Malengo ya Somo la Kipindi cha 1

Baada ya kusoma katika Kipindi hiki, unapaswa kuwa na uwezo wa:

1.1 Kufafanua na kutumia kwa usahihi maneno yote muhimu yaliyochapishwa kwa herufi nzito. (Swali la kujitathmini 1.1)

1.2 Kueleza umuhimu wa utunzaji baada ya kuzaa kwa kuzingatia wakati ambapo kina mama wengi na watoto wachanga hufariki na visababishi vikuu vya vifo hivi. (Swali la kujitathmini 1.2)

1.3 Kueleza kwa kifupi mabadiliko makuu ya kifiziolojia kwa mama na mtoto mchanga katika kipindi cha baada ya kuzaa. (Swali la kujitathmini 1.3)

1.4 Kueleza dalili kuu za hatari kwa mama na mtoto mchanga katika kipindi cha baada ya kuzaa. (Swali la kujitathmini 1.3)

1.5 Kueleza umuhimu wa kujihusisha kwa jamii katika utunzaji wa baada ya kuzaa na kuelezea jinsi utakavyojenga ushirikiano na watu mashuhuri katika jamii hiyo. (Swali la kujitathmini 1.2)

Kipindi cha 1 Utunzaji baada ya kuzaa katika kituo cha afya na katika Jamii

1.1 Je, kwa nini utunzaji baada ya kuzaa ni muhimu?