1.2 Je, ni wakati upi ambapo kina mama na watoto wachanga hufariki katika kipindi cha baada ya kuzaa?

Kina mama na watoto wao wachanga wamo katika hatari zaidi ya kufariki mwanzoni mwa kipindi cha uchanga, hasa saa 24 za kwanza baada ya kuzaa na katika siku saba za kwanza baada ya kuzaa (tazama Jedwali 1.1). Jinsi unavyoweza kuona katika jedwali, asilimia 45 hadi 50 ya vifo vya kina mama na watoto wachanga hutokea katika saa 24 za kwanza baada ya kuzaa. Asilimia 65 hadi 75 ya vifo vya kina mama na watoto wachanga hutokea katika muda wa juma moja baada ya kuzaa. Huu ni ushahidi unaolazimu utoaji wa utunzaji bora na kikamilifu kwa kina mama na watoto wachanga katika siku chache za kwanza baada ya kuzaa.

Jedwali 1.1 Makadirio ya vifo vya kina mama na watoto wachanga katika siku saba za kwanza baada ya kuzaa
Vifo baada ya kuzaaSaa 24 za kwanza (%)Siku saba za kwanza (%)
Vifo vya kina mama4565
Vifo vya watoto wachanga 5075

Kwa hali fulani zinazohatarisha maisha ya mama na mtoto mchanga, utunzaji bora baada ya kuzaa hutolewa katika saa na siku chache za kwanza au baadaye kwa kuchelewa. Hali hizi za kiafya zinapotambulika mapema ndivyo zinavyoweza kuthibitiwa kikamilifu; ndivyo mama na mtoto wanavyopewa rufaa ya kupata matibabu spesheli kwa haraka na ndivyo matokeo yatakavyokuwa mazuri. Nyingi za tatuzi hizi hutegemea sana wakati. Unapaswa kuzingatia haya unapotoa utunzaji kwa kina mama na watoto wao siku chache za kwanza za maisha baada ya kuzaa.

1.1 Je, kwa nini utunzaji baada ya kuzaa ni muhimu?

1.3 Je, kina mama na watoto wachanga katika kipindi cha baada ya kuzaa hufariki kutokana na nini?