Maswali ya kujitathmini ya Kipindi cha 2 Kwa kuwa umetamatisha Kipindi hiki, jibu maswali haya ili kujitathmini ulivyosoma.

Swali la kujitathmini 2.1 (linatathmini Lengo la Somo la 2.1)

Je, ni ipi kati ya kauli hizi isiyo sahihi? Kwa kila kauli, (i) eleza kisicho sahihi na (ii) fafanua neno lililoandikwa kwa herufi nzito.

  • A.Mwanamke wakati wa puperiamu hatatoa lokia kikawaida baada ya kuzaa.
  • B.Mwanzo wa utengenezaji wa maziwa na kolostramu hufuata mara tu baada ya kuzaa mtoto.
  • C.Utunaji wa matiti ni ishara kwamba unyonyeshaji unaweza kuanza.
  • D.Endometriamu inaweza kuchukua wiki 7 ili kupona baada ya kuzaa.

Answer

  • A.Si sahihi: wanawake wote baada ya kuzaa watakuwa na mchozo ulio majimaji na wenye rangi (lokia) kwa muda wa takribani majuma matano baada ya kuzaa. Huu ni takribani muda sawa na ule wa puperiamu ambao ni kipindi cha mabadiliko ya kifiziolojia yanayotokea katika majuma matatu hadi sita baada ya kuzaa.
  • B.Sahihi: kuanza kwa utengenezaji wa maziwa – yaani, utengenezaji wa kolostramu (‘maziwa ya kwanza’ ambayo ni malai na ya manjano na huwa na virutubishi na antibodi za mama) hufuata wenyewe mara tu baada ya kuzaa na kisha maziwa halisi kuanza baada ya takribani siku tatu.
  • C.Si sahihi kabisa: utunaji wa matiti ni mwitiko wa mwanzo wa utoaji wa maziwa na kwa kawaida hutendeka takribani siku tatu baada ya kuzaa. Kina mama wanahimizwa kuanza kunyonyesha katika saa moja ya kwanza baada ya kuzaa.
  • D.Si sahihi: endometriamu (ambayo ni bitana ya ndani ya uterasi) hupona haraka na ifikiapo siku ya saba huwa imerudi katika hali yake ya kawaida isipokuwa sehemu ya kondo.

Mwisho wa jibu

Swali la kujitathmini 2.2 (linatathmini Malengo ya Somo la 2.2 na 2.3)

Unamhudumia mwanamke aliyezaa mtoto wake wa pili siku 14 zilizopita. Mwanamke huyu anaonekana kuwa mwenye afya lakini mwenye wasiwasi kidogo. Eleza kwa ufupi vipimo vyote utakavyofanya kuhakikisha kuwa kila kitu kiko sawa na anapata nafuu kikawaida.

Answer

Kuna vipimo vingi unavyoweza kufanya - hivi ni baadhi ya vile vikuu.

  • Kwa kutomasa chini ya kitovu cha mwanamke unaweza kubainisha ikiwa uterasi imerudi katika hali yake ya kawaida.
  • Muulize ikiwa ana mchozo mwingi utokao ukeni na ni wa rangi gani.
  • Kwa kufanya uchunguzi ukeni, baini kuwa upana wa mwanya wa sevikisi umepungua hadi chini ya upana wa kidole kimoja.
  • Chunguza ikiwa uvimbe wa uke na vulva unapungua au u karibu kuisha.
  • Ikiwa msamba ulikatwa au uliraruka wakati wa kuzaaa, hakikisha unapona sawasawa, na ikiwa ni hivyo, mhimize mama kuanza kufanya mazoezi ya misuli yake ya msamba.
  • Chunguza ikiwa anayo matatizo katika kunyonyesha au (iwapo ameamua kutonyonyesha) anafanikiwa katika kupunguza utengenezaji wa maziwa.
  • Chunguza kuwa mtoto si baridi wala mwenye joto sana, anakula vizuri na anakunya mara kwa mara.
  • Uliza kwa hekima ikiwa mama huyo anahisi kushurutishwa na mwenzi wake kurejelea ngono kabla hajahisi kuwa tayari kufanya hivyo.
  • Jaribu kutathmini ikiwa amerejelea kazi nyingi mapema isivyotarajiwa.
  • Kwa kuukagua mwili wake, utatambua dalili kuu zitakazokufahamisha ikiwa puperiamu inaendelea kikawaida, na ikiwa ni hivyo, unaweza kumwondolea shaka mama huyo mwenye wasi wasi. Yale atakayoweza kusema kama majibu ya maswali ya kibinafsi yatakuwa magumu sana kutathmini. Utahitaji kutumia hisia zako na hekima ili kubainisha ikiwa kuna kitu kingine kinachoenda mrama.

Mwisho wa jibu.

Muhtasari wa Kipindi cha 2