Maswali ya kujitathmini kwa Kipindi cha 1

Kwa kuwa umekamilisha Kipindi hiki cha somo, unaweza kutathmini ni kwa kiwango kipi umeweza kuyatimiza malengo ya somo hili kwa kujibu maswali yafuatayo. Andika majibu yako katika shajara yako kisha ujadiliane na mkufunzi wako katika mkutano saidizi wa masomo utakaofuata. Unaweza kulinganisha majibu yako na muhtasari juu ya maswali ya kujitathmini yaliyo mwishoni mwa moduli hii.

Swali la kujitathmini 1.1 (linatathmini Malengo ya Somo la 1.1)

Ifuatayo ni orodha ya maneno muhimu yaliyotumiwa katika Kipindi hiki cha somo. Kila neno na ufafanuzi. Ni ufafanuzi upi hapa chini ulio (i) sahihi kabisa (ii)sahihi kwa kiasi fulani na (iii) si sahihi. Andika sentensi fupi kwa kila mmoja wa ufafanuzi ulio sahihi kwa kiasi fulani au usio sahihi kwa kulitumia neno hilo kwa usahihi.

  • a.Mtoto mchanga - ni mtoto aliyezaliwa
  • b.Utunzaji baada ya kuzaa - utunzaji anaopewa mtoto mara tu baada ya kuzaliwa
  • c.Kiwango cha vifo vya watoto wachanga - idadi ya watoto wanaofariki katika siku 28 za kwanza za maisha yao kwa kila 1,000 wanaozaliwa wakiwa hai.
  • d.Kipindi mwanzoni mwa uchanga - kipindi punde tu baada ya kuzaliwa hadi mwisho wa siku saba za kwanza za maisha.
  • e.Uwiano wa vifo vya kina mama kabla, katika na muda mfupi baada ya kuzaa - idadi ya kina mama wanaofariki kutokana na kuzaa.
  • f.Kiwango cha vifo vya watoto mwanzoni mwa uchanga - idadi ya watoto wanaofariki punde tu baada ya kuzaliwa.
  • g.Kipindi cha uchanga - kipindi tangu kuzaliwa hadi siku 28 baada ya kuzaliwa
  • h.Mbadilishano wa gesi - hali wanayojishughulisha nayo raia wa Marekani waendapo kwenye kituo cha petroli.
  • i.Umanjano kwa watoto wachanga - hali inayoweza kutokea ini la mtoto mchanga lisipoweza kuzimua sumu kikamilifu katika damu.

Answer

  • a.Sahihi: mtoto mchanga ni mtoto mchanga.
  • b.Sahihi kwa kiasi fulani: ni utunzaji unaotolewa kwa mtoto na mama yake mara tu baada ya kuzaa na kwa muda wa majuma sita ya kwanza ya maisha.
  • c.Sahihi: kiwango cha vifo vya watoto wachanga ni vifo vya watoto wachanga katika siku 28 za kwanza za maisha kwa kila watoto 1,000 wanaozaliwa wakiwa hai.
  • d.Sahihi : mwanzoni mwa kipindi cha uchanga ni tangu kuzaliwa hadi siku 7 za kwanza.
  • e.Sahihi kwa kiasi fulani: ni idadi ya kina mama wanaofariki wakati wa kuzaa na kutokana na matatizo yatokeayo mara tu baada ya kuzaa. Barani Afrika, kiwango cha vifo vya kina mama kabla, katika na muda mfupi baada ya kuzaa kiko juu sana kikiwa na takribani vifo 673 kwa kila watoto 100,000 wanaozaliwa wakiwa hai. Kumbuka kuwa kiwango cha vifo vya watoto wachanga hukadiriwa kwa kila watoto 1,000 wanaozaliwa wakiwa hai ilhali Kiwango cha vifo vya kina mama kabla, katika na muda mfupi baada ya kuzaa hukadiriwa kwa kila watoto 100,000 wanozaliwa wakiwa hai.
  • f.Si sahihi: ni idadi ya vifo katika juma la kwanza la maisha kwa kila watoto 1,000 wanozaliwa wakiwa hai. Hii pia iko juu sana barani Afrika ambapo ni takribani vifo 39 kwa kila watoto 1,000 wanaozaliwa wakiwa hai.
  • g.Sahihi: kipindi cha uchanga ni tangu kuzaliwa hadi siku ya 28.
  • h.Si sahihi: ni mchakato ambapo mapafu yetu hufyonza oksijeni na kutoa monoksidi ya kaboni. Mchakato huu hutendeka tangu kuzaliwa.
  • i.Sahihi: Kwa undani zaidi, kinachotendeka ni kuwa ini hukosa kuitoa protini ya bilirubini ambayo hutolewa katika mchakato wa kuharibu seli zee nyekundu za damu. Dalili ya umanjano kwa mtoto mchanga (yaani malimbikizo ya bilirubini) ni ambapo ngozi huanza kuwa na rangi ya manjano hasa kwa viganja na nyayo za mtoto.

