1.4.2 Matatizo kwa mtoto mchanga

Hatari ya maambukizi

Akiwa kwenye uterasi, mtoto huwa amelindwa vizuri na membreni za fetasi na kiowevu kizuia-bakteria cha amnioni ambamo fetasi hiyo huwa, vile vile na antibodi za mama zinazopitia kwenye plasenta na kuilinda dhidi ya maambukizi ambayo mama huyu ashakabiliana nayo. Antibodi kwenye kolostramu (maziwa ya kwanza ya mama) na maziwa komavu ya mama pamoja na vizuizi asilia kama vile ngozi ya mtoto humpa mtoto mchanga kiasi kikubwa cha kinga dhidi ya maambukizi anayopata mara tu anapozaliwa. Mfumo wa kingamwili wa mtoto huyu utachukua miezi kadhaa kabla ya kukua kikamilifu.

Hatari ya asfiksia

Mfumo wa mzunguko wa damu wa mtoto huyu mchanga ni mkumbwa na marekebisho kadhaa anapopumua kwa mara ya kwanza nje ya uterasi. Kiasi kidogo cha damu huenda kwenye mapafu mtoto akiwa ndani ya uterasi kwa sababu hapumui hewa. Mapafu ya fetasi hayawezi kutekeleza mbadilishano wa gesi (kufyonza oksijeni na kutoa dioksidi ya kaboni) unaofanyika tangu kuzaliwa na kuendelea.

  • Je, mbadilishano wa gesi hufanyika wapi kwa mtoto akiwa kwenye uterasi?

  • Oksijeni hufyonzwa katika damu ya fetasi kutoka kwa damu ya mama mifumo hii inapokaribiana katika plasenta; dioksidi ya kaboni kutoka kwa fetasi huingia katika damu ya mama na kutolewa kutoka kwa mwili wake kupitia katika pumzi yake.

    Ulijifunza kuhusu mbadilishano wa gesi kwenye plasenta katika Kipindi cha 6 cha somo kwenye moduli ya Utunzaji katika Ujauzito.

    Mwisho wa jibu

Mara tu baada ya kuzaliwa, mishipa ya damu inayopita kwenye mapafu hufunguka na kisha damu yote katika mzunguko wa mtoto iweze kupita kwenye mapafu, ambapo mbadilishano wa gesi hufanyika. Ni wakati muhimu sana kwa mtoto mchanga mapafu yanapoanza kufanya kazi. Kutopumua ni sababu ya kawaida ya asfiksia ya kuzaliwa. Pia watoto waliozaliwa kabla ya muda wa ujauzito kuisha, mara nyingi huwa na ugumu wa kupata oksijeni ya kutosha kwa sababu mapafu yao hayajakomaa kikamilifu na kwa hivyo mbadilishano wa gesi hautafanyika ifaavyo.

Utajifunza mengi kuhusu ugonjwa wa manjano kwa watoto wachanga katika Kipindi cha 6 cha na pia kwenye moduli juu ya Udhibiti Unganifu wa Maradhi ya Watoto Wachanga na ya Utotoni.

Mtoto akiwa kwenye uterasi, kemikali nyingi zenye sumu au uchafu huondolewa mwilini mwake na plasenta inayozielekeza kwenye ini ambapo huharibiwa (mchakato unaoitwa uzimuaji sumu). Baada ya kuzaliwa, ini la mtoto hulichukua jukumu hili na kuzimua sumu kwenye uchafu wa kemikali unaotengenezwa mwilini au kuingiziwa mdomoni. Mojawapo ya majukumu yanayotekelezwa na ini ni kuizimua sumu kwenye protini iitwayo bilirubini. Protini hii hutolewa kwa seli zee nyekundu za damu zinapoharibiwa. Seli nyekundu za damu huishi kwa muda mfupi tu na kuharibiwa na kisha seli nyekundu mbadala kutolewa. Ini la mtoto lisipoweza kustahimili kiwango cha seli zee nyekundu zinazofaa kuharibiwa, bilirubini hulimbika katika mwili wa mtoto na kuifanya ngozi yake iwe na umanjano. Hali hii huitwa ugonjwa wa manjano kwa watoto wachanga na ni hatari sana hasa ngozi ya viganja vya mikono na nyayo za miguu inapoonyesha umanjano.

Figo za mtoto mchanga pia huchangia pakubwa katika uondoaji wa kemikali zenye sumu zinazoondolewa mwilini kupitia kwa mkojo. Uchanga katika utendakazi wa figo pia unaweza kusababisha matatizo kwa watoto wachanga kemikali zenye sumu zinapolimbika mwilini.

  • Dhania kuwa unazungumza na mama wa mtoto mchanga kisha akuambie kuwa mtoto alizaliwa kabla ya muda wa ujauzito kuisha. Je, ni nini unachopaswa kutilia shaka na kushughulikia mara moja?

  • Kwanza chunguza ikiwa mtoto anakula vizuri. Fikiria kuhusu uchanga wa mapafu ya mtoto aliyezaliwa kabla ya muda wa ujauzito kuisha na uchunguze ikiwa mtoto huyu anaonyesha dalili zozote za matatizo ya kupumua. Pia zingatia uchanga wa figo na ini kisha uchunguze ikiwa ana dalili za ugonjwa wa manjano.

    Mwisho wa jibu

1.4.1 Mabadiliko ya kifiziolojia kwa mama baada ya kuzaa

1.5 Utakayofanya katika kipindi cha baada ya kuzaa