2.1.7 Matiti na mwanzo wa utungaji wa maziwa

Tukio jingine muhimu mara tu baada ya kuzaa ni mwanzo wa utungaji wa maziwa (kutengenezwa kwa kolostramu na kisha maziwa kwenye matiti) na kutolewa kwa viowevu hivi vyenye virutubishi mtoto anaponyonya chuchu ya mama. Matiti huanza kukuza uwezo wa kutengeneza maziwa ujauzito unapoendelea kukua kama mwitiko kwa homoni zinazozunguka katika damu ya mama. Kwa siku chache za kwanza baada ya kuzaa, matiti hutoa kolostramu (dutu yenye rangi ya malai). Kolostramu huwa na virutubishi vingi vya mtoto na pia antibodi za mama ambazo humkinga mtoto mchanga dhidi ya maambukizi. Kwa sababu hii, ni muhimu sana watoto wote walishwe kolostramu. Katika baadhi ya maeneo barani Afrika, tendo la kuwalisha watoto wachanga kolostramu linachukuliwa kuwa lisilo zuri na salama kiafya. Hata hivyo, jaribu kumshawishi mama huyo asiyatupe maziwa hayo hata akionekana mwenye kusita.

Antibodi ni protini maalumu zinazosaidia kutambua na kuharibu visababishi vya maambukizi.

Matiti huwa imara na kuanza kutoa maziwa siku tatu baada ya kuzaa kama mwitiko kwa mwongezeko wa homoni zitokazo kwenye tezi ya pituitari zinazochochea utengenezaji wa maziwa. Matiti hayo hufuka, huwa ngumu na yenye joto kwa haraka kutokana na ongezeko la damu, hali hii ya matiti huitwa kutuna, yaani, kuongezeka katika ukubwa wa ogani kutokana na mrundikano wa damu (Picha 2.2). Hali hii huendelea kwa muda wa takribani saa 24-48 na kisha kurudi katika hali yake ya kawaida kivyake. Baada ya haya, matiti kamwe si magumu na pia hayana joto bali huwa imara na laini yanavyojazwa maziwa kutoka safari moja ya unyonyeshaji hadi nyingine, na kuwa laini na kupungua katika ukubwa maziwa yanapoondolewa kupitia unyonyaji wa mtoto. Utengenezaji wa maziwa unaoendelea huchochewa na unyonyaji wa mtoto. Jinsi mtoto anyonyavyo ndivyo matiti yanavyoendelea kutengeneza maziwa.

Picha 2.2 Takribani siku tatu baada ya kuzaa, ukubwa wa matiti umeongezeka yanavyojazwa na maziwa kwa mara ya kwanza. (Picha:Hazina ya Dharura ya Watoto ya Umoja wa Mataifa)

Unapaswa kuwashauri kina mama waliozaa mara ya kwanza kuwa kuanza kunyonyesha mapema (katika saa moja baada ya kuzaa) na kumnyonyesha mtoto pasipo kumpa vyakula vingine vyovyote (mtoto asipewe vyakula wala viowevu vingine vyovyote) katika miezi sita ya kwanza ndio mwanzo mwema wa kilishe maishani. Mruhusu mtoto kunyonya kila anapotaka kula tangu siku ya kwanza na kuenedelea. Unyonyeshaji kamwe si rahisi wala haufanyiki tu wenyewe na huchukuwa muda mwingi kila siku mchana na pia usiku. Mama anahitaji nguvu nyingi kumnyonyesha mtoto wake kwa miezi sita bila kumpa chakula kingine chochote kile. Kutengeneza maziwa mengi yenye virutubishi vingi huhitaji nguvu nyingi za ziada. Mama huyu anahitaji virutubishi na viowevu zaidi. Kwa hivyo, mshauri anywe viowevu safi kwa wingi na ajaribu iwezekanavyo kula mlo zaidi kila siku katika muda wake wa kunyonyesha. Habari kamili kuhusu unyonyeshaji imeelezewa katika Kipindi cha 7 cha somo.

Ukomeshaji wa utungaji wa maziwa kwa wanawake wasionyonyesha

Kunazo hali ambapo mama hawezi au hatanyonyesha. Kwa mfano, ikiwa mtoto amezaliwa akiwa amefariki au akifariki katika majuma kadhaa ya kwanza, au mama anapostahabu kwa dhati kumlisha mtoto wake maziwa mbadala chupani, imependekezwa kuwa mwanamke huyo afungwe bendeji ya kubana katika kifua chake ikifunika matiti katika siku mbili hadi tatu za kwanza baada ya kuzaa ili kupunguza matatizo ya ukubwa unaoendelea wa matiti. Uangalifu unafaa kudumishwa ili matiti yasichochewe kwa njia yoyote ile kutengeneza maziwa. Vibonge vya barafu pia vinaweza kuwekwa kwenye matiti na mama kupewa dawa za kutuliza maumivu zilizo na aspirini au paracetamol ili kupunguza wepesi wa matiti kuumia.

2.1.8 Kuondolewa kwa viowevu vya mwili vya ziada