3.1.1 Visababishi vya kuvuja damu iliyochelewa baada ya kuzaa

Kwa kawaida kutokwa na damu husababishwa na mikazo duni ya uterasi baada ya kuzaa, ambayo hushindwa kufunga kapilari iliyoraruka mahali ambapo plasenta ilivutwa nje. Iwapo uterasi haipungui kwa unene wake wa kawaida, inaweza kuwa ni kwa sababu ya maambukizi, au uzuiaji wa kipande cha plasenta, ambayo baadaye huraruka na kuwachana na kuta ya uterasi na kusababisha uvujaji damu. Kisanduku 3.1 linaeleza kwa muhtasari sababu za kawaida za kutokwa na damu uliochelewa baada ya kuzaa.

Ikiwa kawaida kuna uvujaji wa damu nyingi ukeni, au unashuku kuwa kuna uvujaji wa damu nyingi ndani ya mwili, rufaa mama hospitalini au kwa kituo cha afya iliyoko karibu yenye huduma ya kuongeza damu mwilini.

Kisanduku 3.1 Visababishi vya kutokwa na damu iliyochelewa baada ya kuzaa

  • Maambukizi ya ukuta wa endometria: Endometritisi imeelezwa katika Sehemu ya 3.2.1. Wakati eneo la plasenta bado halijapona, maambukizi katika uterasi inaweza kusababisha kapilari katika eneo la plasenta zianze kutokwa na damu tena.
  • Uterasi yenye mikazo duni: Uterasi inaweza kukosa mikazo yanayotarajiwa kwa sababu ya maambukizi, vipande vya plasenta vilivyobaki, au kwa sababu isiyojulikana. Kama hivyo, uvujaji damu unaweza kuanza tena.
  • Plasenta iliyobaki: Mabaki ya tishu ya plasenta au tando za fetasi yaliyobaki katika uterasi ndizo visababishi vya kawaida vya kutokwa kwa damu iliyochelewa baada ya kuzaa.
  • Kutengana kwa sehemu ya plasenta: Kuna uwezekano kwamba sehemu ya plasenta iliyopona hutengana na kufungua kapilari ya damu tena.
  • Ujauzito isiyo kuwa ya kawaida: Ingawa sio kawaida kwa mwanamke kupata ujauzito isiyo kuwa ya kawaida, matokeo yake inaweza kuwa na matatizo ya kutisha maisha; kumea kasi kwa kwa tishu kama zabibu katika uterasi inaweza kusababisha kutokwa na damu nyingi.

3.1 Kuvuja damu baada ya kuzaa

3.1.2 Rufaa kabla ya kudhibiti uvujaji damu baada ya kuzaa