Muhtasari wa Kipindi cha 2

Katika Kipindi hiki cha somo umejifunza kuwa:

  1. Kipindi cha wiki sita baada ya kuzaa huitwa puperiamu. Huu ni wakati ambapo mabadiliko ya kifiziolojia yaliyotendeka kwa mwili wa mama wakati wa ujauzito hurudi katika hali ya kawaida. Uterasi, seviksi, uke na vulva hupungua kwa ukubwa na viowevu zaidi vilivyobakizwa wakati wa ujauzito huondolewa haraka kupitia katika mkojo wa mama.
  2. Kina mama baaada ya kuzaa wana mchozo wa kawaida ambao ni mwekundu na majimaji uitwao lokia ambao hupungua pole pole wakati wa puperiamu na kubadilika rangi kuwa manjano hafifu.
  3. Mabadiliko kwa matiti ambayo huyatayarisha kwa unyonyeshaji hutokea katika muda wote wa ujauzito. Utengenezaji wa kolostramu huanza mara tu baada ya kuzaa na hufuatwa siku 3 baadaye na kutuna kwa matiti na utengenezaji wa maziwa halisi.
  4. Kolostramu inayotolewa kwa matiti katika siku mbili hadi tatu za kwanza baada ya kuzaa ina virutubishi na antibodi za mama. Ni lazima mtoto mchanga alishwe kolostramu hii.
  5. Unyonyeshaji unafaa kuanza katika saa ya kwanza baada ya kuzaa na kuendelea bila kumpa mtoto chakula kikingine chochote na kumnyonyesha kila anapotaka kwa miezi sita ya kwanza.
  6. Kina mama (na mara nyingine kina baba) huhitaji kusaidiwa ili kujizoesha na mahitaji ya kumtunza mtoto mchanga ukiwemo usaidizi wa kuanza kunyonyesha na kudumisha joto na usafi wa mtoto. Kina mama huhitaji muda wa kupumzika na kupata nafuu kabla ya kurejelea shughuli zao za kawaida.
  7. Mbinu tofauti zinazoweza kutumika katika upangaji wa uzazi baada ya kuzaa sharti zijadiliwe na wazazi wote wawili.

Maswali ya kujitathmini ya Kipindi cha 2 Kwa kuwa umetamatisha Kipindi hiki, jibu maswali haya ili kujitathmini ulivyosoma.