3.2.2 Maambukizi kwa mfumo wa mkojo

Sababu nyingine ya kawaida ya maumivu na joto jingi mwilini wakati wa puperiamu ni maambukizi ya mfumo wa mkojo. Mwanamke mwenye Maambukizi ya Mfumo wa Mkojo hulalamika mkojo hutoka kila mara, anahisi akichomeka anapokojoa, na hamu ya kukojoa mara kwa mara. Unapofinya fumbatio lake juu ya pelvisi, anahisi uchungu. Mwanamke huyu anahitaji rufaa ili atibiwe na antibiotiki.

Maambukizi ya Mfumo wa Mkojo ni kawaida wakati wa ujauzito na puperiamu kwa sababu ya:

  • Kufungwa kwa mkojo kwa ajili ya kizuizi kwa mfumo wa mkojo katika baadhi ya wajawazito wakati wa kipindi cha mwisho cha ujauzito.
  • Msongamano wa mifupa na jeraha kwa urethra wakati wa leba na wa kuzaa, ambayo huongeza hatari ya bakteria kutoka kwa mfumo wa kuzalisha na rektamu kwenda juu na kuingia ndani ya kibofu na kutoka hapo hadi kwa figo.

3.2.3 Mastitisi ya pupera