1.6.1 Mbinu za kuhamasisha utendaji wa jamii
Kisanduku 1.1 linatoa muhtasari wa mbinu kuu za uhamasishaji wa jamii. Hapa tunaziangazia kwa kifupi kwa sababu ushakumbana na mbinu zote katika moduli juu ya Elimu ya Afya, Utetezi na Uhamasishaji wa Jamii.
Kisanduku 1.1 Mbinu za uhamasishaji wa jamii
Mabango: Mabango yaliyobuniwa vizuri na kuwekwa mahali panapofaa yanaweza kuwasilisha jumbe ili kuwakumbusha watu mara kwa mara kuhusu suala husika.
Uandikaji barua: Hii ni njia moja ya kuwasilisha jumbe za kiafya kwa wanajamii wasomi. Barua hutoa ujumbe sahihi na inaweza kuwekwa ili kurejelewa baadaye.
Kurasa zenye vielelezo: Picha ni njia nzuri ya kufikisha ujumbe kwa watu wasioweza kuelewa barua kutokana na ujuzi wao haba wa kusoma(Picha1.3).
Kuwatembelewa nyumbani: Hii ndio njia bora zaidi ya kuihamasisha jamii kwa sababu unaweza kuwa na hakika kuwa ujumbe umewasilishwa.
Msingi wa uhamasishaji wa jamii ni kushiriki pakubwa kwa jamii ambako hufanyika wanajamii wanaposhiriki katika kutambua matatizo na mahitaji na kisha wapange, watekeleze, wasimamie na kutathmini shughuli za jamii ili kutatua tatizo hilo.
Kanuni ya kimsingi unayofaa kukumbuka ni kuwa hauko pale ‘kushurutisha’ ushiriki wa jamii. Wajibu wako ni kuchunguza, kujifunza kutoka kwa hekima ya jamii na kuelimisha na kuwarai wanajamii kuleta mabadiliko yatakikanayo - katika muktadha huu, kuboresha matokeo baada ya kuzaa. Neno na uamuzi wa mwisho huwa ya jamii.
1.6 Uhamasishaji wa jamii kuhusu utunzaji baada ya kuzaa