2.2.2 Kupumzika na kupona kwa mama

Ujauzito, uchungu wa kuzaa, kuzaa na utunzaji wa mtoto mchanga ni matukio yachokeshayo na yasababishayo mfadhaiko. Kwa hivyo, mama anahitaji pumziko la kutosha ndiposa apone. Pia, anahitaji habari kuhusu wakati mwafaka anapoweza kurejelea shughuli zake za kawaida. Mwambie kuwa anaweza kuanza tena kufanya baadhi ya shughuli za nyumbani katika siku mbili au tatu za kwanza baada ya kuzaa mradi hahisi uchungu au matatizo yoyote. Msingi wa kurejelea shughuli za kawaida si kufanya kazi kwa siku moja kiasi kwamba ajihisi mchovu kabisa siku itakayofuata.

2.2 Habari muhimu kwa kina mama waliozaa mara ya kwanza

2.2.3 Mbinu za kudhibiti uzazi