1.4 Je, kwa nini wanawake na watoto wachanga wamo katika hatari kubwa katika kipindi cha baada ya kuzaa?

Saa 4-6 za kwanza baada ya kuzaa ndicho kipindi ambapo mama anaweza kuathiriwa sana na matatizo yatokanayo na kutokwa na damu nyingi. Visababishi huwa kupoteza damu nyingi kupitia katika eneo ambapo plasenta ilikuwa imejishikiza kwenye uterasi ya mama au kupasuka kwa uterasi wakati wa uchungu wa kuzaa na kuzaa. Kutokwa na damu kabla ya kuzaa pia kunaweza kuhatarisha maisha ya mtoto kwa kumkosesha oksijeni na virutubishi.

Mama pamoja na mtoto wamo katika hatari kubwa ya kukumbwa na matatizo mengine ikiwa marekebisho ya kifiziologia yanayotokea katika miili yao hayatatokea ifaavyo baada ya kuzaa. Hii inaweza kusababisha ukosefu wa utendaji kazi au ukatizaji wa usambazaji wa mahitaji muhimu ya oksijeni na virutubishi vinavyohitajika kudumisha maisha.

1.3 Je, kina mama na watoto wachanga katika kipindi cha baada ya kuzaa hufariki kutokana na nini?

1.4.1 Mabadiliko ya kifiziolojia kwa mama baada ya kuzaa