8. Utunzaji Maalum kwa Watoto Waliozaliwa kabla ya Kuhitimu Muhula na Waliozaliwa wakiwa na Uzani wa Chini

Kipindi cha 8 Utunzaji Maalum kwa Watoto Waliozaliwa Kabla ya Kuhitimu Muhula na Waliozaliwa wakiwa na Uzani wa Chini

Utangulizi

Katika Kipindi hiki, utajifunza kuhusu huduma maalum na ya ziada inayohitajika na watoto waliozaliwa kabla ya kuhitimu muhula na waliozaliwa wakiwa na uzani wa chini. Tutaleleza kwa kina sababu za watoto hawa kuhitaji utunzaji maalum, na jinsi unavyoweza kuwahudumia. Pia tutaeleza jinsi ya kuwashauri kina mama na watu wengine wa familia kuhusu kuwahudumia watoto hawa. Lengo letu ni kudhibiti matatatizo yanayohusiana na kuwalisha watoto waliozaliwa kabla ya kuhitimu muhula na waliozaliwa wakiwa na uzani wa chini, na jinsi ya kuwapasha joto. Utajifunza hasa kuhusu njia mwafaka na inayochukuliwa kuwa ya kisasa ya kudhibiti jotomwili la mtoto mkembe au mwenye kimo kidogo sana. Njia hii hujulikana kama Utunzaji wa Mama wa aina ya Kangaruu.

Malengo ya Somo la Kipindi cha 8