3.2.1 Endometritisi

Endometritisi ni mchakato wa maambukizi inayoshirikisha ukuta wa ndani ya uterasi (endometria). Kwa kawaida inasababishwa na bakteria kupanda juu kutoka ukeni, au bakteria iliyohamishwa kutoka kwa rektamu na mkundu hadi mfumo wa uzazi. Sababu zinazojulikana na zinazoweza kuzuiwa zinazochangia hatari ya endometrisi ni pamoja na:

Kupasuka kwa Tando Kabla ya Wakati ni mada ya Kipindi cha 17 cha Moduli ya Utunzaji katika ujauzito.

  • Leba ya muda mrefu: Hatari hii inaweza kudhibitiwa kwa kurufaa wanawake walio katika leba iliyochukuwa muda mrefu.
  • Kupasuka kwa Tando kabla ya Wakati na iliyochukuwa muda mrefu: Hatari ni kubwa iwapo Kupasuka kwa Tando kabla ya imetokea muda mrefu Kabla mtoto hajazaliwa. Unaweza kupunguza hatari kwa kurufaa haraka.
  • Uchunguzi wa mara kwa mara wa ukeni: Unaweza kuepukana na hatari hii kwa kukosa kutekeleza uchunguzi wa ndani isiyohitajika.
  • Hali duni ya elimusiha na usafi wakati wa kuzalisha: Kwa mfano, kuingiza mkono mchafu ukeni, au kutumia vyombo vilivyo na vimelea, vinaweza kusambaza maambukizi.
  • Maambukizi yaliokuwa: Maambukizi ukeni na uterasi kutokana na magonjwa ya zinaa au kwa mfumo wa mkojo.
  • Mabaki ya plasenta au tando za fetasi: Seli zilizokufa katika tishu hizi huchangia kuongezeka kwa bakteria.
  • Kutoa plasenta kwa kutumia mikono: Kambakitovi ikikatika ukivuta polepole ili kusaidia kutoa plasenta, inaweza kubakia na mwanamke huweza kuvuja damu nyingi. Katika hali hizi, utalazimika kutoa kwa kuingiza vidole ndani ya pengo la endometria, kutambua plasenta, na kuitoa vipande vipande au mzima. zaidi ya hatari kwa mama kutokana na kuvuja damu, kuna hatari pia za maambukizi za endomeria.
Mchoro 3.4 Maumivu kwa fumbatio yanaweza kuwa dalili ya endometritisi.
  • Anemia: Hatari inayojulikana ya endometiritisi na aina zingine za maambukizi ya pupera, anemia inaweza kusababishwa na upungufu wa damu wakati wa ujauzito, leba, au kuzaa, au kwa matatizo ya lishe.
  • Jeraha la kuzalisha: (kwa mfano, kwa kutumia koleo, au kwa operesheni ya kisu)
  • Kutokwa na damu iliyochelewa baada ya kuzaa.

Magonjwa ya zinaa yameelezwa katika Kipindi cha 31 katika Moduli ya Magonjwa Ambukizi; Maambukizi kwa mfumo wa mkojo yamejadiliwa katika Kipindi cha 18 cha Moduli ya Utunzaji katika ujauzito

Dalili za endomentritisi

Mwanamke aliye na endometritisi kwa kawaida huwa na homa ya Sentigredi 38° au zaidi, mpigo wa kasi wa mshipa, na maumivu (maumivu unapoguswa) unapogusa fumbatio (Mchoro 3.4). Baadhi ya wanawake wanaweza kupata mchozo iliyoganda inayoonekana kama maziwa ya rangi ya manjano iliyo na harufu mbaya kutoka ukeni, ambapo wengine huwa na mchozo kiasi kisichokuwa na harufu. Kwa ufupi, kumkagua mama kwa maambukizi ya uterasi, muulize kama ana:

  • Historia ya joto jingi mwilini au iwapo anahisi joto. Mpime joto lake na ikiwa ni sawa au zaidi ya Sentigredi 38, basi ana joto jingi mwilini.
  • Maumivu katika sehemu ya chini ya fumbatio.
  • Harufu mbaya, mchozo unaoonekana kama maziwa yalio ganda kutoka ukeni.

Iwapo mama ana mojawapo ya matokeo yaliyotajwa hapo awali, uchukulie kwamba ana endometritisi na umpatie rufaa ya haraka hospitalini au kwa kituo cha afya kilichokaribu.

Iwapo utashuku mama wakati wa puperiamu kuwa ana endometritisi unapofanya ziara yako, ni muhimu kumrufaa haraka kwa matibabu zaidi. Ikiwa ana shinikizo la chini la damu (diastoli chini ya mililita 60 ya zebaki), unaweza kuanza uamishaji wa Saline ya kawaidakwa mishipa. Mweke alale chali miguu yake yakiwa yameinuka kwa kuweka mito chini ya magoti yake (mtindo wa mstuko), kabla ya kumpeleka kwa kituo cha afya.

  • Ni hatari zipi za ukuaji wa endometritisi, unaweza kutekeleza, wewe binafsi?

  • Kuhakikisha viwango vya juu vya elimusiha na usafi wakati wa kuzaa; na kujiepusha, iwezekanavyo, na urudiaji wa uchunguzi ukeni mwa mama.

    Mwisho wa jibu

3.2 Sepsisi inayosababishwa na uzazi na joto jingi mwilini

3.2.2 Maambukizi kwa mfumo wa mkojo