3.1.2 Rufaa kabla ya kudhibiti uvujaji damu baada ya kuzaa

Kumbuka kwamba kiasi chochote cha damu kinachotoka ukeni baada ya masaa 24 (ya wakati huo au nyekundu sana) inaweza kuwa imesababishwa na mojawapo ya yale yalioorodheshwa katika Kisanduku 3.1, au zingine zisizotajwa. Hivyo basi, unapaswa kurufaa wanawake wanaovuja damu hospitalini bila kujali kiasi cha damu kinachotoka. Kumbuka pia kuongezwa damu pekee ndiyo njia inayoweza kuokoa maisha ya mama, Ikiwa anavuja damu sana.

Udhibiti ulioelezwa kwa kina zaidi kuhusu kutokwa na damu baada ya kuzaa ulifunzwa katika Kipindi cha 11 cha Moduli ya Utunzaji wa Leba na kuzaa na kimeelezwa katika Kipindi cha 22 cha Moduli ya Utunzaji katika Ujauzito, kama vile katika tajriba yako.

  • Je, vipindi hivi vya masomo vimekufunza nini kabla ya kurufaa wanawake wanaovuja damu baada ya kuzaa?

  • Mchoro 3.2 Mdungiye 10 IU ya oxytocin (au umpatie mikrogramu 400 za misoprostol) kabla kurufaa mwanamke anayevuja damu baada ya kuzaa.

    Weka laini dawa ya kudungia mshipa, na umwanzishe na tiba ya kumwingiza dawa ndani ya mshipa kwa kutumia Ringer’s Lactate au Saline ya kawaida, ukitumia ml 1,000 (lita-1) ya mfuko na kiwango cha mtiririko kilichowekwa kitiririke haraka iwezekanavyo.

    Mwisho wa jibu

Kama tiba ya kabla rufaa, pia mpe dozi ya pili ya misoprostol (mikrogramu 400 mdomoni au kupitia rektamu), au 10 IU oxytocin kwa sindano ya ndani ya misuli (Mchoro 3.2).

3.1.1 Visababishi vya kuvuja damu iliyochelewa baada ya kuzaa

3.2 Sepsisi inayosababishwa na uzazi na joto jingi mwilini