Mwisho wa jibu

Swali la kujitathmini 1.2 (linatathmini malengo ya Somo la 1.2 na 1.5)

Dhania kuwa unajaribu kumshawishi Waziri wa Fedha wa bara Afrika kuweka pesa zaidi kwa utunzaji wa kiafya baada ya kuzaa na anataka ushahidi kuhusu sababu zake kufanya hivyo. Andika barua fupi ukieleza kwa muhtasari hoja kuu utakazosisitiza.

Answer

Kuna hoja nyingi unazoweza kumtolea Waziri huyo wa Fedha. Zifuatazo ni baadhi ya zile muhimu:

  • Afrika ina baadhi ya viwango vya juu sana vya vifo vya kina mama kabla, katika na muda mfupi baada ya kuzaa na vya watoto mwanzoni mwa kipindi cha uchanga duniani (unaweza kutaja tarakimu halisi).
  • Kipindi cha hatari kubwa (yaani, mara tu baada ya kuzaa na katika siku 7 za kwanza za maisha na hadi mpaka siku 28) pia ni wakati ambapo kuna kiwango cha chini cha matumizi ya huduma za utunzaji wa afya ya mama na mtoto katika Afrika.
  • Utunzaji bora zaidi wa baada ya kuzaa ni lazima utendeke katika saa chache za kwanza au utakuwa umechelewa sana. Utatuzi mwafaka katika kipindi cha baada ya kuzaa una uwezo wa kupunguza vifo vya watoto wachanga kwa asilimia 10-27. Hii itaisaidia Afrika kutimiza Malengo ya Millenia ya Maendeleo ya kupunguza vifo vya kina mama kabla, katika na muda mfupi baada ya kuzaa na vya watoto.
  • Tayari tunajua visababishi vikuu vya vifo katika kipindi cha baada ya kuzaa (unaweza kumpa orodha hii) na tunajua vyema cha kufanya kuhusu haya na hili hasa ni suala la kuwepo kwa mhudumu wa afya aliyehitimu ili kutekeleza hayo.
  • Unaweza pia kusisitiza kuwa ili uweze kufaa zaidi, utunzaji wa baada ya kuzaa huhitaji pia kuhusisha jamii (kuwafanya wahusike katika mchakato wote kuwezesha kubadilika kwa mienendo duni ya kitamaduni na mengineyo) kisha umuelezee jinsi utakavyokuwa ukiyatekeleza haya, kwa mfano kuzungumza na watu mashuhuri na utambulishe msaada wa wakunga wa kienyeji katika jamii.

Mwisho wa jibu

Swali la kujitathmini 1.3 (linatathmini malengo ya Somo la1.3 na 1.4)

Umefanya kazi nzuri kumshawishi Waziri wa Fedha. Hata hivyo, amemtaka Waziri wa Afya achunguze na kuthibitisha ikiwa kweli unafahamu unachokizungumzia. Anakutaka uorodheshe dalili kuu za matatizo yanayoweza kutokea unazopaswa kuchunguza kwa mama aliyezaa na dalili kuu za hatari kwa mtoto mchanga. Je, utaandika nini katika orodha yako?

Answer

Dalili za hatari kwa mama aliyezaa:

Dalili kuu za kuchunguza ni ukosefu wa maji mwilini, uterasi isiyopungua ipaswavyo, kutokwa na damu upya, kupungua kwa shinikizo la damu na kupanda kwa mpwito wa ateri. Dalili za hatari za muda mrefu unazopaswa kujua ni kuganda kwa damu na dipresheni.

Dalili za hatari kwa mtoto mchanga

Unayopaswa kuchunguza kwanza ni: je, mtoto ananyonya vizuri, rangi ya ngozi ni ya kawaida au ni ya manjano, kuna joto la juu mwilini, mtoto ni baridi au vuguvugu sana akiguswa, kupumua ni kwa kawaida, kuna kutokwa na damu, vigubiko vya macho ya mtoto ni vyekundu au vimevimba? Pia utachunguza ikiwa mtoto alizaliwa kabla ya muda wa ujauzito kuisha ili kutambua ikiwa yuko katika hatari zaidi ya kupata matatizo mengine. Huenda ulipata mengi ya haya. Ikiwa haukupata mengi ya haya au hauwezi kukumbuka yanayoashiria, soma tena sehemu 1.5.2 ‘kumtathmini mtoto mchanga’

Mwisho wa jibu.

Muhtasari wa Kipindi cha 1