1.4.1 Mabadiliko ya kifiziolojia kwa mama baada ya kuzaa

Kuna kupoteza damu na viowevu vingine vya mwili (kwa mfano kupitia kutapika na kutokwa na jasho) kusikoweza kuepukika wakati wa uchungu wa kuzaa. Hata hivyo, wanawake wengi wanaweza kustahimili haya. Upotezaji huu wa viowevu ni kawaida kwa kiwango fulani. Aidha, wanawake wengi hubaki katika uchungu wa kuzaa kwa saa nyingi bila kula wala kunywa, jambo ambalo linaweza kuwafanya wakose maji mwilini. Wasipopewa maji mwilini kwa haraka baada ya kuzaa, wana uwezekano wa kupata matatizo ya kifiziolojia

Katika ujauzito, shughuli hubadilika katika karibu mifumo yote ya mwili wa mama, ikiwemo moyo, mapafu, kiasi cha damu na vilivyo kwenye damu, mfumo wa uzazi, matiti, mfumo wa kingamwili na homoni. Katika kipindi baada ya kuzaa, mifumo hii yote ya mwili yenye kubadilika sharti ibadilike kutoka katika hali ya ujauzito hadi hali ilivyokuwa kabla ya ujauzito. Kuna uwezekano wa hatari ya matatizo marekebisho haya yanapotendeka. Mifano ya matatizo yanayotokea sana ni maambukizi ya matiti na mivilio ndani ya vena (vibonge vya damu ndani ya vena za miguu), ambayo yameelezewa katika Kipindi cha 3 cha somo kwenye Moduli hii. Kipindi ambapo marekebisho haya ya kifiziologia hufanyika katika mwili wa mama aliyezaa huitwa puperiamu. Utajifunza kuhusu haya yote katika Kipindi cha 2 na cha 3 cha somo.

Aidha, uchungu wa kuzaa ni tukio lenye maumivu kwa wanawake wengi, hasa wale wanaozaa kwa mara ya kwanza. Wanawake pia hupata fadhaa na mhangaiko kuhusu jinsi matokeo ya uchungu wa kuzaa utakavyokuwa. Kuwa na mtoto ni furaha (Picha 1.1), lakini pia inaweza kuwa chanzo cha wasiwasi. Wanawake walio katika kipindi cha baada ya kuzaa mara nyingi hukabiliana na hali ya mfadhaiko na hivyo wanahitaji usaidizi wa kisaikolojia.

Picha 1.1 Kuwa na mtoto mwenye afya huleta furaha, jambo linaloweza kudumishwa na utunzaji bora baada ya kuzaa. (Picha: Nancy Durrell McKenna kwa Usalama wa Kina mama)

1.4 Je, kwa nini wanawake na watoto wachanga wamo katika hatari kubwa katika kipindi cha baada ya kuzaa?

1.4.2 Matatizo kwa mtoto mchanga