2.1.4 Msamba

Msamba ni sehemu ya mwili iliyo kati ya mwanya wa uke na mwanya wa mkundu. Sehemu hii hutanuliwa na kujeruhiwa na wakati mwingine kuraruliwa katika kuzaa. Vile vile mkunga stadi anaweza kuukata kwa kukusudia kwa kutumia makasi yaliyotiwa kifisha vijidudu ili kuupanua mwanya na kumsaidia mtoto kutoka. Nyingi ya nguvu za misuli ya msamba hurejea katika muda wa majuma sita baada ya kuzaa na kuimarika zaidi katika miezi michache ifuatayo. Unaweza kumsaidia mama kurudisha nguvu za misuli kwa kumhimiza kukaza na kulegeza misuli ya msamba mara kumi mara tu anapoweza kufanya hivyo na kurudia zoezi hili mara kadhaa kila siku. Kuuimarisha msamba ni muhimu kwa sababu ndio unaotengeneza msingi wa kaviti ya pelvisi ambayo huhimili uterasi, uke na kibofu cha mkojo.

2.1.5 Ukuta wa fumbatio