1.1 Je, kwa nini utunzaji baada ya kuzaa ni muhimu?

Utunzaji bora baada ya kuzaa unaweza kuleta tofauti zaidi kwa afya na maisha ya kina mama na watoto wachanga mwanzoni mwa kipindi cha uchanga na siku saba za kwanza za maisha. Hata hivyo, kipindi hiki cha uchanga, tangu kuzaliwa hadi siku 28 baada ya kuzaliwa ni wakati wa kiwango cha juu cha hatari. Vifo vya watoto wachanga waliozaliwa wakiwa hai vitokeavyo katika kipindi cha siku 28 za kwanza huripotiwa na nchi zote ulimwenguni kama kiwango chavifo vya watoto wachanga kwa kila watoto 1,000 wanaozaliwa wakiwa hai. Vile vile, ripoti za vifo vya kina mama vitokanavyo na ujauzito ni vifo vya wanawake vitokanavyo na matatizo yanayohusiana na matatizo ya baada ya kuzaa na sio tu yale yanayotokea wakati wa kuzaa. Viwango hivi vyote ni viashiria muhimu vya ubora wa utunzaji baada ya kuzaa.

Kipindi baada ya kuzaa ni wakati muhimu kwa mama na mtoto wake mchanga. Hii ndiyo sababu ya kwanza ya kukufanya ulenge utunzaji zaidi na mazingatio kwa kipindi hiki. Afrika, uwiano wa vifo vitokanavyo na ujauzito ni miongoni mwa wiano za juu zaidi ulimwenguni. Kina mama 673 hufariki kwa kila watoto 100,000 wanaozaliwa wakiwa hai. Vile vile, kiwango cha vifo vya watoto mwanzoni mwa kipindi cha uchanga piakilikuwa juu sana ambapo watoto 39 walifariki katika juma la kwanza la maisha kwa kila watoto 1,000 waliozaliwa wakiwa hai. Afrika ni mojawapo ya bara ambako nusu ya jumla ya vifo vya watoto wachanga hutokea.

Kipindi hiki chenye hatari ya juu pia ndio wakati ulio na kiwango cha chini cha matumizi ya huduma za kiafya kwa kina mama na watoto barani Afrika. Hii ndiyo sababu ya pili inayokulazimu kuzingatia sana utunzaji baada ya kuzaa.

Ikiwa watoto wote wachanga watapokea utatuzi bora na kwa gharama nafuu katika kipindi cha baada ya kuzaa, imekadiriwa kuwa vifo vya watoto wachanga vinaweza kupunguzwa kwa asilimia 10-27. Hii ina maana kuwa, kiwango cha juu cha matumizi ya utunzaji wa baada ya kuzaa kinaweza kuokoa maisha ya watoto wachanga 60,000 kila mwaka barani Afrika na kuisaidia nchi hiyo kutimiza Lengo la Milenia la Maendeleo la kupunguza vifo vya watoto walio chini ya umri wa miaka mitano kwa theluthi mbili kufikia mwaka wa 2015.

Kwa kweli, utunzaji wa baada ya kuzaa ni bora ukitolewa katika kituo cha afya. Hata hivyo, kutokana na sababu nyingi za kijamii, kiuchumi na kitamaduni kama vile umbali na gharama ya kwenda kuhudumiwa, kina mama wengi vijijini huzalia nyumbani. Kwa hivyo, njia halisi zaidi ya kutoa utunzaji baada ya kuzaa katika siku za usoni barani Afrika huenda iwe ni kwa mhudumu wa afya kama wewe kuwatembelea nyumbani.

Malengo ya Somo la Kipindi cha 1

1.2 Je, ni wakati upi ambapo kina mama na watoto wachanga hufariki katika kipindi cha baada ya kuzaa?