1.5.2 Kumkagua mtoto mchanga

Unapaswa kumkagua mtoto mchanga kwa dalili zifuatazo katika saa sita za kwanza:

Unyonyeshaji umeelezewa kikamilifu katika Kipindi cha 7 cha somo.

  • Unyonyaji haba: Watoto waliozaliwa kabla ya muda wa ujauzito kutimia, waliozaliwa na uzito wa chini, wenye asfiksia au walio wagonjwa kwa kawaida hawawezi kunyonya maziwa matitini vizuri. Unyonyaji huzidisha utengenezwaji wa maziwa. Kwa hivyo, usimpinge mama huyo kunyonyesha iwapo hatoi maziwa ya kutosha mwanzoni. Mwongezee maji na umhimize mtoto kunyonya.
  • Ugonjwa wa manjano kwa mtoto mchanga: Umanjano kwenye ngozi ya mtoto mchanga ni ishara kuwa anahitaji rufaa kupelekwa kwenye kituo cha afya au hospitalini mara moja iwapo umanjano huu utaanza katika saa 24 za kwanza au akiwa na umri wa majuma mawili.
  • Kiwango cha juu cha joto, kutapika mara kwa mara, fumbatio kuvimba au kutotoa kinyesi baada ya saa 24: Kiwango cha juu cha joto (kiwango cha joto sawa na au juu ya nyuzijoto 37.5), kutapika na dalili zingine za hatari huashiria kuwepo kwa maambukizi hatari na/au kizuizi mahali fulani katika ufereji wa utumbo.
  • Hipothemia: Hipothemia ni hali ambapo mtoto ni baridi ukimgusa au ana kiwango cha joto chini ya nyuzijoto 35. Mweke mtoto katika hali ambapo ngozi yake itagusana moja kwa moja na ya mama kisha uwafungie kwenye blanketi iliyo vuguvugu na uweke chepeo au shali kwenye kichwa cha mtoto. Wape rufaa mara moja iwapo kiwango cha joto cha mtoto hakitapanda kwa haraka hadi hali ya kawaida.
  • Matatizo ya kupumua: Mtoto huwa na matatizo ya kupumua iwapo anapumua pumzi 60 kwa dakika, kifua kikijivuta ndani (mbavu kujivuta ndani mtoto anapotweta kwa kutafuta pumzi), midomo kuwa na rangi ya samawati na/au kipimo cha mpigo wa moyo kikiwa juu ya mipigo 160 kwa dakika.
  • Kutokwa na damu kwenye kitovu au sehemu nyingine: Kitovu kinaweza kutoka damu iwapo hakikufungwa kwa kukazwa kabla ya kiungamwana kukatwa, au mtoto anaweza kutokwa na damu mkunduni, ambayo huashiria kupoteza kwa damu kutoka kwa tumbo au matumbo.
  • Vigubiko vyekundu vilivyovimba au kutokwa na usaha machoni: Ikiwa tayari umeyatibu macho ya mtoto kwa kutumia lihamu ya tetrasaiklini wakati wa kuzaliwa, mpe mama huyo na mtoto wake rufaa kwa utunzaji maalumu.

Uzuiaji wa hipothemia kwa kutumia ‘kanuni ya msisimko fululizi’ umeelezewa kikamilifu katika Kipindi cha 7 cha somo.

Kiasi kamili cha damu kwa mtoto mchanga mwenye uzani wa wastani ni milimita 240 pekee; hata kupoteza milimita 30 za damu kunatosha kusababisha mshtuko.

1.5.1 Kumkagua mama aliyezaa

1.5.3 Kufuatilia baada ya huduma ya mwanzoni mwa kipindi cha baada ya kuzaa