2.1.8 Kuondolewa kwa viowevu vya mwili vya ziada

Mwili wa mwanamke huwa na viowevu vingi wakati wa ujauzito kuliko wakati ambapo hana ujauzito. Kiasi fulani cha maji haya ya ziada huwa kwenye tishu zake, mengine kwenye damu yake iliyoongezeka na mengine kwenye uterasi. Maji haya ya ziada huondolewa haraka baada ya kuzaa. Guliguli aminio hutokea kwenye uke. Kutoka siku ya pili baada ya kuzaa, kiasi cha mkojo kitaongezeka kwa siku kadhaa hadi lita tatu kwa siku lakini hurudi katika mkondo wake wa kawaida katika muda wa juma moja. Nafasi ya kibofu huongezeka na kuwa na ujazo wa mililita 1,000 hadi 1,500 za mkojo bila matatizo katika kipindi ambapo viowevu huondolewa mwilini. Kutakuwa na ongezeko la hatari ya maambukizi kwenye mfumo wa mkojo iwapo mkojo utabakizwa kibofuni kwa kipindi kirefu kutokana na urethra kufunga na kuvimba au kujeruhiwa kwa tishu baada ya kuzaa.

Ulijifunza kuhusu maambukizi ya mfumo wa mkojo katika Kipindi cha 18 cha Moduli ya Utunzaji katika ujauzito.

2.1.7 Matiti na mwanzo wa utungaji wa maziwa

2.2 Habari muhimu kwa kina mama waliozaa mara ya kwanza