2.2 Habari muhimu kwa kina mama waliozaa mara ya kwanza

2.2.1 Kumtunza mtoto

Kina mama waliozaa kwa mara ya kwanza (na mara nyingi hata kina baba wa mara ya kwanza) wanafaa kufunzwa utaratibu wa kumtunza mtoto ukiwemo kumuogesha na kudumisha usafi wa mwili na nguo zake kutokana na kinyesi na mkojo. Wafundishe wazazi hawa wanachoweza kutarajia kutoka kwa mtoto kwa mujibu wa kulala, kukojoa, mwenendo wa matumbo, kula, na kulia. Sharti joto lidumishwe kwa mtoto. Hata hivyo, asifungwe kwa kukazwa. Anafaa kuchunguzwa kwa uangalifu mara kwa mara ili kuhakikisha kuwa hana baridi au joto jingi na anakula vizuri na kutoa kinyesi na mkojo wa kawaida mara kwa mara. Mengi kuhusu utunzaji wa mtoto mchanga yameangaziwa baadaye kwenye Moduli hii katika Kipindi cha 6 hadi cha 8 cha somo.

2.1.8 Kuondolewa kwa viowevu vya mwili vya ziada

2.2.2 Kupumzika na kupona kwa mama