1.6.3 Kujenga ushirikiano na watu mashuhuri katika jamii

Watu wa kwanza kulenga kwa utunzaji wa baada ya kuzaa ni mama, mtoto wake mchanga na baba. Hata hivyo kuna watu wa kulenga baadaye ambao ni watu mashuhuri katika jamii wanaoweza kushawishi uamuzi unaoathiri afya ya mama na mtoto. Unahitaji kuwahusisha watu hawa kutoka mwanzo unapotanguliza huduma za utunzaji wa baada ya kuzaa katika jamii yako. Zingatia kuhusisha:

  • Wasimamizi rasmi wa kijiji
  • Viongozi wa kidini, vikundi vya makanisa au misikiti
  • Viongozi mashuhuri na wazee wa kijiji
  • Mashirika au vyama vya wanawake
  • Mashirika ya vijana
  • Kamati za kijamii katika eneo hilo
  • Mashirika ya wakulima au ya ukulima
  • Wakunga na madaktari wa kienyeji
  • Wanao uza dawa vijijini
  • Wengineo unaoweza kufikiria ni muhimu kwa hali maalumu.

Bila ushirikiano wa watu binafsi na vikundi hivi, itakuwa vigumu kutoa utunzaji bora baada ya kuzaa. Hasa ni muhimu kuimarisha uhusiano bora na upatanishe juhudi zako na za wakunga wa kienyeji. Shughuli zifuatazo zitakusaidia kutimiza haya (Kisanduku 1.2)

Kisanduku 1.2 Kujenga ushirikiano na wakunga wa kienyeji

  • Wasiliana na wakunga wa kienyeji katika jamii yako kisha mjadiliane jinsi ya kusaidiana katika kutoa utunzaji wa baada ya kuzaa kwa wanawake, watoto wachanga na familia. Kwa pamoja mnaweza kuibuka na maarifa mapya yaliyo mwafaka zaidi kwa mahali pale.
  • Heshimu maarifa, uzofeu, maoni na ushawishi wao. Waulize waeleze maarifa wanayoshiriki na jamii.
  • Shiriki nao habari kuhusu utunzaji wa baada ya kuzaa. Toa nakala za elimu ya afya ambazo ungependa kusambaza kwa wanajamii na ujadiliane nao yaliyomo.
  • Wahusishe katika vikao vya kutoa ushauri kwa familia na wanajamii wengine. Wajumuishe katika mikutano yako na viongozi wa jamii na vikundi mashuhuri.
  • Jadili pendekezo kuwa kila uzalishaji unafaa kufanywa na mhudumu mwenye ujuzi kama wewe. Iwapo hili haliwezekani au halipendelewi na mwanamke huyo na familia yake, jadili jinsi wakunga wa kienyeji wanavyoweza kutoa utunzaji bora zaidi wa baada ya kuzaa, na ni katika hali zipi wanapopaswa kutoa rufaa ya dharura mwanamke huyo aje kwako au aende katika kituo cha afya cha juu.
  • Hakikisha wakunga wa kienyeji wamejumuishwa katika utaratibu wa kutoa rufaa na uwape majibu kuhusu wanawake waliowatuma kwako.
  • Je, kwa nini unafikiri ni muhimu kuwahusisha wakunga na madaktari wa kienyejii jinsi ilivyoelezewa hapo awali?

  • Wao ni wambia muhimu kwa sababu wanajua desturi za mahali pale, wanaheshimiwa na wanajamii na wana uzoefu mwingi wa kukabiliana na mengi ya matatizo ya kijamii yanayotokea katika kipindi baada ya kuzaa.

    Mwisho wa jibu

  • Dhania kuwa wewe ni mkunga wa kienyenji mwenye uzoefu wa miaka mingi. Muhudumu wa afya nje ya hospitali anaanza kufanya kazi katika kijiji chako kisha aombe usaidizi wako. Je, ni mambo gani yanayoweza kukufanya uweze kushirikiana naye kusaidia kazi yake?

  • Kwa kweli jibu sahihi si moja tu kwa swali hili jinsi tu ilivyo kwamba majibu yote hayatamfaa mkunga mmoja kwa usawa. Hata hivyo huenda ulitaja pia yafuatayo:

    • Anakutendea vyema kwa heshima na kama mwenzi.
    • Anaonyesha moyo wa kupenda kujua kuhusu uzalishaji wa kienyeji katika kijiji chako.
    • Unaweza kuona kuwa anathamini maarifa na uzoefu wako.
    • Anakupa fursa ya kujifunza kuhusu mbinu mpya za kuzalisha.
    • Anakusihi uungane naye kama mbia katika juhudi za pamoja ili kuboresha utunzaji baada ya kuzaa kwa wanawake na watoto wachanga katika kijiji chako.
    • Anakualika katika mikutano yake na viongozi wa kijiji na watu wengine mashuhuri ili kuhamasisha jamii kuunga mkono huduma za utunzaji baada ya kuzaa.

    Mwisho wa jibu

1.6.2 Je, Kwa nini kushiriki kwa jamii ni muhimu sana?

1.7 Kukagua wasifu wa jamii