1.5.3 Kufuatilia baada ya huduma ya mwanzoni mwa kipindi cha baada ya kuzaa

Katika safari ya kwanza ya utunzaji baada ya kuzaa, unapaswa kukumbuka:

  • Kumshauri mama na mumewe/mwenziwe kuhusu upangaji uzazi, chanjo na unyonyeshaji jinsi utakavyojifunza baadaye katika moduli hii.
  • Kumpa miadi aje katika kituo chako cha afya au umtembelee nyumbani kwake baada ya siku tatu, sita na majuma sita (Picha 1.2) ikiwa kila kitu kinaendele kikawaida.
  • Kumpa miadi zaidi ya kumtembelea nyumbani kwake baada ya siku mbili ikiwa kuna matatizo yoyote ambayo hayajasababisha rufaa au iwapo mtoto alizaliwa kabla ya muda wa ujauzito kuisha, uzito wa chini au anaathiriwa na kiwango cha chini cha joto.

Watoto waliozaliwa kabla ya muda wa ujauzito kuisha na waliozaliwa na uzito wa chini ndio mada ya Kipindi cha 8 cha somo.

Picha 1.2 Uchunguzi katika kipindi cha baada ya kuzaa ni wakati mwafaka wa kuwashauri kina mama kuhusu chanjo na upangaji uzazi. (Picha: Hazina ya Dharura ya Watoto ya Umoja wa Mataifa/Indrias Getachew)

1.5.2 Kumkagua mtoto mchanga

1.6 Uhamasishaji wa jamii kuhusu utunzaji baada ya kuzaa