6. Uchunguzi wa Kidesturi wa Watoto Wachanga ili Kubaini Hali Hatari

Kipindi cha 6 Uchunguzi wa Kidesturi wa Watoto Wachanga ili Kubaini Hali Hatari

Utangulizi

Katika Kipindi hiki, tutarejelea dalili hatari za kijumla zinazoonyesha kuwa mtoto mchanga yuko hatarini, kama zilivyoorodheshwa kwa kifupi katika Kipindi cha 1. Sasa tutalenga kwa kina zaidi uchunguzi na uainishaji wa hali hizi hatari. Pia tutazungumzia hatua unazohitaji kuchukua ili kuzuia na kutibu matatizo ya mtoto mchanga yanayotokea mara nyingi. Tutalenga maambukizi ya mfumo wa pumzi, macho na kitovu, na pia dalili hatari kama vile umanjano na pepopunda. Kumhusisha mama katika utaratibu huu ni sehemu muhimu ya utunzaji wa baada ya kuzaa. Mama anaweza kuokoa maisha ya mtoto wake kwa kutia juhudi na kuwa tayari kutafuta msaada wako anapotilia shaka hali ya mtoto.

Malengo ya Somo la Kipindi cha 6