2.1.2 Seviksi

Mara tu baada ya kuzaa, kuta zenye misuli za seviksi hulegea, huwa nyembamba na zilizotanuka. Seviksi inaweza pia kuonekana iliyovimba na kuvilia kutokana na kuzaa. Pia inaweza kuwa na mikato midogo katika sehemu ambapo tishu iliraruka mtoto alipokuwa akizaliwa. Hata hivyo, seviksi kwa kawaida huwa imepungua na kurudi katika hali yake thabiti katika siku ya kwanza. Mwanya wa uke unafaa kuwa na kipenyo cha vidole viwili saa 24 baada ya kuzaa na kipenyo cha kidole kimoja ifikiapo mwisho wa juma la kwanza ukiuchunguza kwa kutumia mkono uliovishwa glavu.