2.1.6 Ovari

Ubadilikaji wa ovari na urudiaji hali yake ya kawaida ni wa kubadilika na huathiriwa pakubwa na unyonyeshaji wa mtoto huyo mchanga. Mwanamke anayemnyonyesha mtoto tu pasipo kumpa vyakula vingine vyovyote hukosa hedhi kwa kipindi kirefu na ovulesheni yake ya kwanza baada ya kuzaa huchelewa akilinganishwa na mama anayempa mtoto maziwa kwa chupa. Mwanamke asiyenyonyesha anaweza kutoa ova mapema kabisa kama vile majuma manne baada ya kuzaa na wengi wao hupata hedhi ifikiapo juma la kumi na mbili. Muda wa wastani kwa hedhi ya kwanza kwa mwanamke asiyenyonyesha ni majuma saba hadi tisa baada ya kuzaa.

Wakati wa kuanza kwa hedhi kwa mwanamke anayenyonyesha ni wa kubadilika sana na hutegemea vipengele kadhaa vikiwemo ni kwa kiasi kipi na ni mara ngapi mtoto huyo hulishwa, na ikiwa chakula hiki kimeongezwa maziwa bandia. Ovulesheni husitishwa kwa mwanamke anayenyonyesha na homoni itolewayo kwenye tezi ya pituitari iliyo ubongoni mtoto anaponyonya. Nusu hadi theluthi tatu za wanawake wanaowanyonyesha watoto wao pasipo kuwapa vyakula vingine vyovyote huanza kipindi chao cha kwanza cha hedhi katika majuma 36 baada ya kuzaa.

  • Je, ni ushauri upi unaoweza kumpa mama aliyezaa mara ya kwanza hivi karibuni na ananyonyesha akikuuliza anapoweza kuanza tena kushiriki ngono?

  • Unaweza kusema kuwa baada ya mchozo utokao ukeni (lokia) kukoma na kuwa wa rangi ya manjano hafifu (baada ya majuma matano hadi saba), anaweza kuanza tena kushiriki ngono ikiwa anahisi yuko tayari kimwili na kihisia. Unaweza pia kumweleza kuwa unyonyeshaji hufanya iwe vigumu kutabiri wakati atakapoanza kutoa ova tena. Pia, unaweza kumshauri kuwazia swala la upangaji uzazi kwa kufafanua hatari za ujauzito mwingine mara tu baada ya kuzaa na manufaa ya uzazi wa majira ya miaka miwili au zaidi.

    Mwisho wa jibu.

2.1.5 Ukuta wa fumbatio

2.1.7 Matiti na mwanzo wa utungaji wa maziwa