanahitaji utunzaji spesheli?
Vidokezo vikuu vinavyoashiria kuwa watoto waliozaliwa kabla ya kuhitimu muhula na wale waliozaliwa wakiwa na uzani wa chini huhitaji utunzaji spesheli ni:
Mwisho ya jibu
Jaza mapengo katika Jedwali 8.2
Uzani wa kuzaliwa na umri wa ujauzito | Uainishaji | Hatua za kuchukuliwa |
---|---|---|
Uzani wa chini ya gramu 1,500 | ||
Walizaliwa wakiwa na umri wa ujauzito wa chini mno | ||
Umri wa ujauzito wiki 32-36 | Ikiwa hukuna tatizo jingine, mshauri kuhusu kunyonyesha kikamilifu, kuzuia maambukizi na kuhakikisha mtoto amepata joto la kutosha. | |
Uzani wa kawaida na muhula yote ya ujauzito |
Rejelea Kisanduku 8.1 katika Kitengo cha 8.2.1 na ulinganishe na yale uliyoandika katika jedwali 8.2
Mwisho wa jibu
Ulimzuru mama aliye na mtoto aliyezaliwa akiwa na uzani wa gramu 2,000 kwa mara ya kwanza saa 12 baada ya kuzaa. Yamkini ana uwezo wa kunyonya, ingawa sio kwa muda mrefu, na mama yake ana wasi wasi kuwa hawezi kupata maziwa ya kutosha. Je utamshauri vipi?
Kwa kuwa ana uzani wa gramu 2,000 mtoto huyu ana uzani wa chini, lakini anaonekana kuwa na uwezo wa kunyonya. Hata hivyo, ikiwa mama yake anafikiria kuwa mtoto hapati maziwa ya kutosha kwa sababau anachoka haraka akinyonya, unapaswa kumpendekezea ampatie lishe ya ziada ya maziwa ya mama ya kujikamua na kumnywesha kwa kikombe. Kwanza unapaswa umfafanulie jinsi ya kujikamua na namna ya kuhifadhi maziwa (rejelea Kitengo cha 8.3.3 kama huwezi kukumbuka), kisha umwonyeshe jinsi ya kumnywesha mtoto kwa kikombe.
Mwisho wa jibu
Mwisho wa jibu