1.3 Je, kina mama na watoto wachanga katika kipindi cha baada ya kuzaa hufariki kutokana na nini?

Lengo kuu la kutoa utunzaji bora baada ya kuzaa ni kuzuia vifo vya kina mama na watoto wachanga na vile vile matatizo ya muda mrefu. Unapaswa kujua visababishi vikuu vya vifo katika kipindi cha baada ya kuzaa ili uweze kutoa utunzaji bora wa baada ya kuzaa na kwa wakati ufaao pale nyumbani na katika kituo cha afya.

Kujua ni nini hasa kinachosababisha vifo vya kina mama na watoto wachanga ni muhimu kwa kutambua hatua muhimu zinazowezakutatuavisababishi vikuu vya vifo katika kipindi baada ya kuzaa. Jedwali 1.2 linaonyesha asilimia ya vifo vya kina mama na visababishi vikuu vya vifo hivi kwa wanawake barani Afrika.

Ulijifunza kuhusu anemia, matatizo yanayosababisha shinikizo la damu, na uavyaji mimba katika vikao vya18, 19 na 20 vya somo katika Moduli ya utunzaji katika ujauzito. Vizuizi na kutokwa na damu nyingi wakati wa kuzaa vilifundishwa katika Vikao vya 9 na 11 vya moduli ya utunzaji katikauchungu wa kuzaa na kuzaa.

Jedwali 1.2 Visababishi vya vifo vya kina mama vitokanavyo na ujauzito barani Afrika.
Visababishi vya vifo vya kina mamaAsilimia (%)
Kutokwa na damu nyingi baada ya kuzaa34
Maambukizi ya sehemu fulani au yaliyosambaa (Sepsisi)16
Matatizo yanayosababisha shinikizo la damu katika ujauzito (ugonjwa wa ujauzito, eklampsia)9
VIRUSI VYA UKIMWI/ UKIMWI6.2
Vizuizi katika kuzaa4
Uavyaji mimba 4
Anemia4
Visababishi vingine vya vifo  30

Jedwali 1.3 linaonyesha visababishi vya vifo vya watoto wachanga barani Afrika. Utajifunza kuhusu utunzaji maalum kwa watoto waliozaliwa kabla ya muda wa ujauzito kuisha na waliozaliwa na uzani wa chini katika Kipindi cha 8 cha somo cha Moduli hii.

Maambukizi, yakiwemo magonjwa ya kuhara na pepopunda, yameelezewa kwa undani katika Moduli juu ya magonjwa ya kuambukiza. Asifiksia ya kuzaliwa na uhaisho (urejeshaji uhai wa mtu mahututi) wa mtoto mchanga yaliangaziwa katika Kipindi cha 7 cha somo cha moduli juu ya utunzaji katika uchungu wa kuzaa na kuzaa.

Jedwali 1.3 Visababishivya vifo vya watoto wachanga barani Afrika
Visababishi vya vifo vya watoto wachanga Asilimia (%)  
Maambukizi:               47
  • Kuhara           
  • Pepopunda
  • Maambukizi mengine yakiwemo sepsisi

3

7

37

Asifiksia ya kuzaliwa 25
Kuzaliwa kabla ya muda wa ujauzito kuisha na kuzaliwa na uzani wa chini25
Ulemavu wa kuzaliwa4
Visababishi vingine vyote 7
  • Je, kwa nini ni muhimu sana uelewe visababishi vikuu vya vifo vya kina mama na watoto katika kipindi cha baada ya kuzaa?

  • Huenda ulifikiria sababu nyingi, lakini iliyo bayana zaidi ni tofauti kubwa inayoweza kuletwa na utoaji wa utunzaji bora wa baada ya kuzaa na kwa wakati ufaao kwa kiwango cha vifo vya watoto wachanga barani Afrika: kupungua kwa asilimia 10 hadi 27 ya vifo vya watoto wachanga au kuokoa maisha ya takribani watoto wachanga 60,000.

    Mwisho wa jibu

  • Fikiria kuhusu visababishi vikuu vya vifo vya kina mama na watoto wachanga. Je, ni vipi unavyotarajia kukumbana navyo unapotekeleza jukumu lako kama mhudumu wa afya nje ya hospitali?

  • Ukitumia takwimu zilizo kwenye Jedwali 1.2 na 1.3, basi huenda ulitaja kutokwa na damu nyingi baada ya kuzaa kwa kina mama, na aina fulani ya maambukizi kwa watoto na kina mama. Huenda pia ulichagua eklampsia na asifiksia ya watoto wachanga.

    Mwisho wa jibu.

1.2 Je, ni wakati upi ambapo kina mama na watoto wachanga hufariki katika kipindi cha baada ya kuzaa?

1.4 Je, kwa nini wanawake na watoto wachanga wamo katika hatari kubwa katika kipindi cha baada ya kuzaa?