2.2.3 Mbinu za kudhibiti uzazi

Mama pamoja na mwenzi wake wanapaswa kupewa ushauri kuhusu mbinu tofauti za kudhibiti uzazi. Huenda asiwe tayari kuamua mbinu yoyote lakini anafaa kuzijua mbinu tofauti zilizoko. Uamuzi wake utategemea vipengele kadhaa vikiwemo sababu za kutumia mbinu fulani, idadi ya watoto alionao na ikiwa ananyonyesha.

Kunazo mbinu nyingi tutakazozitaja kwa kifupi tu. Mbinu hizi zimeelezewa zaidi katika Moduli ya Upangaji uzazi.

  • Mbinu za kiasili zinahusisha kuchunguza hali ya kamasi la seviksi (ubora na kiasi). Hii inaweza kutumiwa vyema ili kuonyesha wakati ambapo mwanamke anatoa ova (ovulesheni). Hata hivyo, si njia mwafaka ya kuzuia ujauzito.
  • Kumnyonyesha mtoto bila kumpa vyakula vingine vyovyote na kumnyonyesha kila anapotaka kunaweza kutoa kinga dhabiti dhidi ya ujauzito kwa muda wa hadi miezi sita iwapo vipindi vya hedhi vya mwanamke huyu havijarejea.

  • Mbinu za kutumia vizuizi kwa uzuiaji ujauzito hutengeneza kizuizi kati ya mbegu ya kiume na uke au seviksi. Mbinu ya vizuizi inayotumika sana ni utumiaji wa kondomu za wanaume ambazo zinapatikana kote.
  • Mbinu za homoni za uzuiaji ujauzito ni tembe za kuzuia mimba, dawa za kuzuia ujauzito zinazoingizwa kwa sindano na vipandikizi (chuma kidogo sana kinachowekwa chini ya ngozi kilicho na homoni zinazotoka polepole ).
  • Vifaa vya kuzuia ujauzito vitiwavyo ndani ya uterasi hutiwa hapo ili kuzuia upandikizi wa kiinitete. Vinaweza kuwekwa mwishoni mwa puperiamu.
  • Mbinu za kudumu za kudhibiti uzazi ni kukata na kufunga mishipa ya falopio (inayotoka kwenye uterasi katika pande zote mbili ikielekea kwenye ovari) kwa wanawake na kukata mishipa inayosafirisha mbegu ya kiume kutoka kwa kende hadi kwa dhakari (vasektomi).
  • Bila kutazama nyuma katika sehemu zilizo hapo juu, jiandikie muhtasari mfupi wa hoja kuu utakazowaambia wazazi wa watoto wachanga ukiwashauri kuhusu jinsi ya kumtunza mtoto wao.

  • Sasa linganisha orodha yako na habari iliyo kwenye sehemu ya 2.2.1, 2.2.2 na 2.2.3Mwisho wa jibu.

2.2.2 Kupumzika na kupona kwa mama

2.3 Kwa kutamatisha