1.5.1 Kumkagua mama aliyezaa

Katika saa sita za kwanza, mkague mama huyo kwa dalili za hatari zifuatazo:

  • Uterasi kutopungua kikamilifu: Uterasi isiyopungua ipaswavyo ni dalili ya hatari; mpendekezee rufaa iwapo baada ya saa sita uterasi ni kubwa kuliko ukubwa wake wa kawaida baada ya wiki 20 ya ujauzito na haiwezi kuhisika kwa urahisi ukitomasa kwa sababu uterasi ni laini.
  • Kutokwa na damu mbichi ukeni: Ni kawaida kutokwa na kiowevu chenye damu (kiitwacho lokia) mwanzoni mwa kipindi cha baada ya kuzaa. Hata hivyo, kusiwe na kutoka kwa damu mbichi kunakoendelea.
  • Dalili kuu zisizothabiti au zinazoashiria mshtuko: Shinikizo la damu na mpwito wa ateri sharti viwe katika hali ya kawaida kabala ya kumuacha mama huyo. Ikiwa shinikizo lake la damu linapungua huku mpwito wa ateri ukipanda, mwanamke huyu anaweza kuwa anaelekea kuwa na mshtuko kutokana na kuvuja kwa damu ndani ya mwili. Ikiwa uterasi itabaki kuwa kubwa baada ya kuzaa na dalili kuu ziashirie mshtuko, inaweza kuwa ni kutokana na limbikizo la damu kwenye uterasi.

Mpe mama rufaa mara tu unapoona dalili zozote za hatari peleka mtoto pia.

1.5 Utakayofanya katika kipindi cha baada ya kuzaa 

1.5.2 Kumkagua mtoto mchanga