Muhtasari wa Kipindi cha 1

Katika Kipindi cha 1 umejifunza kuwa:

  1. Uwiano wa vifo vya kina mama kabla, katika na muda mfupi baada ya kuzaa na kiwango cha vifo vya watoto wachanga barani Africa viko miongoni mwa viwango vya juu sana ulimwenguni
  2. Takribani asilimia 45-50 ya kina mama na watoto wachanga hufariki katika saa 24 za kwanza baada ya uzazi na asilimia 65-75 ya vifo vya kina mama na vya watoto wachanga hutokea katika juma la kwanza.
  3. Utunzaji bora baada ya kuzaa katika saa sita za kwanza na baada ya siku mbili, sita na majuma sita unaweza kupunguza vifo vya kina mama kabla, katika na muda mfupi baada ya kuzaa na vya watoto wachanga kwa kiwango kikubwa.
  4. Visababishi vya mara kwa mara vya vifo vya kina mama muda mfupi baada ya kuzaa ni kutokwa na damu, eklampsia, maambukizi na kupasuka kwa uterasi.
  5. Visababishi vikuu vya vifo vya watoto wachanga ni maambukizi, asfiksia ya kuzaliwa, kuzaliwa kabla ya muda wa ujauzito kuisha na kuzaliwa na uzito wa chini
  6. Kipindi baada ya kuzaa ni wakati wa marekebisho ya haraka ya kifiziolojia kwa mama kurudi katika hali ya kutokuwa na ujauzito na kwa mtoto mchanga anayezoea maisha nje ya uterasi.
  7. Dalili za hatari kwa mama katika kipindi cha baada ya kuzaa ni uterasi kutopungua sawasawa, kutokwa na damu ukeni na mshtuko.
  8. Dalili za hatari kwa mtoto mchanga ni umanjano, ugumu katika kupumua, kiwango juu cha joto mwilini na dalili zingine za maambukizi, hipothemia, kutapika mara kwa mara na kutokwa na damu kutoka kwa kitovu au mkundu.
  9. Kabla ya kuanzisha huduma za utunzaji wa baada ya kuzaa, unapaswa kuendesha vikao vya uhamasishaji ili kuhakikisha kushiriki kikamilifu kwa jamii. Wahusishe viongozi wa jamii, wakunga na madaktari wa kienyeji. Pia zuru nyumba kwa nyumba ili kuwafundisha wazazi na watunzaji na usambaze vifaa vya habari, elimu na mawasiliano.

1.7 Kukagua wasifu wa jamii

Maswali ya kujitathmini kwa Kipindi cha 1